Huyu Dk Bana katumwa na nani?

Mimi nashangaa sana kwa nini vyombo vya habari vinapenda sana kusikia kauli za huyu Dr. Banna inapotokea issue yoyote ya kisiasa? Si magazet, si television, utamwona tu Dr. Banna pale na maoni yake. Na siku zote maoni yake ni pro-ccm na anti-chadema. Lakini hayo yote yanachangiwa na wanataaluma wetu wa vyuo vikuu vyetu vikongwe kuendelea kuitegemea serikali kwa mishahara yao na kwa karibu kila kitu. UDSM kwa umri ulio nao ilipaswa kuwa inajitegemea sana kifedha na kujigharamia project kubwa muhimu za utafiti. Lakini ilivyo sasa vyanzo vya mapato pale hasa kule kwenye department za political, social sciences na sheria wanategemea fedha ya serikali kupitia kwenye consultancies fulani fulani za kiserikali. Na serikali si ya ccm? Sasa hapo ndo unawaona akina Banna wanakuja upfront kwenye vyombo vya habari na matokeo yake tunayaona. Yaani kuisifia CCM kwa kwenda mbele na kuikandia chadema kisawasawa.

Department zisizojihusisha na masuala ya kisiasa pale UDSM masikini zimetelekezwa kweli kweli pale. Kila project kubwa zinazohitajika kufanyiwa kazi hazipati hela yoyote serikalini maana hawana chochote cha kurudisha serikalini kwa mfumo wa kuisifia ccm. Hivyo huwezi kumwona professa yeyote wa biology, physics, chemistry au medicine akikaribishwa kujimwaga mwaga mbele ya vyombo vya habari kuelezea matokeo ya utafiti fulani wa science yake na impact yake kwa jamii ya watanzania. Upande wa serikali wana makosa kutothamini michango ya wanasayansi hapa nchini lakini pia na vyombo vya habari vinakosea kuwaalika hawa madokta vibaraka vya wanasiasa. Tumechoka siasa za ccm sisi .
 
Kwa taarifa tuu, Prof. Palamagamba Kabudi, ndie mwanafunzi pekee, wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, aliyewahi kupata GPA ya juu zaidi tangu chuo kikuu cha Dar es Salaam kuanzishwa miaka 50 iliyopita, yeye alipata GPA 4.8 ambayo haikuweza kupatikana tena na mtihani wa mwisho, alifumua A+ 6, A ya kawaida 1 na B+ moja!. Hivyo Ph.D yake ni ya halali!.

Kupata 1st class ni jambo moja, kuwa na Ph.D ni jambo jingine, lakine kuwa mzuri kwenye field, ni jambo jingine kabisa. Nimrod Mkono, ana pass tuu lakini ndie anaemiliki kampuni kubwa na tajiri kuliko zote za uwakili Tanzania, wakati huyo Kabudi, na 1st Class yake, na Ph.D yake, hajawahi kusimama mahakamani na kushinda kesi yoyote!.

Prof. Issa Shivji ni mmoja wa mabingwa wa katiba, na ameandika mengi kuhusu katiba ikiwemo ukosoaji wa katiba yetu ya mwaka 1977 na jinsi Muungano ulivyokiuka katiba.
u r right
 
usipoteze muda wako kumsikiliza huyu jamaa. hao waliomtuma waache wawe wanamsikiliza yeye. hizi njaa hazina adabu. jamaa anaongea pumba huku akijua wazi kuwa anachoongea ni pumba...njaa banna!
 
nasikiliza kipindi cha morning magic kupitia magic FM, namuona huyu doc anaongea utadhani ametumwa vile, analaani kitendo cha chadema kutoka nje, anasema kitendo hicho kina kiuka maadili ya mtanzania na kuvunja sheria za bunge. pia amefunguka zaidi kusema kuwa kumlalamikia spika kuwa anapendelea upande flani ni uongo kwani anafuata sheria za bunge.

Mbufya, umesahau kuwa kesha pewa chaka alilokuwa nalo Mkandala? Nani kiongozi wa REDET pale udsm?
 
Mkuu Pasco sihitaji kuhoji uhalali wa PhD ya Palamagamba kwani ninaamini fika kuwa UDSM ni chuo ambacho kina credibility 100% katika suala la wakufunzi wake, hivyo Palamagamba kuwa Professor of UDSM ni dhahiri anaqualify kama academician. Suala ninalotaka kujua ni je Thesis yake ameandikia kwenye nini hasa, maana A+ au GPA ya 4.8 ni level ya Undergraduate ambayo sidhani kama inamfanya mtu awe na PhD.

