Huwezi Kuamini: Sukari iliyoagizwa na Serikali nayo Imeuzwa kwa bei ya Kuruka!

Shebbydo

JF-Expert Member
Feb 12, 2015
1,174
1,937
Habari wana JF,

Baada ya serikali kuagiza sukari na jana kiasi fulani kuwa kimeingia katika mikoa mbalimbali kwa bei elekezi kama ilivyoelekezwa, nilijua sasa tatizo limekwisha. Tatizo ambalo linaleta taharuki kubwa kwa Watanzania.

Niliyoyaona jana kwenye duka moja la jumla la Mhindi yamenivunja moyo kabisa juu ya mafanikio ambayo niliyatarajia kwa utawala huu usiyokuwa na simile kwa maovu. Nilienda dukani hapo na rafiki yangu alienda kununua sukari kwa ajili ya duka lake. Sukari kilo 50 imeuzwa kwa Tsh.135000/=, inamaana rejareja iuzwe sh.3000/=.

Mchezo ulivyokuwa unafanyika ni "urushaji"(neno hili lilitumika miaka ya nyuma wakati bidhaa kama sukari, sigara na nyinginezo zilipokuwa adimu. Wavuta sigara walikuwa wanauziana kwa "pafu"). Risiti ilikuwa inaandikwa elfu 95 halafu Mhindi anapokea 135000, anakuambia wewe ni mfanyabiashara utajua mwenyewe utauza je.

Sukari hiyo kufikia saa 12 ilikuwa imeisha, wafanyabiashara wa jiji la Mwanza bado wanahaha kutafuta sukari. Mimi nikajiuliza maswali ambayo sikupata majibu. Serikali ilisema sukari hiyo itauzwa rejareja sh. 1800, ambapo kilo 50 isingezidi sh. elfu 70, Sasa bei ya risiti ilikuwa elfu 95, rejareja kilo moja iuzwe 2000, je ni nani anayewasaliti Watanzania? Jumlisha cha juu Mhindi alichokuwa anaweka, utake ununue usitake uwache, mtaani ikiuzwa kilo 3000 Wananchi wataielewa je serikali? Utaratibu wa kuipata hiyo sukari iliyoletwa na serikali upo je?

Wakuu na nyinyi mnaweza toa mawazo yenu, mimi kwangu naona nchi hii ilishaharibika labda zitungwe sheria za kunyonga, kutumbua majipu tu haitoshi.
 
Serikali imeagiza sukari lini?
Hujamsikikiza Majaliwa?na nyingine ipo njiani Tatizo sukari hapo awali ilitumiwa na ccm kupata pesa kwa kuruhusu msamaha wa kodi kama rejesho.Pia sukari ipo tatizo wananchi wanapaniki bure
 
Serikali imeagiza sukari lini?
Imeagiza sukari tani elfu 70 lakini zinakuja kwa awamu jana zimeingia tani kadhaa, walisema leo zitaingia tani kadhaa(nimesahau figure halisi ndiyo maana natumia neno kadhaa). Au sivyo hivyo?
 
Hah.........wakati nimesoma mahali watu tisa wametiwa mbaroni kwa kuuza sukari bei tofauti na ile elekezi.....ss kama na hiyo ya serikali ipo juu tutasimamia wapi?
 
Wenye akili tumeeleza na kuonya mapema suala la sukari ila akina mr-know-all wakawa wanachezesha wanasesere kwa wapumbavu na malofa ili kumfichia mkuu aibu. Sukari inapiga hodi kwenye sh5,000/kg na hata wanayoleta haitarudisha kilo kwenye 1,800 ng'o!!
 
Hivi sigara nayo inaweza kuadimika?! Ntafurahi kuona haipatikani kabisa.
Hiyo ya sigara ilikuwa kitambo lakini kwa sasa sidhani kama inaweza kuadimika. Hii nchi imepitia majaribu mengi. Nakumbuka wakati wa bidhaa kuadimika, kwa mfano sukari ilikuwa ikija kwenye maduka ya ushirika ni foleni kubwa ilikuwepo, ubavu wako ndiyo utakao kusaidia. Kuna mtoto aliwahi kukanyagwa dukani hadi akapoteza maisha.
 
Wenye akili tumeeleza na kuonya mapema suala la sukari ila akina mr-know-all wakawa wanachezesha wanasesere kwa wapumbavu na malofa ili kumfichia mkuu aibu. Sukari inapiga hodi kwenye sh5,000/kg na hata wanayoleta haitarudisha kilo kwenye 1,800 ng'o!!
Kwa nini isirudishe kwenye 1800/= ilihali itauzwa kwa bei ambayo imelenga rejareja iuzwe 1800/= hapo ndipo hujuma inapoanzia.
 
Hili la sukari, hapa lilipofika linahitaji mpango mkakati kabambeee, zaidi serikali ikusanye sukari yote nchini hii uuze kwa usimamizi wa TRA
 
Unamaanisha sukari wanayodai waliagiza walimpa muhndi ndye auze? Sasa sukar aliagiza muhnd au Serkal?
 
Hiyo ya sigara ilikuwa kitambo lakini kwa sasa sidhani kama inaweza kuadimika. Hii nchi imepitia majaribu mengi. Nakumbuka wakati wa bidhaa kuadimika, kwa mfano sukari ilikuwa ikija kwenye maduka ya ushirika ni foleni kubwa ilikuwepo, ubavu wako ndiyo utakao kusaidia. Kuna mtoto aliwahi kukanyagwa dukani hadi akapoteza maisha.
Bro unanikumbusha mbal sana. Hii nch tumepitia meng sana. Nakumbuka ndio tumerud kutoka vitan kumuondoa nduli amin hal ilikuwa mbaya sana had hapo 1984 yan nguo ni viraka tuu. Iliniuma sana kuona kwa macho yang wafanya biashara wakimwaga sukar mton. This thing has been a Trauma to me for the last three decades.
 
Back
Top Bottom