Huyu dada nimfanyeje niko njia panda

Huyu dada nimfanyeje niko njia panda

The most mistake ulio ifanya mkuu ni kumpa mapenzi yooote, these people are to be loved intelligently, never care much, never ur umtime and part of yr wealth ili kumridhisha mwanamke, au binadam yeyte, unaweza ukaja kuwa mtu mbaya sana baada ya kuachwa,,
 
The most mistake ulio ifanya mkuu ni kumpa mapenzi yooote, these people are to be loved intelligently, never care much, never ur umtime and part of yr wealth ili kumridhisha mwanamke, au binadam yeyte, unaweza ukaja kuwa mtu mbaya sana baada ya kuachwa,,
Kweli kabisa mkuu
 
Pole sana mdogo wangu.

Hizi mada kila siku zinahubiriwa JF.
1. Mpende kwa kiasi
2. Mhudumie kiasi
3. Usimuamini zaidi ya 20% , hivi mnakwama wapi?

Hope umejifunza sasa.

Ila umeongeza single mother mjini.
 
Pole sana mdogo wangu.

Hizi mada kila siku zinahubiriwa JF.
1. Mpende kwa kiasi
2. Mhudumie kiasi
3. Usimuamini zaidi ya 20% , hivi mnakwama wapi?

Hope umejifunza sasa.

Ila umeongeza single mother mjini.
Wanajikuta wanajua kupenda kuliko wakubwa wao
 
SASA TUENDELEEEEE

Baada ya kutoka kuzungumza na uyo binti nilikua km plug azichomi ivi maana nilihisi moyo tu ndio unafanya kazi viungo vyote na akili vimesimama kwa kutokuamin yanayo tokea katika maisha yang ukumbuke tang tufahamiane na G ni miezi8 ilikua imepita ayo ndio yanaanza kutokea iyo siku ndio siku ya kwanza natumia pombe Kali konyagi maana sikutaka kukumbuka kitu usiku nakumbuka nililewa Sana na sikuweza kwenda nyumbani nilijikuata Niko kwenye chumba cha lodge Niko peke yang na kila kitu chang kiko salama na ni SAA4 asubuh wafanya usafi ndio wananiamsha nilijimwagia maji nikaenda home Ku change nikaenda shop nikafungua kisha nikaenda kwa G Niki taka kupata uthibitisho wa yale nilio yasikia kutoka kwa ndugu yake ,
Alinikaribisha huku km ajiamin ivi nilamsalimu baada ya salaam nikamuuliza kwanin? Amebadilika ukumbuke kipindi icho na simu na text zimepungua Mara apokee Mara asipokee ndivyo ilivyo kua basi tuendelee akasema amuna kitu ni u busy tu namimi sikumficha nikamueleza kila kitu nilicho elezwa kuhusu yeye mpka tarehe ya mahar na kunithibitishia alinyamaza kimya akanambia aliona Mimi nampotezea mda na sikua na mpango nae na tayar tulikua tushapanga mwaka unaofuata yaan 2017 ndio ndoa yetu akuwa na cha kusema ni aibu tu kwa hasira nikaondoka huku kichwa kikiwa na msongo mwingi wa mawazo nikiwaza nishamtbulisha kwa watu Wang wa karbu watanielewaje na alimanusura nmpeleke nyumbani nishaanza kuingia kwenye kamati za harusi mbali mbali nikijua yangu aiko mbali ivyo nianze kuchanga maana nitahtaji kuchangiwa na mimi ayo mambo yote yalinivuruga kichwa nikaona bora nilewe tu pengine Niko ndotoni nitazindika kutoka usingizini lakini aikua ivyo ,

