Nilibahatika kupata mchumba hivi karibuni ambaye tulifahamiana muda mrefu tangu kipindi tunasoma sekondari takribani miaka 10 iliyopita. Wakati wote huo alikuwa rafiki yangu wa karibu ambaye tulishirikiana vizuri sana katika masomo. Japo binafsi sikuwahi kufikiria juu ya uhusiano wa kimapenzi kati yake na mimi, yeye anadai alikuwa akinipenda sana na kwamba aliteseka sana kimawazo juu yangu lakini alishindwa kuniambia kutokana na aibu za kike na kwa kuwa mawazo yangu wakati huo yalikuwa kwa mtu mwingine. Tangu tulipomaliza sekondari hatukuwahi kukutana wala kuwa na mawasiliano yoyote mpaka 2010 ndipo tulipoamua kuitumia nafasi hiyo kuambiana ya moyoni. Uhusiano wetu umekuwa na vipindi vya amani na furaha lakini zengwe kama kawaida halikosekani. Msichana huyu ana wivu uliopitiliza ambao kusema kweli haunipi raha hata kidogo. Anaona wivu hata kwa msichana wangu tuliyeachana miaka 10 iliyopita na ambaye wala sina mawasiliano naye kwa kipindi chote hicho. Wakati fulani aliwahi kuniambia nim'jaze' mimba ili tu awe na uhakika sitamuacha! Sikuafikiana naye kwani sikuwa tayari kubeba majukumu ya kuwa baba kwa wakati huo. Anaponikosea huwa namsamehe wala simuwekei kinyongo chochote kwani natambua wazi binadamu hatujakamilika. Ninapomkosea hali huwa tofauti. Nadhani anadhani anastahili kupokea msamaha zaidi yangu na hukasirika hata kwa vitu vidogo ambavyo kama angetulia na kufikiri kwa kina angegundua si vitu vya kukasirika. Tukitulia huwa namfafanulia juu ya kile kilichomkasilisha, ananielewa na kuomba msamaha kwa hasira za haraka alizoonesha. Hivi karibu alini'beep' kwenye simu yangu ya mkononi. Kwa bahati mbaya simu yangu haikuwa na credit na tayari ilikuwa usiku hivyo nilishindwa kuwasiliana naye kwa usiku ule japo aliendelea ku'beep' kwa muda mrefu. Asubuhi nilimtumia message kumuomba msamaha na kumuelezea kilichotokea lakini hakujibu. Vipo vituko vingine vingi anavyofanya kutokana na wivu. Mawasiliano kati yangu na yeye siyo mazuri hivi sasa. Ninaogopa endapo tutaoana maisha ya ndoa yatakuwa mzigo mzito kwetu sote na watoto. Natambua fika kwamba wivu ni sehemu ya mapenzi lakini unapopitiliza humaanisha nini? Upendo uliopitiliza au?. Nimfanyaje mpendwa huyu? Naombeni ushauri wenu wapendwa.
Gates
Peace & Love
Gates
Peace & Love