kabila01
JF-Expert Member
- Apr 21, 2009
- 4,235
- 4,949
Kuna demu mmoja nilikua na mahusiano naye zamani sana ilikua mwaka 2003, mahusiano yetu yalikaa kama miezi mitatu then akaondoka kurudi kwao Ngara. Katika kipindi cha mahusiano yetu hatukuwahi kufanya tendo la ndoa, lakin kwa jinsi tulivyokua tunapendana kila mtu alijua pale mtaani hadi wazazi wangu na ndugu zake pia. By that time yeye alikua amemaliza form six na mimi nikifanya kazi ya ualimu kijijini. Alipoenda kwao Ngara tuliendelea kuwasiliana kama miezi sita baada ya hapo mawasiliano yakafifia baadae tukapoteana kabisa. Baadae nikiwa chuo kikuu akanitafuta kwenye cm ingawa nilikua nimebadili line na akaniambia kua yupo chuo kikuu Mwanza Sauti. Hapo mawasiliano yakawa kwa mbali sana labda mie ndo nimpigie simu. akiwa mwaka wa mwisho chuoni akafunga ndoa na alinipa taarifa nikamtumia hela ya mchango kupitia a/c yake. Ingawa niliumia lakin baadae nikaamua kuchukulia kawaida na kuanzisha maisha mapya mwenyewe. alipomaliza chuo na mimi pia nikawa namaliza chuo nikabahatika kupata kazi yeye akawa bado yupo nyumbani kwa mumewe. akiwa kwa mumewe alikua akiniomba nimsaidie kumtafutia kazi nami nikawa nikiziona nafasi za kazi nampatia ajaribu, mawasiliano yakawa kama kaka na dada. Sasa hivi baada ya yeye kupata kazi na mimi nikawa nimehamishiwa jirani na mkoa alipo yeye. Sasa kasheshe ikaja siku niliyomwambia kua nimehamishwa tena kikazi nahamia Dar. Hapo ndo akaaanza kuniambia kua mimi nipo Moyoni mwake na anapata sana mateso juu yangu. usiku akilala na mumewe anahisi kama amelala na mimi, hata akiwa anafanya tendo la ndoa na mumewe bado anahisi kama yupo na mimi. imefikia kipindi hata akikaa na mumewe sebulen basi anatoroka anaenda nje ili anipigie tu simu tuongee.
Nimejitahidi kwa kila hali kumkwepa na kumwambia kua mie saizi nina mchumba ninayempenda na nataka kumuoa hivi karibuni bado anaendelea kua king'ang'anizi. nimejaribu kubadilisha line ya simu sijui wapi kaipata no yangu nashangaa ananipigia simu.
Naelewa kua mke wa mtu ni sumu na ni noma kutembea na mke wa mtu na hasa akijua bwana wake. najaribu kutopokea hata simu zake akipiga na akiandika sms sijibu lakin wapi. amesema ataamua kukimbia kwenye ndoa yake na kuja kwangu kitu ambacho ni hatari sana
sielewi wana JF huyu demu nimwambie nini anielewe maana ataniharibia future yangu ya maisha
Nimejitahidi kwa kila hali kumkwepa na kumwambia kua mie saizi nina mchumba ninayempenda na nataka kumuoa hivi karibuni bado anaendelea kua king'ang'anizi. nimejaribu kubadilisha line ya simu sijui wapi kaipata no yangu nashangaa ananipigia simu.
Naelewa kua mke wa mtu ni sumu na ni noma kutembea na mke wa mtu na hasa akijua bwana wake. najaribu kutopokea hata simu zake akipiga na akiandika sms sijibu lakin wapi. amesema ataamua kukimbia kwenye ndoa yake na kuja kwangu kitu ambacho ni hatari sana
sielewi wana JF huyu demu nimwambie nini anielewe maana ataniharibia future yangu ya maisha