Mipango ya harus iliendelea na wakafunga ndoa ya kihalali kanisa katoliki huku Mimi familia na jamaa wasijue kitu gan kimenipata duka nilimuachia yule dogo walevi ndio wakawa rafiki zang nakumbuka Mara kadhaa nilipelekwa na mama kuombewa kwa watumishi tofauti tofauti wakiamin nimelogwa kumbe G ndio ameniloga juhudi zote azikua na mafanikio mtaji uliyumba nikaanza kukopa kwenye taasisi na pesa izo akuna nilicho fanyia zaidi ya pombe mambo yakawa Magumu heshima yang nyumbani ikaisha nikabakia kuitwa mlevi sababu ya G ata marafiki nilio kua nao wakawa wananikwepa maana nilitoka kunywa henken,castle lite mpka kwenye pombe za karatasi au viroba,
Mambo yakawa magumu madeni kila kona na huku mikoan tunajuana Sana nikageuka story of the town watu wasijue kitu gan kimenipata,.

Ndani ya miez 8 nilikua nimetoka kwenye ujana mpka uzee ata ile sura yang ya ujana imepotea kila kitu ni kingine watu wanasema nimwlogwa,madeni yalinizidi nikakimbia mji ulikua mchungu nikaenda zang kwa bashite nikiwa sina hata nakumbika nauli ya kwenda huko niliuza laptop nilio kua naitumia chuo,.

Nilifika dar nikaanza maisha mapya kwa mkubwa Wang yeye ni mfanya biashara kko ivyo asubuh tukawa tunaenda nae na jion tunarudi lakin tayar nishakua teja maana mda wote nilikua alcohol na nikipotea kidogo tu nilikua naenda Ku charge betri.
Niliendelea ivyo ivyo na ayo maisha mpka siku Mungu alipo nirudishia akili zang Mimi mja wake nakumbuka iyo siku usiku sikunywa Sana ivyo ikapelekea usingizi kuisha mapema kwenye SAA8 iv ulikua umekata nikaanza kukumbuka mambo ya nyuma ikiwa ni mwaka umepita nikaangalia nilivyo kua na Sas NIKAAPA KUTOKUTUMIA POMBE TENA KWENYE MAISHA YANGU mwanzon nilipata shida maana nilikua nasikia kiu km mtu alieshinda kwenye jua siku tatu akifanya kazi ngumu bila kunywa maji ila hakika Mungu ni mwema alinisaidia nikaanza kwenda kanisan na kujitenga na marafiki walevi ambao ata dar nilikua nishakuaa nao,

Baada ya miezi mitatu nishakua na tabia njema wazazi na ndugu wakanichangia pesa nikafungua duka LA Viatu kkoo na maisha yakaanza upya,

UYU IBILISI WA KIKE sijui nan ! Alimwambia Niko sawa saaaiv akaanza kunitafta kuniomba msamah mi nikamuambia ujanikosea Kila mtu anachagua mtu sahii wa maisha yake ndio akaanza kunisimulia Analia jamaa yake alimdanganya anafanya kazi ofsi ya rais atamtaftia kazi BOT au wizara ya fedha kumbe jamaa ni mwalimu tena shule ya private alikua anaazima magar kwenda kwao G basi akaniomba nimsamehe na kwa kipindi icho G alivyo jua jamaa amemudanganya akavunja ndoa akarudi kwao ,tukawa tunasalimiana tu kawaida mpka mwaka huu Mwezi wa 1 alikuja dar kwenye harus ya ndugu yake akasema anataman afike kwangu maana nishatoka kwa bro najitegemea,

Ilikua siku ya jumamos nilienda kkoo. kwenye mishe zangu akanipigia simu mida ya saa8 anataka kuja home basi nikamwacha mshikaji makufuli jion atafunga mi nikaenda home Nikamuelekeza akafika nilikua nataman nimuone maana ni. siku nyingi na nilikua nampenda shida nijeraha moyoni alifika akashangaa kukuta Niko poa tu maana wanaume Kurudia khali yetu ni simple tofaauti na wanawake tulipiga story 2,3 mpka usiku ukaingia nasubr mtu aage sioni mtu km anadalili za kuondoka nikamwambia usiku unazidi kua mrefu naomba nikusindikize nashangaa MTU anaanza kulia nimsamehe kumbembeleza kujikuta tuko kitandani tunatinduana,