GPA ya juu si kigezo kwamba wewe ni nguli kwenye eneo lako kama ulivyoelevya hapo chini, ila ni academic achievement tu. Philophers believe that 'Education without application is useless' na kwa kuwa huyu jamaa unasema kuwa hajawahi kupanda kizimbani hata siku moja ku-argue case ni dhahiri kuwa practically ni impotent, na kwa maana hiyo hiyo kama hawezi kutumia ubongo wake ambao kumbukumbu za academic achievement zinaonesha ulikuwa sharp katika kuanalyse makaratasi ya maswali yanayotaka majibu (Mitihani) kuna uwezekano mkubwa sana aging imepunguza uwezo wake na hivyo vyeti vyake kuwa obsolete. Kuna wazee walipata A za hesabu wakati wa mkoloni leo hii hawajui hata computer inafanyaje kazi.

Huyu Kabudi ninamuweka kwenye kundi la Frustrated elites kama mwalimu mmoja wa Communication Skills UDSM ambao jua linakuchwa hawana la maana walilolifanya kwenye maisha yao ya ualimu na hivyo kujikuta ana compromise taalum ili atupiwe makombo na watawala.
Hofstede, mbona hili nilisha lisemea!
Kupata 1st class ni jambo moja, kuwa na Ph.D ni jambo jingine, lakine kuwa mzuri kwenye field, ni jambo jingine kabisa!.
 
Huyo kama kabudi achana nao kwanza tunahoji hata hizo phd walizipataje labda kwa kudesa wao wanatanguliza ukada zaidi kuliko weledi wa kitaaluma

Jamani, huyo mtu nilikuwa naye chuoni. Hamna kitu kabisa pale. Hao ndiyo wanaoshusha hata hadhi ya PhD - maana haieleweki inakuwaje mtu ambaye kila siku alikwa akizunguka kuatafuta madesa halafu leo awe ni kati ya watu tunaodhani wanaweza kuwa na mchango wa maana katika Taifa hili. Watu kama akina Bana, hata katika masuala ya kawaida, ni afadhali ukatafute ushauri kwa baadhi ya wanavijiji walioishia STD 7, angalao watakuambia kwa kuzingatia dhamira na akili zao. Bana ni mnafiki, na huishi kwa kujipendekeza, ndiyo maana ni vigumu kujua kama anachozungumza ndicho anachoamini au anazungumza ili kuwafurahisha anaodhani wanasaidia kutunza tumbo lake.

Itakapotokea CHADEMA wamechukua dola, mfuatilieni Bana - hakika atakuwa mtu wa kwanza kuponda utawala wa sasa na CCM.
 
Jamani, huyo mtu nilikuwa naye chuoni. Hamna kitu kabisa pale. Hao ndiyo wanaoshusha hata hadhi ya PhD - maana haieleweki inakuwaje mtu ambaye kila siku alikwa akizunguka kuatafuta madesa halafu leo awe ni kati ya watu tunaodhani wanaweza kuwa na mchango wa maana katika Taifa hili. Watu kama akina Bana, hata katika masuala ya kawaida, ni afadhali ukatafute ushauri kwa baadhi ya wanavijiji walioishia STD 7, angalao watakuambia kwa kuzingatia dhamira na akili zao. Bana ni mnafiki, na huishi kwa kujipendekeza, ndiyo maana ni vigumu kujua kama anachozungumza ndicho anachoamini au anazungumza ili kuwafurahisha anaodhani wanasaidia kutunza tumbo lake.

Itakapotokea CHADEMA wamechukua dola, mfuatilieni Bana - hakika atakuwa mtu wa kwanza kuponda utawala wa sasa na CCM.

JF inafurahisha na inaelimisha.
 
nakerwa sana na hii tabia ya vitoto vya chadema, wao wanataka kila mtu awe na mawazo yanayoendana na uchadema! Huu ni upuuzi na ukosefu wa demokrasia na uvumilivu...lazima uruhusu watu watofautiane huu ndio utajiri wenyeweb wa uumbaji! Mtu akitofautiana na chadema wanaanza kuhoji usomi wake na kusema lete cv....

hapa umenena..maana no 1 is perfect 100% lazima ukubal challenge ili uone na wengine wanaupeo gan then kama kuna mazur unayachukua na kuongezea kwako
afadhali mimi sijatekwa na huu ujinga unaoitwa chadema!

hapa hujawa mstaarabu kabisa..kwan yapo mazur meng tu waliyo tutasaidia..mazur chukua mbaya achana nayo bila hawa cdm kuwa na upinzan mkubwa na ccm kuna mambo meng sana tungekuwa hatuyajui..peoples power
 
Nimemsikia asubuhi,

Kweli ni masikitiko makubwa juu huyu mpotoshaji!sijui kazaliwa wapi na haya maneno anayasema akijiamini nini.

