kamituga
JF-Expert Member
- May 31, 2019
- 1,195
- 1,937
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2015 ndio nakutana na huyu Dada kwenye moja ya mikoa kanda ya ziwa alikuja kwa mjomba wake na mimi nilikuwa zangu nishaanza mapambano ya kusaka $ .
Alikuwa amemaliza Kati ya moja ya vyuo jijini Mwanza na kwa wakati huo alikuwa yupo yupo hivyo mjomba wake akaona ni vema aje kwake kipindi anasubri mambo yake amsaidie kuuza duka la vifaa vya ujenzi mjini hapo ambapo mjomba wake ana maduka kadhaa.
Katika pitapita zangu mtaani maana mimi pia nilikuwa nafanya hiyo biashara mtaa wa pili na kilichonikutanisha na huyo binti ni mteja wangu alikosa item aliyoitaka dukani kwangu akaomba nikamtaftie kwa wenzangu kwa kigezo cha mimi ndio najua ubora wa item kufika pale ndio nikakuta MTOTO amesimama sio sura sio rangi sio umbo mrefu km mtusi mate yakanitoka mdomoni mithiri ya muathirika wa dawa za kulevya wa muda mrefu hapo ndio mwanzo wa kujuana na huyu mrembo aliyegeuka badae sumu katika maisha yangu.
Sikuwa na papala siku ya kwanza na maadam nilijua anapopatikana nilijiapiza kufanya kila ninachoweza ili awe wangu nikaona sio vema kwenda nae kwa speed nikapanga mikakati kama ya Michael Scolfied kwenye prison break.
Zilipita siku tatu na siku ya nne nilirejea tena pale dukani kwa mjomba wake nikamsalimia kwa bashasha na ukarimu wa hali ya juu huku nikiwa nimetupia pamba mpya kwanzia juu mpaka chini na nimetoka barbar shop muda sio mrefu kabla sijamtokea pale.
Alinisalim pia lakini hakuonesha kunijali ikawa km hanikumbuki hivyo ilinilazimu kumkumbusha akanikumbuka na sikuwa na mambo mengi nilimwambia kilichonipeleka pale nilihitaji kujua anaitwa nan? Nilimwambia sio vema tunafanya biashara mtaa mmoja na biashara ya aina moja tusijuane,hilo alikumsumbua kichwa akanieleza jina lake anaitwa G na Mimi nikamwambia la kwangu.
Siku hiyo ilikuwa ya furaha sana kwangu kwakuwa mission yangu ya siku iyo ilitimia,Niliondoka dukani pale huku mission inayofuatia ni ya kuchukua namba yake ya simu ya kiganjani.
Baada ya siku mbili kupita niliamka asubuhi na mapema nikajiandaa kwenda dukani kwangu huku nikijiapiza moyoni kuchukua namba ya simu. Siku hiyo nilifika dukani kama kawaida nikafungiu kisha nikamsubiri dogo kuna dogo nilikuwa nae pale alivyofika nikaondoka kwenda kuzunguka madukani kutafuta simu mpya maana ile yangu niliona kama haifai na imeshakaa mwaka mmoja hivyo nilifanikiwa kununua simu nyingine akili nyingine ya kiwenda wazimu ikanituma ninunue nguo mpya tena kwa kigezo zangu hazifai sijui yule mwanamke nilimuonaje kwa kipindi hicho tofauti na sasa.
Nilirejea dukani kwa mtoto mzuri nikamkuta anaendelea na biashara safari hii ikawa tofauti akanisalimu kwa ukalimu na pia akanambia nimependeza sana hapo moyo unafurahi kwa ndani na kichwa kinavimba. Alivyomaliza tukapiga story mbili tatu za kibiashara mwisho wa siku nikamuomba namba kwa kigezo cha kibiashara kwamba kuna vitu vingine unakuta sina dukani kwangu hivyo kujua kama anavyo endapo wateja wangu watahitaji tunapaswa kuwasiliana. Hiyo technique alikuwa hawezi kuruka akaniomba simu aandike kumbuka nimenunua simu latest kwa wakati huo kwa watu wenye uchumi wa kawaida lakini unaweza kujiuliza nilikuwa naweza kuyamudu haya yote ukumbuke miaka miwili nyuma nilikuwa nimetoka chuo na sikuamini kuajiriwa hivyo mzazi alinibariki pesa za kuanzisha biashara na kwa kipindi hicho chote nilikuwa niko home pesa yangu ilikuwa ya matumizi yangu tuu sikuhusishwa kwa lolote na chochote.
