MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,221
- 22,286
Ninawasalimu kwa jina la Chama pendwa, CCM.
Kwanza tuanze kufahamu nini maana ya PRANK. Kwa tafsiri nyepesi ni mzaha wa kumfanyia mtu ili kujifurahisha. Yaani kama utani tu. Sio jambo geni kwasababu hata majumbani mwetu wanafamilia huwa tunataniana sana. Kwa mfano mama na mwana au mara chache tunamtania baba ila kwa tahadhari ya hali ya juu maana BABA HAZOELEKI.
Tofauti na hizi pranks zetu za asili, hii ya mitandaoni imefikia pabaya sana ili mradi tu mtu apate views. Yaani comedians wamefikia hatua mbaya mno. Kuna mizaha wanayofanya inaleta mishtuko mikubwa sana kwa watu kiasi kwamba hata kifo kinaweza tokea. Imagine huna hili wala lile mtu anakuwekea nyoka wa bandia shingoni... huko YOU TUBE ukiingia utaona mengi sana. Mtu akikasirika ndo utasikia eti "tunarekodi". Binafsi ukinifanyia mzaha wa kunishtua au kutweza utu wangu haitaisha salama... sitaelewa kabisa.
Kwenye video ni prank ya jamaa anawabusu kina dada barabarani. Huu ni ujinga mtupu anaoletwa na kuiga upumbavu wa Magharibi.
Kwanza tuanze kufahamu nini maana ya PRANK. Kwa tafsiri nyepesi ni mzaha wa kumfanyia mtu ili kujifurahisha. Yaani kama utani tu. Sio jambo geni kwasababu hata majumbani mwetu wanafamilia huwa tunataniana sana. Kwa mfano mama na mwana au mara chache tunamtania baba ila kwa tahadhari ya hali ya juu maana BABA HAZOELEKI.
Tofauti na hizi pranks zetu za asili, hii ya mitandaoni imefikia pabaya sana ili mradi tu mtu apate views. Yaani comedians wamefikia hatua mbaya mno. Kuna mizaha wanayofanya inaleta mishtuko mikubwa sana kwa watu kiasi kwamba hata kifo kinaweza tokea. Imagine huna hili wala lile mtu anakuwekea nyoka wa bandia shingoni... huko YOU TUBE ukiingia utaona mengi sana. Mtu akikasirika ndo utasikia eti "tunarekodi". Binafsi ukinifanyia mzaha wa kunishtua au kutweza utu wangu haitaisha salama... sitaelewa kabisa.
Kwenye video ni prank ya jamaa anawabusu kina dada barabarani. Huu ni ujinga mtupu anaoletwa na kuiga upumbavu wa Magharibi.