Labda nianze kwa kusema, tanzania na hasa katika bunge, hakuna hoja kwa miaka ya hivi karibuni, imepitishwa kwa vigezo vya hoja zilizotolewa na wabunge badala la kelele za kishabiki na kukidhi matakwa yao! Utamaduni upi wa mtanzania anaoueleza, nani hajui utamaduni wa sasa uliojengwa na watawala na kuasi utamaduni wa viongozi wetu waasisi wa nchi! Alienda mbali na kugusia suala la wananchi kuamua juu ya hili, na kweli sisi tutaamua kwani wanachokifanya chadema ni kitenda cha kiungwana kuwasilisha dukuduku lao kwa wananchi, sisi ndo kimbilio lao kwani vyombo husika kama kamati za bunge zimekuwa zikiegamia upande mmoja na hili liko wazi, aliwataka wafanye nini?

Kaenda mbali zaidi kaongelea suala la hoja kama zinakataliwa au hawapewi nafasi inabidi wamfate speaker na kumueleza hivi huyu jamaa vip? Wamfate mara ngapi na kanuni na taratibu za bunge zinasemaje kuhusu hili, mara ngapi amewapuuza juu ya haya maswala, bunge linaamua mambo kwa hoja, bunge hili nilijualo mimi?sio kelele za ndiyoo!je kama watu ni wachache inakaaje hii?tuna vigezo vya kuamua jambo ndani ya bunge kwa kupima uzito wa hoja hapa??? Mbona usomi unaupaka matope bwana benso bana, mbona unajipunguzia credit zako na uwered wako juu ya kutetea uozo na ushenzi unaofanywa na ccm na speaker wao,

umeulizwa swali juu ya upendeleo wa speaker na sikuona jambo la msingi ulililo liongea juu ya hili badala yake umekwepa na kuongelea mambo ya ajabu, je ni wangapi wapo kijiweni na hawana elimu hata ya std 7 lakini huu upendeleo wanauona, kama kweli wewe ni mtaalam wa sayansi ya siasa mbona umeshindwa kulisemea hili??

Wewe ni kada pamoja na unafiki wako kujifanya unatoa maoni na kushauri mambo ya kisiasa nchi, msomi ninayemwamini aliyetukuka na heshima yake itakuwa palepale ni profesa issa shivji, siku zote huyu mzee hamung'unyi jambo na ndo maana serikali hawamtumiii, yeye ndo mtaalam wa sheria na katiba tangu enzi za sokoine na baba wa taifa, je usomi wake umeteteleka wapi hadi nchi ishindwe kumtumia katika kipindi hiki?wanaogopa na kuwatumia watu kama bana wenye mtazamo wa karibu na utetezi wa walanguzi wa nchi yetu.

Matatizo ya hii nchi yanapigiliwa msumari na wasomi kama hawa, mbona hakuongelea utovu wa nidham wa wabunge wa ssm waliotumia muda wa walipa kodi kuzungumza kukashifu na kuwatukana chadema huku speaker wao akiweka mikono yote miwili kwenye kidevu?hilo hakuliona kuwa na utovu wa nidhamu?tumewatuma waende kufanya mipasho ndani ya jengo wanaliliita tukufu?utukufu wa jengo ni upi hai waliomo ni makafiri, hakuna dhambi mbaya kama kuwadhurum wananchi, kuwatapeli na kuwasaliti wapiga kura!hayo hayaoni anaona la chadema tu. Huyu mtu anatakiwa kutangazwa kuwa moja ya watu hatari wa kisisa za nchi yetu![/QUOTE

