Huyu dada mtu simuelewi kabisa!!

Mwanabalagha

Senior Member
Nov 11, 2015
196
235
Habari za saa hii wananzengo...?

Kiufupi ni kwamba, miaka miwili nyuma kuna msichana mgeni nilimuona mtaani kwangu.Sasa baada ya kupeleleza nikaambiwa amekuja kumtembelea dada yake hapo mtaani, kwasababu aliyavuta macho yangu moyo nao ukataka kutoka kumfuata lakini bahati mbaya ukakwama kwenye kifua hivyo ikabidi urudi tu ndani ukaendelee kuugulia maumivu polepole.

Kiukweli ni msichana ambaye kama wewe ni mwanaume halafu ukakutana nae njiani,usipogeuka kumuangalia tena lazima utakuwa mchawi tu.Nilitokea kumpenda kiukweli...nikaanza kumchombeza taratibu huku nikizingatia vigezo na masharti nisije kuharibu.
Kwa bahati mbaya kabla hatujaelewana vizuri akawa amerudi kwao Babati.Sasa tukaanza kuwasiliana akiwa mbali, na bahati nzuri dada yake alikuwa anajua kinachoendelea hivyo nae akawa anasaidia kumchombeza mdogo wake anikubali arudi huku bongo.

Baadae nikakata tamaa kabisa manake yule msichana alikuwa akiniambia nakuja tarehe fulani....lakini tarehe ikifika haji aliniahidi zaidi ya mara nane kwamba anakuja ila hakufanya hivyo.
Ndipo siku moja nikiwa sina hili wala lile huku nikiwa nimekata mawasiliano nae kabisa, siku hiyo dada mtu alikuja ofisini kwangu na kuniambia kwamba yule binti atakuja kusherehekea sikukuu ya xmass huku hivyo nikae tayari.
Na kweli baada ya siku kama tatu mbele yule msichana akaja....alipofika tu akanitafuta tukaonana na mambo yakaanzia hapo na yakaendelea na mpaka sasa bado yanaendelea.

Kiufupi nimeshamtolea barua bado mahari, sasa dada mtu alimwambia aje tu kwangu aishi wakati anasubiria mahari...kweli binti akaja kwangu tukaanza kuishi huku dada mtu akiwa anakuja siku mojamoja kututembelea hapo nyumbani, cha ajabu sasa huyo dada mtu kabadilika kawa kama anayeona wivu vile mi kuwa na mdogo wake ,mara anamwambia hivyo vihela vya mmeo vitaisha tu we jifanye kuringa kwanza rudi nyumbani mpaka utolewe mahari... bint akaja akanieleza nikamwambia ok! mwambie dada mahari nitaleta baada ya wiki mbili....na umuombe uendelee kukaa huku siku mahari ikikaribia unarudi nyumbani.

Alivyomueleza hivyo akakubali na akamruhusu kuja kukaa nami, cha kushangaza baada ya siku mbili kabadilika tena amempigia simu mpaka baba akamueleza kuwa mdogo wake hayupo pale nyumbani kwake na hajui alipo na kaka yao akamwambie vivyo hivyo wakati anajua yupo kwangu...baba kapiga cm kamwambia afungashe vilago arudi nyumbani....sasa nashindwa kumuelewa huyu dada mtu anataka nini!!!
 
Habari za saa hii wananzengo...?

Kiufupi ni kwamba, miaka miwili nyuma kuna msichana mgeni nilimuona mtaani kwangu.Sasa baada ya kupeleleza nikaambiwa amekuja kumtembelea dada yake hapo mtaani, kwasababu aliyavuta macho yangu moyo nao ukataka kutoka kumfuata lakini bahati mbaya ukakwama kwenye kifua hivyo ikabidi urudi tu ndani ukaendelee kuugulia maumivu polepole.

Kiukweli ni msichana ambaye kama wewe ni mwanaume halafu ukakutana nae njiani,usipogeuka kumuangalia tena lazima utakuwa mchawi tu.Nilitokea kumpenda kiukweli...nikaanza kumchombeza taratibu huku nikizingatia vigezo na masharti nisije kuharibu.
Kwa bahati mbaya kabla hatujaelewana vizuri akawa amerudi kwao Babati.Sasa tukaanza kuwasiliana akiwa mbali, na bahati nzuri dada yake alikuwa anajua kinachoendelea hivyo nae akawa anasaidia kumchombeza mdogo wake anikubali arudi huku bongo.

