Huu ujinga unaoitwa "PRANK" ni wa kukemewa

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,221
22,286
Ninawasalimu kwa jina la Chama pendwa, CCM.

Kwanza tuanze kufahamu nini maana ya PRANK. Kwa tafsiri nyepesi ni mzaha wa kumfanyia mtu ili kujifurahisha. Yaani kama utani tu. Sio jambo geni kwasababu hata majumbani mwetu wanafamilia huwa tunataniana sana. Kwa mfano mama na mwana au mara chache tunamtania baba ila kwa tahadhari ya hali ya juu maana BABA HAZOELEKI.

Tofauti na hizi pranks zetu za asili, hii ya mitandaoni imefikia pabaya sana ili mradi tu mtu apate views. Yaani comedians wamefikia hatua mbaya mno. Kuna mizaha wanayofanya inaleta mishtuko mikubwa sana kwa watu kiasi kwamba hata kifo kinaweza tokea. Imagine huna hili wala lile mtu anakuwekea nyoka wa bandia shingoni... huko YOU TUBE ukiingia utaona mengi sana. Mtu akikasirika ndo utasikia eti "tunarekodi". Binafsi ukinifanyia mzaha wa kunishtua au kutweza utu wangu haitaisha salama... sitaelewa kabisa.

Kwenye video ni prank ya jamaa anawabusu kina dada barabarani. Huu ni ujinga mtupu anaoletwa na kuiga upumbavu wa Magharibi.

 
Kuna mpumbavu mmoja aliwahi nirushia nyoka mdogo wa bandia nilikimbia barabarani. Cha kushukuru Mungu usiku ule kulikuwa na foleni lasivyo nisingekuwepo hapa kutype.

Huu ujinga ukemewe kabisa. Siku mtu akinitania jamani sitajali kama ni prank au prunku au vipi kitakachompata atajuta aisee
 
Kuna mpumbavu mmoja aliwahi nirushia nyoka mdogo wa bandia nilikimbia barabarani. Cha kushukuru Mungu usiku ule kulikuwa na foleni lasivyo nisingekuwepo hapa kutype.

Huu ujinga ukemewe kabisa. Siku mtu akinitania jamani sitajali kama ni prank au prunku au vipi kitakachompata atajuta aisee
mwaka fulani nilikua nakatiza mitaa ya Kariakoo, ghafla machinga ananiletea usoni nyoka wa plastic eti anauza..asee kidogo nigongwe na gari mana niliruka na nilivyobeba vyote vikaanguka yule mpuuzi sijui aliwaza nini!
 
mwaka fulani nilikua nakatiza mitaa ya Kariakoo, ghafla machinga ananiletea usoni nyoka wa plastic eti anauza..asee kidogo nigongwe na gari mana niliruka na nilivyobeba vyote vikaanguka yule mpuuzi sijui aliwaza nini!
watu wanakera sana huwa hawawazi matokeo, sasa mimi ile siku nilinusurika ajali mbili. Kwanza niliruka kikaango cha mafuta ya moto kipo motoni halafu nikakimbilia barabarani.

Nilikuwa ofisini kwangu, aliyenitishia alikuwa fundi cherehani jirani mpaka leo namchukia. Ukunga niliopiga watu wote hadi upande wa pili wa barabara walitoka kuangalia. Nililia kama mtoto watu walinionea huruma na kunicheka.
 
watu wanakera sana huwa hawawazi matokeo, sasa mimi ile siku nilinusurika ajali mbili. Kwanza niliruka kikaango cha mafuta ya moto kipo motoni halafu nikakimbilia barabarani.

Nilikuwa ofisini kwangu, aliyenitishia alikuwa fundi cherehani jirani mpaka leo namchukia. Ukunga niliopiga watu wote hadi upande wa pili wa barabara walitoka kuangalia. Nililia kama mtoto watu walinionea huruma na kunicheka.
Pole sana Chief!
 
Kuna prank WA washkaji wa Dubai, inaitwa Gold prank.

Yaan unakuta mtu anamfukuzia pisi Kali akiwa kawaida tu kama Hana pesa hv.

Kwa kawaina manzi ataruka futi nyingi Sana.

Baadae jamaa anarudi akiwa Kashine balaa na Maserati yenye rangi ya gold Hadi rims z gold.

Ndipo manzi atamuelwewa jamaa baada ya kujua ndo yule WA mida Ile alomkataa huanza kuona aibu .ooh inafrahsha sana.
 
Kuna mpumbavu mmoja aliwahi nirushia nyoka mdogo wa bandia nilikimbia barabarani. Cha kushukuru Mungu usiku ule kulikuwa na foleni lasivyo nisingekuwepo hapa kutype.

Huu ujinga ukemewe kabisa. Siku mtu akinitania jamani sitajali kama ni prank au prunku au vipi kitakachompata atajuta aisee
mpaka nime zoom Avatar yako, pole sana kwa kuwekewa nyoka.
 
Back
Top Bottom