Baada ya Ku-win biko km sio tatu mzuka ya kupata no mission yangu kwa 75%ilikuwa imekamilika nilianza kuangalia madhaifu na mapungufu yake nikagundua kwenye suala la chakula na usafiri ni changamoto maana unakuwa busy kiasi kwamba anakosa nafasi ya kwenda sehemu nzuri kuagiza chakula hivyo inamlazimu kula chakula kwa mamantilie wanaouza mabarabarani na kwenye usafiri nikagundua asubuhi anakuja na mjomba wake na jioni anapanda pikipiki nikawa nimepata sehemu ya kuchukulia point3 kavu.
Tushakuwa na mawasiliano na kila mtu anamjua mwenzie katika kuchat chat nikamuomba nimpe lunch siku hiyo akanambia hawezi kutoka nikamjulisha itamfata hapo hapo akakubali ofa yangu nikafurahi sana nikatafuta mgahawa unaouza chakula kizuri mkoani hapo haikuwa kazi ngumu kuna wasomali ni mabingwa wa kupika nikaomba kuweka bili wakakukubali nikawaelekeza duka la huyo mrembo lilipo kwa makubaliano ya kuanza bili siku inayofuatia Ila siku hiyo nililipia cash na nikamuagizia pilau na kuku wakampelekea
Alifurahi sana na kukisifu chakula na sikumwambia kama nimemuwekea bila siku iliofuata nilienda kulipia pesa na kuwambia wampelekea chakula cha tofauti na siku iliopita na pia wampe taarifa kuwa amewekewa bili ya msosi hivyo awe anatoa taarifa ya siku inayofuata chakula atakachopenda kutumia.
Alinishukuru kwa ajiribya hilo na ukaribu wetu ukaongezeka tukawa tunawasiliana mara kwa mara bila kuonesha dalili za kutakana, sikutaka kuwa na speed maana nilijua jinsi ninavyompenda angenikataa ningeumia sana.
Ilikuwa weekend moja tulivu nakumbuka siku hiyo mvua ilinyesha nikamuomba tukutane kwenye moja ya hotel nzuri hapo mkoani kwa ajiri ya kupiga story za kirafiki na chakula pia kama hatojali alinikubalia ombi langu na hakua na mashaka na mimi tena.
Hiyo ndio siku niliyofungua moyo na kutoa kilichokuwa ndani alinisikiliza kwa makini na nilimuomba tuwe Wapenzi Ila tukiwa na mpango wa kuoana maana nilimueleza ni jinsi gani moyo Wangu unamuhitaj awe Wang na nikala kiapo kwamba ikitokea ananikubalia sito kuja kumsaliti au kutoka na mtu mwingine kamwe maana nilimuona yeye ndio Mwanzo na mwisho, Kiukweli alikua jambo gumu kwake akanijibu nimpe mda nimemshitukiza hakua amejiandaa kwa hilo nikamuelewa tukaendelea kutumia vinywaji alipendelelea red bull na Mimi nikawa natumia vitamalt nachanganya na coke nilikua Natumi Bia lakin sikupenda kujiweka wazi maana sikujua angenichukulia vp kpz Wang uyo,
Siku kadhaa zilipita tukiendelea kuwasilaana kawaida na mimi sikua na presha maana tayar mzigo nilio kua nimebeba moyoni tayar nisha utua ghafla text msg ikangia kwenye siku yangu ilikua km ifuatavyo (E nakupenda kuliko kitu chochote nakupa moyo Wang tafadhali usije ukanitoa machozi) Hapo ndio dunia mpya ikawa imefunguka baina yang na G sio siri kwa mtu yoyote alie tuona kipindi hicho alipendezwa na namna tulivyokuwa mda baada ya kazi nilimpeleka mpaka nyumbani sio siri alionesha kunipenda na mimi nikampenda Sana tena Sana na tulifanya mambo mazur km sio yote ambayo watu wanao pendana wanapswa kufanyiana.
GHAFLA ibilisi akaingilia penzi letu ndio kilicho pelekea Leo naandika yote haya G akaanza kubadilika taratibu akaanza kufunga biashara anaenda nyumban bila kuniarifu nikawaza ni bahati mbaya kumbe alikusudia na mimi mshale ukaanza kunigota kutaka kujua ni nni? Kinachotaka kudhulumu penzi langu nikaanza kufatilia kuna baadhi ya ndugu zake nilikuwa nafamiana nao ndio mmoja akanambia G amepata mchumba anataka kumuoa na nyumbani amekuja ameleta vitu mahari ni mwezi ujao ,Sio siri nilipokuwa sijui mwanamke ananikwepa kwepa kumbe anayake.ITAENDELEA BADADAE KIDOGO
Alikuwa amemaliza Kati ya moja ya vyuo jijini Mwanza na kwa wakati huo alikuwa yupo yupo hivyo mjomba wake akaona ni vema aje kwake kipindi anasubri mambo yake amsaidie kuuza duka la vifaa vya ujenzi mjini hapo ambapo mjomba wake ana maduka kadhaa.