Akaa siku 2 lakini nishasema sito kaaa nirudiane nae uyo mwanamke alivyo toka tu nika mbolck akasafr kurudi mkoan na baada ya miezi mitatu Ananiambi anaujauzito Wang na awezi kuutoa ata km simpendi lakini atoi mimba Mimi nae nimemkaushia na nimebadili na namba Za simu maaana nikikumbuka aliko nipitisha naumia Sana aibu aliyo nipatia alafu Leo nimuoe apana acha tu abaki na mtoto wa makumbusho ameshaniaribia moyo wang iman sina tena tamani kuoa Ila yale matukio nikiyakumbuka moyo unasita na umri unasonga na Nimekua na tabia ya kuanzisha uhusiano na ghafla naanza kumchukia tena munisaidie nitafanyeje niweze kurudi hali ya mwanzo niweze kumuamin tena mchumba nitakae mpta MaanA km moyo wa kupenda sina tena

Pole mkuu jipe nafasi ya kupona majeraha kabla ya kuanzisha mahusiano mengine ila mtoto hasuswi hata kama humtaki mama yake
 
waliosoma nipeni summary please. story ndefu sana bro.
 
Nakumbuka ilikua mwaka 2015 ndio nakutana na uyu Dada kwenye moja ya mikoa kanda ya ziwa alikuja kwa mjomba wake na mimi nilikua zangu nishaanza mapambano ya kusaka $ .

Alikua amemaliza Kati ya moja ya vyuo jijini mwanza na kwa wakati huo alikua yupo yupo ivyo mjomba wake akaona ni vema aje kwake kipindi anasubri mambo yake amsaidie kuuza duka la vifaa vya ujenzi mjini hapo ambapo mjomba ake ana maduka kadhaaa.

Katika pitapita zangu mtaani maana Mimi pia nilikua nafanya iyo biashara mtaa wa pili na kilicho nikutanisha na uyo binti ni mteja Wang alikosa item alio itaka dukan kwangu akaomba nikamtaftie kwa wenzang kwa kigezo cha mimi ndio najua ubora wa item kufika pale ndio nikakuta MTOTO amesimama sio sura sio rangi sio umbo mrefu km mtusi mate yakanitoka mdomoni mithiri ya muathirika wa dawa za kulevya wa mda mrefu hapo ndio mwanzo wa kujuana na uyu mrembo aliegeuka badae sumu katika maisha yangu.

Sikua na papala siku ya Kwanza na maadam nilijua anapo patikana nilijiapiza kufanya kila ninacho Weza ili awe wang nikaona sio vema kwenda nae kwa speed nikapanga mikakati km ya Michael scolfied kwenye prison break.
Zilipita siku tatu na siku ya nne nili rejea tena pale dukani kwa mjomba wake nikamsalimia kwa bashasha na ukarimu wa hali ya juu huku nikiwa nimetupia pamba mpya kwanzia juu mpka chini na nimetoka barbar shop mda sio mrefu kabla sijamtokea pale.

Alinisalim pia lakini akuonesha kunijali ikawa km anikumbuki ivyo ilinilazimu kumkumbusha akanikumbuka na sikua na mambo mengi nilimwambia kilicho nipeleka pale nilihitaj kujua anaitwa nan? Nilamwambia sio vema tunafanya biashara mtaa mmoja na biashara ya aina moja tusijuane,hilo alikumsumbua kichwa akanieleza jina lake anaitwa G na Mimi nikamwambia la kwangu,
Siku iyo ilikua ya furaha Sana kwangu kwakua mission yangu ya siku iyo ilitimia,Niliondoka dukani pale huku mission inayo fuatia ni ya kuchukua namba yake ya simu ya kiganjani.

