Huyu mkuu wetu wa shule vipi?

Huyu mkuu wetu wa shule vipi?

Habari za blue Monday wanajamvi!

Naenda kwenye mada, nikiwa kama mwanafunzi wa kawaida kabisa katika shule yetu iliyopo huku kijijini nashangazwa sana na huyu kiongozi wetu wa shule; amekua sio mtu wa kuwaacha aliowagawia madaraka watekeleze wajibu wao kama ilivyo kwa shule nyingine nilizowahi kusoma kwakua hapa nimehamia kutoka shule nyingine.

Kiukweli nakuta kama mkuu wa shule hii anatufanya tumzoee mno kiasi kwamba tunakua hatuna hamu nae ya kuweka umakini mkubwa siku akitaka kuzungumza ili tutake kujua ana mpya gani leo! Binafsi sioni kama ni sahihi kwake kufanya hivo,tunatakiwa tummic bhana sasa wanafunzi wakipiga kelele anakuja kutuliza yeye, vitabu vipya vikiletwa anaenda kupokea yeye,wachelewaji anakamata yeye na adhabu zote anataka atoe yeye jamaniii...

Naombeni kuuliza labda nawaza vibaya,au huu ndo uwajibikaji unaotakiwa? Nadhani tunamzoea mno kiasi kwamba akitaka kutupa ujumbe hata kama ni muhimu tutachukulia poa tu na kumwona wa kawaida sana.

Nakumbuka baadhi ya shule nilizowahi kusoma mkuu wa shule kumwona ni nadra,kwanza sijui uwe na ishu nzito kiasi gani mpaka ufike kwake yaani inamaana hawa wengine wote wameshindwa kutekeleza ni ngumu mno! Hadi inapofikia siku anataka kuongea wanafunzi wote tulikua tunaweka attention kubwa kutaka kujua leo kuna jambo gani zito.

Daaah! Naomba niishie hapa,natamani kama ujumbe wangu ungemfikia walau awe anajichimbia kidogo awaache walimu wengine wawajibike yeye awafuatilie kwa karibu hao na kwetu aje baada ya muda fulani walau tupate kamuda kakummic.

Wasaalam,
Mhembejr.

Ujumbe utamfikia mkuu wako wa shule, ila tatizo lake anajiona kisiki cha mpingo aseeee, haambiliki kwa lolote...Pia ashajiona yeye ni bora zaidi ya malaika ndio maana akifa anataka akawaongoze malaika wengine huko mbinguni, hata Gabriel atakuwa chini yake.....

Unawezaje kubadilisha rangi ya jiwe la mtoni?
 
Hama shule tu mkuu mbona simpo sana?

Nenda kwingine, maisha yenyewe mafupi afu mkuu wa shule akuzingue inakuwaje wafikiri,? Ebo
Daaah! Tatizo shule bado naipenda,iko vzr tu sema tu mkuu wa shule ndo anazingua
 
Mbona maelezo yanaonesha hawajamfuatilia katika upokeaji ada/pesa za wanafunzi?Mwalimu mkuu,atubu!
Enheee! Nashukuru kukumbushia hili mkuu! Ada zimekua siri na zinatumika kadri apendavyo,michango nayo imekua mingi Mara walinzi,nembo,mitihani,tahadhari nk ila hatujui inatumikaje mpaka mambo yanakwama sometimes.
 
Wanafunzi hamtosheki nyie hamjui.nn mnataka na akijichimbia ofcn mnasema hawajibiki....
Tumemzoea mno mkuu! Kama ugali wetu maharage tunaokula hapa kila siku,walau aje Mara moja moja basi
 
Hamia Kenya sekondary school au Uganda secondary school. Hizo shule zinajitahid kidogo.
 
Mkuu wa shule hutaki wanafunzi kumsumbuasumbua, ukizingua unapewa suspension ya moja kwa moja
Bora bodi ya shule ingehusishwa katika suspension hizo,na sio suspension in such anawasuspend kabisa wanafunzi hata kwa makosa madogo tu na hakuna wa kumuuliza na hachukuliwi hatua sijui kwann!
 
Back
Top Bottom