Huu ni udhaifu wa TFF kupandanisha timu ya taifa, Simba na Azam

Team JPM

JF-Expert Member
Nov 11, 2018
1,074
1,608
Watanzania wengi ni wapenzi wa michezo haswa Soka, lakini pia ni washabiki wa timu za taifa na vilabu vilevile haswa Simba, Yanga na Azam.

Watanzania hupenda burudani ya mpira kwa kutazama uwanjani, kwenye Tv au kusikiliza redioni.

Leo Novemba 23, Timu ya Taifa ya mpira wa miguu kwa upande wa wanawake inacheza nusu fainali na timu ya Taifa ya Uganda baada ya kuzifunga Burundi, Zanzibar na Ethiopia.

Wakati huo huo, Azam ipo Mwanza inachuana na Mbao FC wakati Simba inachuana na Ruvu Shooting katika Uwanja wa Taifa.

Mechi zote tatu kubwa zinachezwa saa kumi kamili hivyo Watanzania watagawanyika katika kutazama. Ama utazame timu ya taifa, Simba vs Ruvu Shooting au Azam vs Mbao. Kama TFF wangekuwa makini, hizi mechi zingetenganishwa muda.

Hii ingetupatia mashabiki fursa ya kupata burudani zote. Pia mapato yangeongezeka maana wapo ambao wangependa kutazama mechi mbili au zote.

Afisa Mipango wa TFF ajitathmini.
 
Mkuu Wakati mwingine utambue utofauti wa Michuano ya CECAFA na ile ya TFF. Ipo siku utataka TFF iingilie ratiba ya CAF au FIFA kabisaa ili uridhike.

Yaani VPL ipindishe ratiba kuepa mashindano ya CECAFA ya Wanawake? Maajabu haya.
 
Mkuu Wakati mwingine utambue utofauti wa Michuano ya CECAFA na ile ya TFF. Ipo siku utataka TFF iingilie ratiba ya CAF au FIFA kabisaa ili uridhike.

Yaani VPL ipindishe ratiba kuepa mashindano ya CECAFA ya Wanawake? Maajabu haya.
Katika kitu wamefeli TFF ni upangaji wa ratiba inasemakana ligi inasimama tena mpk jan na january itanza ikifika mapinduzi isimame tena.
 
TFF hawakujua ratiba ya CeCAfa?wajiijua.Mechi ya azam au simba moja ingechezwa kesho au mechi ya chamazi ingechezwa saa1 jion mbona hilo liko wazi sana.
Mkuu Wakati mwingine utambue utofauti wa Michuano ya CECAFA na ile ya TFF. Ipo siku utataka TFF iingilie ratiba ya CAF au FIFA kabisaa ili uridhike.

Yaani VPL ipindishe ratiba kuepa mashindano ya CECAFA ya Wanawake? Maajabu haya.
 
Back
Top Bottom