Baada ya siku mbili kupita niliamka asubuh na mapema nikajiandaa kwenda dukan kwangu huku nikijiapiza moyoni kuchukua no ya simu siku iyo nilifika dukan km kawaida nikafungia kisha nikamsubr dogo kuna dogo nilikua Nae pale alivyo fika nikaondoka kwenda kuzunguka madukan kutafta simu mpya Maana ile yangu niliona km aifai na imeshakaa mwaka mmoja hivyo nilifanikiwa kununua simu nyingine akili nyingine ya kiwenda wazimu ikanituma ninunue nguo mpya tena kwa kigezo zang azifai sijui yule mwanamke nilimuonaje kwa kipindi icho tofauti na sasa.
Nilirejea dukan kwa mtoto mzur nikamkuta anaendelea na biashara safar hii ikawa tofauti akanisalimu kwa ukalimu na pia akanambia nimependeza Sana hapo moyo unafrahi kwa Ndani na kichwa kina vimba alivyo maliza tuukapiga story mbili tatu za kibiashara mwisho wa siku nikamuomba namba kwa kigezo cha kibiashara kwamba kuna vitu vingine unakuta sina dukan kwangu ivyo kujua km anavyo endapo wateja wang. watahitaj tunapaswa kuwasiliana,iyo technique alikua awezi kuruka akaniomba simu aandike kumbuka nimenunua simu latest kwa wakati huo kwa watu wenye uchumi wa kawaida lakini unaweza kujiuliza nilikuwa naweza kuyamudu aya yote ukumbuke miaka miwili nyuma nilikua nimetoka chuo na sikuamini kuajiriwa ivyo Mzazi alinibariki pesa za kuanzisha biashara na kwa kipindi icho chote nilikua Niko home pesa yangu ilikua ya matumizi yangu tuu sikuhusishwa kwa lolote na chochote.

Baada ya Ku win biko km sio tatu mzuka ya kupata no mission yang kwa 75%ilikua imekamilika nilianza kuangalia madhaifu na mapungufu yake nikagundua kwenye swala la chakula na usafir ni changamoto maana unakua busy kias kwamba anakosa nafasi ya kwenda sehemu nzur kuagiza chakula ivyo Inamulazimu kula chakula kwa mamantilie wanao uza mabarabarani na kwenye usafir nikagundua asubuh anakuja na mjomba wake na jioni anapanda piki piki nikawa nimepata sehemu ya kuchukulia point3 kavu,

Tushakua na mawasiliano na kila mtu anamjua mwenzie katika kuchat chat Nikamuomb nimpe lunch siku iyo akanambia Awezi kutoka nikamjulisha itamfata hapo hapo akakubali ofa yang nikafurah Sana nikatafta mgahawa unaouza chakula kizur mkoani hapo aikua kazi ngumu kuna wasomali ni mabingwa wa kupika nikaomba kuweka bili wakakukubali nikawaelekeza duka la uyo mrembo lilipo kwa makubaliano ya kuanza bili siku inayo fuatia Ila siku iyo nililipia cash na nikamuagizia pilau na kuku wakampelekea,
Alifurahi Sana na kukisifu chakula na sikumwambia km nimemuwekea bila siku ilio fuata nilienda kulipia pesa na kuwambia wampelekea chakula cha tofauti n siku ilio pita na pia wampe tarifa kua Amewekew bili ya msosi ivyo awe nanatoa tarifa ya siku inayo fuata chakula atakacho penda kutumia,
Alinishukuru kwa ajir ya hilo na ukaribu wetu ukaongezeka tukawa tunawasiliana Mara kwa Mara bila kuonyesha dalili za kutakana sikutaka kuwa na speed maana nilijua jonsi ninavyo mpenda angenikataa ningeumia Sana,.

