Aina ya sanaa anayofanya "Lipota wa Mchongo" ina walakini mkubwa na unaweza kuna kumletea madhara makubwa

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,845
Ni aina ya sanaa mfanano wa prank (kuwafanyia wengine mizaha), lakini ya kwake ikiwa pengine kwa kukosa umakini na miongozo inawadhalilisha na kutweza utu wa watu.

Kusingizia kwa mzaha tuhuma mbalimbali na kubadili maneno ya anayemhoji ni mtindo anaoupendelea zaidi
Ni kweli kafanya ubunifu wa sanaa unaomuingizia kipato lakini sasa anatakiwa kuwa na miongozo yakinifu ili asivuke mipaka ya mizaha na kujikuta anadhalilisha watu wenye staha zao.

Hilo tayari limeshamletea shida mahali pengi na kujikuta anaambulia vipigo vya wastani, lakini si kila siku ni Jumapili atakuja kuingia mahali pasipohitaji mizaha na kukuta watu/mtu ana stress zake akabamizwa akaumizwa sana hata kupelekea majeraha makubwa, ulemavu na si ajabu hata kifo!

Nina hakika hajajikatia bima ya sanaa anayofanya, ili likimtokea la kumtokea asianze kutembeza bakuli la msaada

Serikali nayo kupitia BASATA na BAKITA wampe miongozo sahihi ili aweze kufanya sanaa yake kwenye misingi isiyovuka staha na privacy za watu

Hakuna kitu kinakosa bahati mbaya.. Lakini iwe bahati mbaya kweli na si kwasababu ya uzembe na kutofuata

Miongozo

hqdefault.jpg
20240116_025024.jpg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Misikiti imekuwa mingi sana mitaani! Kuna mingine imejengwa vijijini porini kando ya barabara kuu wala hakuna wa kusali huko!

Hii misikiti mingi nani anasali huko, kuna ambaye ana muda wa kupoteza ndani ya majengo hayo eti anasali? Bora wangejenga viwanda, shule, vitu ambavyo ni potential kwa wananchi wote
 
  • Mshangao
Reactions: rr3
Misikiti imekuwa mingi sana mitaani! Kuna mingine imejengwa vijijini porini kando ya barabara kuu wala hakuna wa kusali huko! Hii misikiti mingi nani anasali huko, kuna ambaye ana muda wa kupoteza ndani ya majengo hayo eti anasali? Bora wangejenga viwanda, shule, vitu ambavyo ni potential kwa wananchi wote
bilashaka unamanisha dodoma
 
Misikiti imekuwa mingi sana mitaani! Kuna mingine imejengwa vijijini porini kando ya barabara kuu wala hakuna wa kusali huko! Hii misikiti mingi nani anasali huko, kuna ambaye ana muda wa kupoteza ndani ya majengo hayo eti anasali? Bora wangejenga viwanda, shule, vitu ambavyo ni potential kwa wananchi wote
Hili ni la kiimani zaidi na linahusika na hisia za watu direct.. Hakuna kitu delicate kama imani ya dini.. Tumakinike!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Misikiti imekuwa mingi sana mitaani! Kuna mingine imejengwa vijijini porini kando ya barabara kuu wala hakuna wa kusali huko! Hii misikiti mingi nani anasali huko, kuna ambaye ana muda wa kupoteza ndani ya majengo hayo eti anasali? Bora wangejenga viwanda, shule, vitu ambavyo ni potential kwa wananchi wote
Fungulia Uzi uweke na picha na video
 
Ni aina ya sanaa mfanano wa prank (kuwafanyia wengine mizaha), lakini ya kwake ikiwa pengine kwa kukosa umakini na miongozo inawadhalilisha na kutweza utu wa watu...
Umetekeleza wajibu wako vema sana, jukumu ni lake sasa ama kuzingatia ushauri na kusonga mbele au kupuuzia ushauri na kurudi nyuma na pengine kupotea kabisa kwenye tasnia..

Yangu macho, namtakia sanaa njema isiyovuka mipaka ya faragha na utu wa wengine ...
 
Misikiti imekuwa mingi sana mitaani! Kuna mingine imejengwa vijijini porini kando ya barabara kuu wala hakuna wa kusali huko! Hii misikiti mingi nani anasali huko, kuna ambaye ana muda wa kupoteza ndani ya majengo hayo eti anasali? Bora wangejenga viwanda, shule, vitu ambavyo ni potential kwa wananchi wote
 
Back
Top Bottom