Katika pitapita zangu mtaani maana mimi pia nilikuwa nafanya hiyo biashara mtaa wa pili na kilichonikutanisha na huyo binti ni mteja wangu alikosa item aliyoitaka dukani kwangu akaomba nikamtaftie kwa wenzangu kwa kigezo cha mimi ndio najua ubora wa item kufika pale ndio nikakuta MTOTO amesimama sio sura sio rangi sio umbo mrefu km mtusi mate yakanitoka mdomoni mithiri ya muathirika wa dawa za kulevya wa muda mrefu hapo ndio mwanzo wa kujuana na huyu mrembo aliyegeuka badae sumu katika maisha yangu.
Sikuwa na papala siku ya kwanza na maadam nilijua anapopatikana nilijiapiza kufanya kila ninachoweza ili awe wangu nikaona sio vema kwenda nae kwa speed nikapanga mikakati kama ya Michael Scolfied kwenye prison break.
Zilipita siku tatu na siku ya nne nilirejea tena pale dukani kwa mjomba wake nikamsalimia kwa bashasha na ukarimu wa hali ya juu huku nikiwa nimetupia pamba mpya kwanzia juu mpaka chini na nimetoka barbar shop muda sio mrefu kabla sijamtokea pale.
Alinisalim pia lakini hakuonesha kunijali ikawa km hanikumbuki hivyo ilinilazimu kumkumbusha akanikumbuka na sikuwa na mambo mengi nilimwambia kilichonipeleka pale nilihitaji kujua anaitwa nan? Nilimwambia sio vema tunafanya biashara mtaa mmoja na biashara ya aina moja tusijuane,hilo alikumsumbua kichwa akanieleza jina lake anaitwa G na Mimi nikamwambia la kwangu.
Siku hiyo ilikuwa ya furaha sana kwangu kwakuwa mission yangu ya siku iyo ilitimia,Niliondoka dukani pale huku mission inayofuatia ni ya kuchukua namba yake ya simu ya kiganjani.
Baada ya siku mbili kupita niliamka asubuhi na mapema nikajiandaa kwenda dukani kwangu huku nikijiapiza moyoni kuchukua namba ya simu. Siku hiyo nilifika dukani kama kawaida nikafungiu kisha nikamsubiri dogo kuna dogo nilikuwa nae pale alivyofika nikaondoka kwenda kuzunguka madukani kutafuta simu mpya maana ile yangu niliona kama haifai na imeshakaa mwaka mmoja hivyo nilifanikiwa kununua simu nyingine akili nyingine ya kiwenda wazimu ikanituma ninunue nguo mpya tena kwa kigezo zangu hazifai sijui yule mwanamke nilimuonaje kwa kipindi hicho tofauti na sasa.
Nilirejea dukani kwa mtoto mzuri nikamkuta anaendelea na biashara safari hii ikawa tofauti akanisalimu kwa ukalimu na pia akanambia nimependeza sana hapo moyo unafurahi kwa ndani na kichwa kinavimba. Alivyomaliza tukapiga story mbili tatu za kibiashara mwisho wa siku nikamuomba namba kwa kigezo cha kibiashara kwamba kuna vitu vingine unakuta sina dukani kwangu hivyo kujua kama anavyo endapo wateja wangu watahitaji tunapaswa kuwasiliana. Hiyo technique alikuwa hawezi kuruka akaniomba simu aandike kumbuka nimenunua simu latest kwa wakati huo kwa watu wenye uchumi wa kawaida lakini unaweza kujiuliza nilikuwa naweza kuyamudu haya yote ukumbuke miaka miwili nyuma nilikuwa nimetoka chuo na sikuamini kuajiriwa hivyo mzazi alinibariki pesa za kuanzisha biashara na kwa kipindi hicho chote nilikuwa niko home pesa yangu ilikuwa ya matumizi yangu tuu sikuhusishwa kwa lolote na chochote.