Ilikua weekend moja tulivu nakumbuka siku iyo mvua ilinyesha nikamuomba tukutane kwenye moja ya hotel nzur hapo mkoani kwa ajir ya kupiga story za kilafiki na chakula pia km atojali alinikubalia ombi lang maana Tuliku tuahakua marafik na hakua na mashaka namimi tena,
Iyo ndio siku nilio fungua moyo na kutoa kilichokua ndani alinisikiliza kwa makini na nilimuomba tuwe Wapenzi Ila tukiwa na mpango wa kuoana maana nilimueleza njinsi gani moyo Wang unamuhitaj awe Wang na nikala kiapo kwamba ikitokea ananikubalia sito kuja kumsaliti au kutoka na mtu mwingine kamwe maana nilimuona yeye ndio Mwanzo na mwisho, Kiukweli alikua jambo gumu kwake akanijibu nimpe mda nimemshitukiza akua amejiandaa kwa hilo nikamuelewa tukaendelea kutumia vinywaji alipendelelea red bull na Mimi nikawa natumia vitamalt nachanganya na coke nilikua Natumi Bia lakin sikupenda kujiweka wazi maana sikujua angenichukulia vp kpz Wang uyo,

Siku kadhaa zilipita tukiendelea kuwasilaana kawaida na mimi sikua na presha maana tayar mzigo nilio kua nimebeba moyoni tayar nisha utua ghafla text msg ikangia kwenye siku yangu ilikua km ifuatavyo (E nakupenda kuliko kitu chochote nakupa moyo Wang tafadhali usije ukanitoa machozi) Hapo ndio dunia mpya ikawa imefunguka baina yang na G sio siri kwa mtu yoyote alie tuona kipindi hicho alipendezwa na namuna tulivyo kua mda baada ya kazi nilimpeleka mpka nyumbani sio siri alionesha kunipenda na mimi nikampenda Sana tena Sana na tulifanya mambo mazur km sio yote ambayo watu wanao pendana wanapswa kufanyiana.

GHAFLA ibilisi akaingilia penzi letu ndio kilicho pelekea Leo naandika yote aya G akaanza kubadilika taratibu akaanza kufunga biashara anaenda nyumban bila kuniarifu nikawaza ni bahati mbya kumbe alikusudia na mimi mshale ukaanza kunigota kutaka kujua ni nni? Kinachotaka kudhulumu penzi lang nikaanza kufatilia kuna baadhi ya ndugu zake nilikua nafamiana nao ndio mmoja akanambia G amepata mchumba anataka kumuoa na nyumbani amekuja ameleta vitu mahar ni mwezi ujao ,Sio siri nilipo kua sijui mwanamke ananikwepa kwepa kumbe anayake.ITAENDELEA BADADAE KIDOGO
Huku mbele hata usimalizie naweza kuiendeleza mwenyewe mkuu hii story.
 
Yaani utadhani unasimulia story yangu haya mapenzi haya basi tu yanaumiza sana, mpaka leo pombe imekuwa kitu cha kawaida kwangu…
 
Yaani hutongozi mpaka uvae nguo mpya na uwe na simu mpya?.hizo ni dariri za kutojiamini na lazima utoswe na mwanamke smart na anayejiamni...
 
Yaani utadhani unasimulia story yangu haya mapenzi haya basi tu yanaumiza sana, mpaka leo pombe imekuwa kitu cha kawaida kwangu…
Pole brother jitaidi utoke huko utaangamia wakati yeye anakula bata
 
Wasukuma bhana story ndeeefu ovyo kabisa
Mmezoe kudharau wengine akuna aliye kulazimisha kusoma na kumbuka kila mtu Ana uhuru humu wa kuandika bila kuwakosea wenzake na kuvuruga taratibu za humu ndani km wew unaiona ovyo wapo wanao ithamini na wanabudika na kujifunza pia mkuu jifunze kuheshimu Mawazo ya wenzio
 
Back
Top Bottom