Mchekeshaji Andrew Ngonyani maarufu Braza K, amelikosoa Bunge akilitaja kuongoza kwa utoaji wa taarifa pasipo mpangilio wala utaratibu kuliko bunge zote ambazo amewahi kuzishudia akiomba mabadiliko, zaidi wampe mualiko ili awasilishe hoja hiyo Bungeni.
"Tokea nimeanza kuona Mabunge, hili linaongoza kwa taarifa. Mtu anaongea kidogo 'taarifa mheshimiwa' yaani ni taarifa taarifa mpaka lini jamani? ebu jadilini vitu vya msingi acheni mtu aongee" amesema