huu ndo upendo wa kweli?

huu ndo upendo wa kweli?

Unapouliza ushauri, ina maana unataka tukupe mawazo ambayo yatamuathiri huyo ulie nae sasa, kumaanisha humthamini ndo maana unafikiria upuuzi wa demu wa zamani..!
Kuwa mwanaume, jifunze kama katika dhiki hakukupenda, hakuona umuhimu wako, leo amekwama kakurudia vipi kesho unajua itakuaje?

Thou wahenga wa zama hizi wanasema ;-

.Ukiona anakupenda...jua kuna mjinga kashalizwa..
.Zakuambiwa...changanya na za kwako..
 
baby come back kwenye maisha ya kweli haijawahi kufanya kazi mkuu!
songesha na maisha yako achana na huyo mtu wewe.
 
Kwa mfano huyu gf mpya utamuachaje?acha 'sambi' em mtel uyo zilipendwa kuwa unam2 na mnamalengo tayari. Ila asijali wewe utamuombea apate mpya atakaemjali,ila u'l be there 4her 4any advice!takecare
 
Hakuna cha kukuchanganya hapo, yaani wewe demu huyo anataka kukutumia kama substitute eti aliekuwa nae wameachana so wahat.Mwambie wewe upo commuted na huyo ulie nae basi na kama huyo ulienae ni kimeo basi tafuta mwingine maana huyo mwalimu wa Mkwawa wamemchakachua the wamemwaga ndo sasa anakutafuta.At the end of the day haya ni mawazo yetu but wewe kama wewe uangalie moyo na uusikilize moyo unakuambia nini
 
Nimatumaini yangu kuwa mko poa.mimi ni kijana wa miaka 28,mwanafunzi wa mwaka wa 3 hapa SAUT mwanza,nasomea masuala ya uhasibu.mwaka 2006 nikiwa form 5 pale META sekondari-Mbeya nilibahati kupata girlfriend ambaye kwa wakati huo alikuwa form 4.kifupi tulipendana sana mpaka nikamshawishi ajiunge na kidato cha tano hapo hapo shuleni kwetu META,kweli binti akaanza form 5 pale shuleni kwetu ikawa yeye form 5 mi form 6.mpaka nikamaliza shule nikaondoka kurudi kwetu rufiji.tukaendelea kuwasiliana kwa muda kama wa miezi 8,baada ya hapo mawasiliano yakaanza kusumbua mara anapatikana mara hapatikani,nikimwuli tatizo akasema simu mbovu inamsumbua.baadae yakakatika kabisa,yeye alimaliza form 6 nakupata nafasi pale MKWAWA university,ila mim sikufanya vizuri nikalazimika kusoma diploma pale CBE dodoma.hivyo mwenzangu amemaliza chuo mwezi 6,mim ndo niko mwaka wa 3.tatizo linalo nikabili ni kwamba amerudi anataka tufanye maisha,nikamwuliza ulikuwa wapi miaka yote tangu umeanza chuo uje unitafute baada ya kumaliza chuo? Sikupata jibu.nikamwuliza je miaka yote hiyo hajapata mtu? Akaniambia alikuwa naye wameachana.pia kwa upande wangu niko kwenye mahusiano ambayo yanazaidi ya miaka 2 na nusu.ndugu zangu nimebaki njia panda cjui nini cha kumsaidia.naomba msaada wa mawazo toka kwenu.

MKUU ACHANA NAYE! ALIKUDHARAU TOKA KITAMBO.... NA UKIFANYA KOSA KUMUACHA ULIYE NAYE SASA MAISHA YENU NA HUYU WAZAMANI YAKAKUWA KAMA HIVI.....




tumblr_md79i5Mmey1qzlo65.jpg


 
si umwambie kuwa unae mtu?kwani tatizo liko wapi?au uliekuwa nae huna mapenzi kama ex wako?maana vitu vyengine wala sio vya kuuliza wakati jibu unalo
 
Dogo acha ushamba, hilo siyo suala la kuamba ushauri stand as a man. Yaani kweli umegeuka dhahabu kwake baada ya kutemwa huko alikokuwa? Mwekee wimbo wa 20%...uliponitosa miee...aah..nilikubembeleza ukakataa ..maa ,sikuwa na kosa mie...endelea ,ningekusamee..ilaa..ilaa..syo kimapenzi...ningekuwa nawee..ilaa , nimeshapata mpenzi...endelea

nimeipenda hio mkuu,wimbo huo unamgusa direct....sasa kama emeachwa na jamaa yake mwingine anataka nn kwako?kwann ww ulimuacha,si aliamua kwenda?umeshakuwa kwenye ukurasa mpya,fanya mambo na uliye naye saizi
 
Niliambiwa na babu yangu,,mwanamke aliyeweza kuruka mto mkubwa kumfuata mwanaume ampendae hatashindwa kumwacha mwanaume yule kama mwanaume mwingine atamwita ng'ambo ya mto mwingine..Silaha nyingine ya mwanamke ni machozi yake
TAFAKARI
 
kweli huku ndo JF,kunautofati mkubwa na fb...napenda nichukue nafasi hii kuwashukuru wote kwa ushauri wenu kwangu.mungu awabariki.together we can make changes.
 
Kama sijakosea umesema unasoma uhasibu, fanya cost-benefit analysis kwa hizo option mbili ulizonazo then u can decide.
 
Back
Top Bottom