Baada ya Ku-win biko km sio tatu mzuka ya kupata no mission yangu kwa 75%ilikuwa imekamilika nilianza kuangalia madhaifu na mapungufu yake nikagundua kwenye suala la chakula na usafiri ni changamoto maana unakuwa busy kiasi kwamba anakosa nafasi ya kwenda sehemu nzuri kuagiza chakula hivyo inamlazimu kula chakula kwa mamantilie wanaouza mabarabarani na kwenye usafiri nikagundua asubuhi anakuja na mjomba wake na jioni anapanda pikipiki nikawa nimepata sehemu ya kuchukulia point3 kavu.
Tushakuwa na mawasiliano na kila mtu anamjua mwenzie katika kuchat chat nikamuomba nimpe lunch siku hiyo akanambia hawezi kutoka nikamjulisha itamfata hapo hapo akakubali ofa yangu nikafurahi sana nikatafuta mgahawa unaouza chakula kizuri mkoani hapo haikuwa kazi ngumu kuna wasomali ni mabingwa wa kupika nikaomba kuweka bili wakakukubali nikawaelekeza duka la huyo mrembo lilipo kwa makubaliano ya kuanza bili siku inayofuatia Ila siku hiyo nililipia cash na nikamuagizia pilau na kuku wakampelekea
Alifurahi sana na kukisifu chakula na sikumwambia kama nimemuwekea bila siku iliofuata nilienda kulipia pesa na kuwambia wampelekea chakula cha tofauti na siku iliopita na pia wampe taarifa kuwa amewekewa bili ya msosi hivyo awe anatoa taarifa ya siku inayofuata chakula atakachopenda kutumia.
Alinishukuru kwa ajiribya hilo na ukaribu wetu ukaongezeka tukawa tunawasiliana mara kwa mara bila kuonesha dalili za kutakana, sikutaka kuwa na speed maana nilijua jinsi ninavyompenda angenikataa ningeumia sana.
Ilikuwa weekend moja tulivu nakumbuka siku hiyo mvua ilinyesha nikamuomba tukutane kwenye moja ya hotel nzuri hapo mkoani kwa ajiri ya kupiga story za kirafiki na chakula pia kama hatojali alinikubalia ombi langu na hakua na mashaka na mimi tena.
Hiyo ndio siku niliyofungua moyo na kutoa kilichokuwa ndani alinisikiliza kwa makini na nilimuomba tuwe Wapenzi Ila tukiwa na mpango wa kuoana maana nilimueleza ni jinsi gani moyo Wangu unamuhitaj awe Wang na nikala kiapo kwamba ikitokea ananikubalia sito kuja kumsaliti au kutoka na mtu mwingine kamwe maana nilimuona yeye ndio Mwanzo na mwisho, Kiukweli alikua jambo gumu kwake akanijibu nimpe mda nimemshitukiza hakua amejiandaa kwa hilo nikamuelewa tukaendelea kutumia vinywaji alipendelelea red bull na Mimi nikawa natumia vitamalt nachanganya na coke nilikua Natumi Bia lakin sikupenda kujiweka wazi maana sikujua angenichukulia vp kpz Wang uyo,
Siku kadhaa zilipita tukiendelea kuwasilaana kawaida na mimi sikua na presha maana tayar mzigo nilio kua nimebeba moyoni tayar nisha utua ghafla text msg ikangia kwenye siku yangu ilikua km ifuatavyo (E nakupenda kuliko kitu chochote nakupa moyo Wang tafadhali usije ukanitoa machozi) Hapo ndio dunia mpya ikawa imefunguka baina yang na G sio siri kwa mtu yoyote alie tuona kipindi hicho alipendezwa na namna tulivyokuwa mda baada ya kazi nilimpeleka mpaka nyumbani sio siri alionesha kunipenda na mimi nikampenda Sana tena Sana na tulifanya mambo mazur km sio yote ambayo watu wanao pendana wanapswa kufanyiana.
GHAFLA ibilisi akaingilia penzi letu ndio kilicho pelekea Leo naandika yote haya G akaanza kubadilika taratibu akaanza kufunga biashara anaenda nyumban bila kuniarifu nikawaza ni bahati mbaya kumbe alikusudia na mimi mshale ukaanza kunigota kutaka kujua ni nni? Kinachotaka kudhulumu penzi langu nikaanza kufatilia kuna baadhi ya ndugu zake nilikuwa nafamiana nao ndio mmoja akanambia G amepata mchumba anataka kumuoa na nyumbani amekuja ameleta vitu mahari ni mwezi ujao ,Sio siri nilipokuwa sijui mwanamke ananikwepa kwepa kumbe anayake.ITAENDELEA BADADAE KIDOGO