Huwezi amini, nilibakia mimi tu

Huwezi amini, nilibakia mimi tu

mtimawachi

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2020
Posts
2,106
Reaction score
3,158
Habari zenu wanasiasa? Nakumbuka tarehe 08/04/2021 nilikuwa nasafiri kuelekea kisiwa cha PATMO usiku kwa ndege

Mle ndani mlikuwa na abiria wengi kutoka mataifa mbalimbali ya wazungu na wengi wao wakiwa makomandoo na viongozi maarufu wa dini.

Kutoka nchi yetu tulikuwa wawili tu.Abiria wote walikuwa wana bashasha isipokuwa abiria mmoja tu ambaye ni mimi, mawazo yangu yalikuwa mbali sana,niliathiriwa sana na kifo cha bwana YOHANA(yule wa tarso).Hivi nini kilimkuta!? Alikufa tu ? aliuawa? Na kama aliuawa nani alihusika? mayahudi? au warumi.?

Na haya makundi ya masadukayo yaliyozuka kumtukana Yohana au lile kundi la mafarisayo linalodai lichanjwe chanjo ya TAUNI wanafanya hayo kwa mamlaka gani?

Nikiwa nawaza ghafla nikagutushwa na kelele za abiria na myumbo wa ndege tulopanda,kumbe ndege ilikuwa inaanguka,kama hiyo haitoshi magaidi wakatusindikizia na bomu kabisa,ndege ikalipuka

Baadae najikuta naning'inia juu nyaya za umeme HV 132kv.

Kipindi najiuliza nitatoka vipi pale nikaona kundi la magaidi linakuja,kwa kasi kuja kumalizia kama kuna mabaki si ndo wakaniona pale juu,wakaanza nivurumishia risasi ikabidi nijiachie,kufika chini tu nikaangukia kwenye kisiki kilichochongoka lakini niliondoka eneo lile bila kuacha alama licha ya kuwa nilikuwa navuja damu

HUWEZI amini kwenye AJALI ile nilibakia mimi,MIMI TU WA KUWALETEA HABARI!

Eti leo ndio niogope kufa kisa tauni!! eti nichanjwe!!

Hii chanjo isikatazwe, iletwe mwenye kuogopa kufa akadungwe,Kusiwepo shinikizo

Mwambieni the Empress asiumize kichwa kuunda tume kwani itakuja na majibu ambayo tayari tunayo ila asiweke shinikizo kwani wengine tayari tuna nusura ya asili kwa kila jambo

Kule kwenye ajali yetu walikufa makomando,viongozi wa dini licha ya maombi waliyokuwa wakiomba ila nilibakia mimi,mimi tu wa kuwaletea habari.

NB: Maono haya nilishushiwa nikiwa katika KISIWA CHA PATMO
 
Lema umerudi tena? Haya twambie umeoteshwa nani anakufa soon asipotubu madhambi yake?
 
Habari zenu wanasiasa? Nakumbuka tarehe 08/04/2021 nilikuwa nasafiri kuelekea kisiwa cha PATMO usiku kwa ndege

Mle ndani mlikuwa na abiria wengi kutoka mataifa mbalimbali ya wazungu na wengi wao wakiwa makomandoo na viongozi maarufu wa dini...
Hadithi zenye utundu mwingi na tungo tata ,haya pole mzee wa Patmo!
 
Sawa Dr. Uliponea. Nilikuwa nakucheki ulipoletwa mbele za kamera kuthibitsha tetesi. Hakika ulikuwa umedhoofu Sana,unakohoa na kuongea na wananchi wa PATMO kwa taabu. Mungu akupe maisha marefu
 
Empress anatupeleka sehemu sahihi baada ya emperor kuondoka na hata rudi tena, mana inasemaka kaumiza wengi mpaka yule mfalme wa kaskazini nae alikosa punzi ya kutoa pesa yake, Jambo la kushukuru kupona katika ajali.
 
Empress anatupeleka sehemu sahihi baada ya emperor kuondoka na hata rudi tena, mana inasemaka kaumiza wengi mpaka yule mfalme wa kaskazini nae alikosa punzi ya kutoa pesa yake, Jambo la kushukuru kupona katika ajali.
Yule mtu alikuwa na nia njema, ukiachana na siasa za vyama.
 
Empress anatupeleka sehemu sahihi baada ya emperor kuondoka na hata rudi tena, mana inasemaka kaumiza wengi mpaka yule mfalme wa kaskazini nae alikosa punzi ya kutoa pesa yake, Jambo la kushukuru kupona katika ajali.
Empress hatuwezi kumpima sasa tumpe muda licha kuonyesha madhaifu baadhi
 
Sawa Dr. Uliponea. Nilikuwa nakucheki ulipoletwa mbele za kamera kuthibitsha tetesi. Hakika ulikuwa umedhoofu Sana,unakohoa na kuongea na wananchi wa PATMO kwa taabu. Mungu akupe maisha marefu
Asante mkuu,bado nauguza majeraha nikiwa huku patmo
 
Nimebaki na ukumbusho wako wa hii picha ulipoanguka kutoka angani katika Boeing 737.
IMG_20210405_160849.jpg
 
Back
Top Bottom