Huwa Sipati Jibu

Huwa Sipati Jibu

Iceman 3D

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2016
Posts
20,611
Reaction score
67,105
Nakumbuka zamani(miaka michache tu iliyo pita) sikuwa mkubwa sana na wala sikuwa mdogo sana, kuna msichana alikuja kwetu , kipindi hicho nilikiwa nakaa mkoani, basi yeye alitoka Dar, na alikuwa mzuri tuu kiasi kwamba mwanaume yeyote angependa kuwa naye,yule dada alinipenda kweli kweli tena bila sababu, (labda kwa sababu nilikuwa kijana wa mkoani), mpaka kuna vijana wengine kitaa wakawa wana nichukia kwa kuchoropoa ndege wao, basi na mimi huwa nina tabia ya kumpenda anaye nipenda, nami nika mpenda tena saaanaa, yeye elimu ilimshinda(japo alikuwa na akili sana za kawaida) ila mimi nilikuwa bado nasoma
sasa nakumbuka akaanza kujisogeza nyumbani kwa mama, anakuja anamsaidia mama kazi, lakini ilitokea tuu mama hakumkubali toka siku ya kwanza baadaye akawa akija hasa mimi nikiwa shule mama ana mwambia nenda tuu kwenu hatuna cha kufanya hapa na mengine mengi, Pia nikirudi hom likizo mama akawa ana niwakia kabisa kuwa hamtaki mtoto kama huyo na hampendi, tena kama wasichana wamenishinda ni bora nika somee u padri tuu... Ki ufupi kwa mwendo huo ikabidi nimwache kwa sababu mi nikiwa na mtu huwa napenda kuweka plani za muda mrefu labda itokee shida tuu, na Lakini nikiangalia mapoyoyo ambao niliwapata baada ya huyo kwa kweli ni shida tupu, mpaka leo huwa nakumbuka kuwa mama alifanya nika mwacha mtu wa maana na liye nipenda kwa jinsi nilivo, tena kwa dhati (japo huwa simlaumu mama wala sijawahi mwambia lolote)

Nakumbuka siku tumekubaliana tuachane aliniambia "najua una niacha kwa sababu ya mama yako" japo nilijitahidi kumsitiri mama yangu, ila huo ndo ulikuwa ukweli, basi huwa sisahau mpaka kesho

*Mwisho wa siku huwa nasema sijui ninge endelea naye tuu!!?_ au pengine ndo mipango ya huyo wanaye dai ndiye Mungu!!, saa nyingine nahisi mama kama alikuwa dikteta kiaina, saa nyingine ndo naona labda ndo wazazi wa kiafrika huwa hawakosei!!!
*ni kama sjielewi elewi hivi! Ki ukweli huwa sipati jibu
 
Nenda kamtake radhi mama yako kwa kumuita dikteta uchwara,Mungu anakuona na hizo zarau zako
 
Nenda kamtake radhi mama yako kwa kumuita dikteta uchwara,Mungu anakuona na hizo zarau zako
Hamna mkuu wala sina lengo la kumdharau, ila ni kweli nilifika stage nika waza hivo.
Tena namuheshimu kweli kweli
Mtingozi
 
yan huwezi amini mkuu, sijategemea kama hyi stories yako imeishia hapo, nlidhani no bonge la love story yan, ndani yake kungekuwa na uaaliti, but very interesting sababu, Dada alishaanza kujiongeza kufanya kazi ndogondogo home kwenu but haikuwa bahati......!
 
Hii chai yakichochezi.
Hahaha
Hapana mkuu, watu huwa wanagombana na wazazi wao mambo kama haya
Ila mimi wala! nilifanya ki amani japo ilikuwa ngumu tuu sema ndio huwa kila siku nawaza kwa nini ilitokea
 
yan huwezi amini mkuu, sijategemea kama hyi stories yako imeishia hapo, nlidhani no bonge la love story yan, ndani yake kungekuwa na uaaliti, but very interesting sababu, Dada alishaanza kujiongeza kufanya kazi ndogondogo home kwenu but haikuwa bahati......!
Ni kweli ndugu na toka mwanzo alikuwa anapenda awajue hom, yaan hata mimi nilisha kuwa nime ridhika naye sema nikaona hapa kwa drama zinazo endelea labda siyo riziki yangu hiyo, nimuache tu apate mtu mwingine
 
Mzaz ni chanzo cha matokeo mabaya na mazuri kwa mtoto., kwa upande wa matokeo mazuri wanapatia asilimia chache sana thus kuwa na maamuzi magumu yenye msimamo wa hatar ili kulinda thaman yako., Aya Sasa utakuta yeye kalipenda poyoyo ambalo kenye hesabu zako hata kwa asilimia -0.000000000000001 huja wahi mfikilia
 
Yaani we unaacha mutoto kisa duu lakini ulisema ulikuwa mtoto natumaini sasahivi akili hizo hauna maana kama bado unazo mmmh nishiida
 
Eeh mkuu
Duniani kuna Mungu zaid ya 500
Ni madai tuu hayo.
Niliweka hivo ili niwe neutral
Mkuu ukisema kuwa zaidi ya 500 ni kuundermine actually ni zaidi ya 5000... ! So chagua mungu wako kutoka humo.. !
 
Back
Top Bottom