Huyu jamaa ni gamba bab kubwa. Si unajua tena hao ndugu zetu akina nshomile waliokuwa wametukuka kwa kitabu siku hizi wamefulia baada ya kujipambanua na CCM, Mkoa wa Kagera ulikuwa unapiga hatua kubwa ya maendekeo na hakutaka kuburuzwa na ccm mfano mzuri kuna mchumi mmoja (Prof. Rweyemamu) enzi ya nyerere aliwahi kuachia wadhifa aliokuwa nao kupinga kudhalilisha fani yake. Siku hizi wamezuka waganga njaa kama akina bana, salva, kilaini n.k ambao wanadhalilisha taaluma zao, matokeo yake sasa hivi mkoa wa Kagera uko katika mikoa mitano ya mwisho kimaendeleo. Mkoa ambao enzi ya Prof. Rweyemamu ulikuwa katika mikoa kumi bora. Kwa hiyo hiyo ni ishara tosha kuwa huyu kilaza anaganga njaa na kuwauza ndugu zake
 
Huyu jamaa ni gamba bab kubwa. Si unajua tena hao ndugu zetu akina nshomile waliokuwa wametukuka kwa kitabu siku hizi wamefulia baada ya kujipambanua na CCM, Mkoa wa Kagera ulikuwa unapiga hatua kubwa ya maendekeo na hakutaka kuburuzwa na ccm mfano mzuri kuna mchumi mmoja (Prof. Rweyemamu) enzi ya nyerere aliwahi kuachia wadhifa aliokuwa nao kupinga kudhalilisha fani yake. Siku hizi wamezuka waganga njaa kama akina bana, salva, kilaini n.k ambao wanadhalilisha taaluma zao, matokeo yake sasa hivi mkoa wa Kagera uko katika mikoa mitano ya mwisho kimaendeleo. Mkoa ambao enzi ya Prof. Rweyemamu ulikuwa katika mikoa kumi bora. Kwa hiyo hiyo ni ishara tosha kuwa huyu kilaza anaganga njaa na kuwauza ndugu zake
 
Ulitegemea CHADEMA waendelee kukaa Bungeni kwa faida ya nani? maana kabla walimuomba Mhe. Spika mjadala uahirishwe mama yule mwenye sura na roho mbaya akakataa. Dawa ni CHADEMA KUWASHTAKI CCM KWA WANANCHI kupitia mikutano ya hadhara na maandamano. Kinachotokea sasa ni CCM bila kujijua wanawapa CHADEMA umaarufu kwa wananchi nabashiri mabadiliko makubwa kwenye za nchi hii Uchaguzi mkuu ujao 2015
 
Mkuu Pasco sihitaji kuhoji uhalali wa PhD ya Palamagamba kwani ninaamini fika kuwa UDSM ni chuo ambacho kina credibility 100% katika suala la wakufunzi wake, hivyo Palamagamba kuwa Professor of UDSM ni dhahiri anaqualify kama academician. Suala ninalotaka kujua ni je Thesis yake ameandikia kwenye nini hasa, maana A+ au GPA ya 4.8 ni level ya Undergraduate ambayo sidhani kama inamfanya mtu awe na PhD.

GPA ya juu si kigezo kwamba wewe ni nguli kwenye eneo lako kama ulivyoelevya hapo chini, ila ni academic achievement tu. Philophers believe that 'Education without application is useless' na kwa kuwa huyu jamaa unasema kuwa hajawahi kupanda kizimbani hata siku moja ku-argue case ni dhahiri kuwa practically ni impotent, na kwa maana hiyo hiyo kama hawezi kutumia ubongo wake ambao kumbukumbu za academic achievement zinaonesha ulikuwa sharp katika kuanalyse makaratasi ya maswali yanayotaka majibu (Mitihani) kuna uwezekano mkubwa sana aging imepunguza uwezo wake na hivyo vyeti vyake kuwa obsolete. Kuna wazee walipata A za hesabu wakati wa mkoloni leo hii hawajui hata computer inafanyaje kazi.

Huyu Kabudi ninamuweka kwenye kundi la Frustrated elites kama mwalimu mmoja wa Communication Skills UDSM ambao jua linakuchwa hawana la maana walilolifanya kwenye maisha yao ya ualimu na hivyo kujikuta ana compromise taalum ili atupiwe makombo na watawala.

Ph.D yake aliipatia Ujerumani na kule alipata ya juu kabisa kwani Ujerumani huwa wanatoa daraja hata kwa Ph.D kama nilivyowahi kuandika kuhusu Prof. Kabudi ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa kupambanua mambo. Tatizo lake ni kuwa anapenda kuwa karibu na watawala na atasema lolote lile kuwaunga mkono watawala. Kwa hilo inakuwa kama midahalo ya sekondari "Maisha ya Kijijini ni bora kuliko maisha ya mjini? Hivyo suala si elimu yake suala ni uzalendo wake.
 
Back
Top Bottom