Mchumba wangu wa kike anauza duka maeneo flani hapa mjini.
Ni wiki mbili tu tangu nilipomtambulisha kwa wazazi.
Jana saa saba na dakika 10 mchana nikamtumia meseji ya kawaida, hakujibu.
Ilipofika saa saba na dakika 33 nikawa na wasi wasi ikabidi nimpigie simu.
Nikapiga mara ya kwanza kimya. Nikatulia dakika 3 zikapita nikapiga tena kimya.
Baada ya dakika kama 5 akanipigia. Kwa hasira sikupokea simu. Akatuma meseji eti sory mpenzi nilienda kununua chakula.
Mmh sikuridhika na sababu yake hiyo maana sikutegemea kama ataacha duka aende kununua chakula zaidi ya dakika 20.
Akaendelea kunitext na kupiga nikakaa kimya. Usiku ikabidi nipokee simu yake, tuliiashia kulaumiana bila muafaka.
Hadi muda huu napoandika hajanitumia SMS wala kupiga tangu jana usiku. Na mimi nimeamua kukaa kimya.
Sasa najiuliza, huyu mchumba vipi? Anafaa kweli? Na nshamtambulisha sasa. Najiuliza nimchukulie hatua gani bila majibu.
Fikiri Kwanza Chukua Hatua Haki Elimu Ngwaaaa Ngwaa!



nimekupendaNimependa tu jibu la kama anafaa au hafai analog mwenyewe.ha ha ha atakomaUliisi hakujibu sababu gani labda?
Umempeleka hadi kwenu means umeridhika nae na umeona anakufaa
Kuna muda kukosa trust kwa mwenzio kunaweza kuvunja uhusiano kirahisi tu
Sababu ya wewe na yeye kulaumiana sio ya msingi kabisa
Na jibu la anafaa ama lah unalo wewe muoaji
Pambana!
Hahahahaaaa... Mkuu hiyo ngwa ngwaa ni kengele ya msisitizo?Fikiri Kwanza Chukua Hatua Haki Elimu Ngwaaaa Ngwaa!
hahahahah emotional disorder.....!!!!!Emotional, and perception disorder,
Uliisi hakujibu sababu gani labda?
Umempeleka hadi kwenu means umeridhika nae na umeona anakufaa
Kuna muda kukosa trust kwa mwenzio kunaweza kuvunja uhusiano kirahisi tu
Sababu ya wewe na yeye kulaumiana sio ya msingi kabisa
Na jibu la anafaa ama lah unalo wewe muoaji
Pambana!
Sawa mkuu. Nitayafanyia kazi hayaMpendwa Yello Masai,
Pole kwa mkasa uliokupata, kwanza unatakiwa ujiulize je duka analouza mpenzi wako ni la jumla au rejareja? anauza bidhaa gani? Je anapata faida yeyote? katika hiyo siku alipata shoti au mahesabu yalikuwa sawa. Inategemea labda TRA walipita katika hilo eneo hilo, kwanini ashindwe kujibu hiyo meseji na kupokea simu kwa wakati?
Fanya huo utafiti halafu utaniambia mwenyewe.
Nakutakia siku njema.