Nimatumaini yangu kuwa mko poa.mimi ni kijana wa miaka 28,mwanafunzi wa mwaka wa 3 hapa SAUT mwanza,nasomea masuala ya uhasibu.mwaka 2006 nikiwa form 5 pale META sekondari-Mbeya nilibahati kupata girlfriend ambaye kwa wakati huo alikuwa form 4.kifupi tulipendana sana mpaka nikamshawishi ajiunge na kidato cha tano hapo hapo shuleni kwetu META,kweli binti akaanza form 5 pale shuleni kwetu ikawa yeye form 5 mi form 6.mpaka nikamaliza shule nikaondoka kurudi kwetu rufiji.tukaendelea kuwasiliana kwa muda kama wa miezi 8,baada ya hapo mawasiliano yakaanza kusumbua mara anapatikana mara hapatikani,nikimwuli tatizo akasema simu mbovu inamsumbua.baadae yakakatika kabisa,yeye alimaliza form 6 nakupata nafasi pale MKWAWA university,ila mim sikufanya vizuri nikalazimika kusoma diploma pale CBE dodoma.hivyo mwenzangu amemaliza chuo mwezi 6,mim ndo niko mwaka wa 3.tatizo linalo nikabili ni kwamba amerudi anataka tufanye maisha,nikamwuliza ulikuwa wapi miaka yote tangu umeanza chuo uje unitafute baada ya kumaliza chuo? Sikupata jibu.nikamwuliza je miaka yote hiyo hajapata mtu? Akaniambia alikuwa naye wameachana.pia kwa upande wangu niko kwenye mahusiano ambayo yanazaidi ya miaka 2 na nusu.ndugu zangu nimebaki njia panda cjui nini cha kumsaidia.naomba msaada wa mawazo toka kwenu.