Baadae nikakata tamaa kabisa manake yule msichana alikuwa akiniambia nakuja tarehe fulani....lakini tarehe ikifika haji aliniahidi zaidi ya mara nane kwamba anakuja ila hakufanya hivyo.
Ndipo siku moja nikiwa sina hili wala lile huku nikiwa nimekata mawasiliano nae kabisa, siku hiyo dada mtu alikuja ofisini kwangu na kuniambia kwamba yule binti atakuja kusherehekea sikukuu ya xmass huku hivyo nikae tayari.
Na kweli baada ya siku kama tatu mbele yule msichana akaja....alipofika tu akanitafuta tukaonana na mambo yakaanzia hapo na yakaendelea na mpaka sasa bado yanaendelea.

Kiufupi nimeshamtolea barua bado mahari, sasa dada mtu alimwambia aje tu kwangu aishi wakati anasubiria mahari...kweli binti akaja kwangu tukaanza kuishi huku dada mtu akiwa anakuja siku mojamoja kututembelea hapo nyumbani, cha ajabu sasa huyo dada mtu kabadilika kawa kama anayeona wivu vile mi kuwa na mdogo wake ,mara anamwambia hivyo vihela vya mmeo vitaisha tu we jifanye kuringa kwanza rudi nyumbani mpaka utolewe mahari... bint akaja akanieleza nikamwambia ok! mwambie dada mahari nitaleta baada ya wiki mbili....na umuombe uendelee kukaa huku siku mahari ikikaribia unarudi nyumbani.

Alivyomueleza hivyo akakubali na akamruhusu kuja kukaa nami, cha kushangaza baada ya siku mbili kabadilika tena amempigia simu mpaka baba akamueleza kuwa mdogo wake hayupo pale nyumbani kwake na hajui alipo na kaka yao akamwambie vivyo hivyo wakati anajua yupo kwangu...baba kapiga cm kamwambia afungashe vilago arudi nyumbani....sasa nashindwa kumuelewa huyu dada mtu anataka nini!!!
Usiyeeleweka ni wewe na si dada mtu. Barua uliitoa kwa nani wakati wazazi wa binti hawajui wala hawakutambui na unakaa na mtoto wao kwa kigezo gani. Kama kweli unampenda mrudishe kwao fanya taratibu za ndoa uhalalishe muishi kihalali.
 
Kiufupi nimeshamtolea barua bado mahari, sasa dada mtu alimwambia aje tu kwangu aishi wakati anasubiria mahari
Kaka sasa si utoe tu mahari ili taratibu zingine zifuate na uhalalishe mambo? Do the right thing man!!! Dada inawezekana ana wivu lakini pia inawezekana roho inamsuta kwa kumruhusu mdogo wake kuishi na wewe ili hali mila na desturi zinaeleweka.
 
Nenda tu kaoe ndio suruhisho la kuwa na kauri juu ya huyo binti vinginevyo mwache arudi kwao dada yupo sahihi tu kwa sababu binti alivyoondoka kwao ilikuwa afukie kwa dada mtu hivyo angepata matatizo dada mtu ndio angeyajibia kwa familia yao.
Ukipenda oa
 
kifupi dada anajishtukia usje ukapeleka mahar na mimba juu ndio maana anakukata stimu anataka utoe mahar kesi yake iishe
 
Watoto wetu wa Kiiraq (endapo atakuwa kabila tajwa) tunawaaga kwa taratibu rasmi na huruhusiwi tu kuchukua Kama nyanya uliyoiokota. Fanya hime wazazi wakujue,utoe mahari kisha uchukue zigo tamu tamu. Nilipoona sofa zake tu,nikajua lazima mtoto atakuwa wa kikwetum
 
Watu wa babati wanapenda uoe wote hawanaga shida na hilo. Mfate huyo dada mtongoze na umgonge utakuwa umemaliza tatizo
 
Nenda kamuoe bhana, yaan alvo kuja kukaa kwako ndo ukajisahau kabsa
Aya changamka uende ala!!
 
We mpaka unapeleka mahari ulijitambulisha kwa nani? Na akina nani walikuwepo?
Walikuwepo wawakilishi wa wazazi wake, yaani dada mtu mama yake mdogo na watu wengine kwenye familia yao.Kifupi ukoo wote unanitambua mama yake nishainana nae kabisa na alikuja kwa ajili ya kuniona tu.
 
Anayejua cv ya Mme wa naibu spika Tafadhali ,maana ikiwa ni week ya kina mama kakataa kuwasikiliza baada ya kudhalilishwa na mbunge wa kiume, kwa vile kwenye cv kuna namba za cmu tutampigia tumwambie mkewe alichofanya si kizuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom