Huu ndio utajiri mkubwa kuliko wote duniani...

Huu ndio utajiri mkubwa kuliko wote duniani...

Kila mtu kwa nafasi yake anausaka utajiri kwa nguvu zake zote na kwa akili yake.Kkila mtu akilini mwake anaamini fedha na mali ndio kila kitu katika maisha yake.Wengi wanaamini kuwa huzuni walizo nazo, mateso waliyo nayo , na mahangaiko waliyo nayo duniani hapa duniani yataondoshwa na fedha.

Kila mmoja hutumia kila mbinu haijalishi ziwe za halali au ziwe za haramu kujipatia fedha na kujilimbikizia fedha.

Kuna watu wameshaitoa sadaka miili yao kwa ajili ya fedha au utajiri.

Wengine mpaka huwa wanawatoa kafara ndugu zao au hata wazazi wao kwa ajili ya mali na fedha.

Lakini cha kushangaza hao wote wanaotafuta fedha na mali wanajikuta bado hawana furaha maishani mwao hata baada ya kupata hizo fedha na mali.

Bado hawana amani ndani ya nafsi zao.

Walikuwa hawajui kuwa utajiri wa mtu na umasikini wa mtu unaanzia moyoni mwake.

Hapa namaanisha kuwa siri ya kwanza ya utajiri ni ridhiko la nafsi yako.

unatakiwa ujifunze kuridhika na kile ambacho unakipata hata kama ni kidogo kwani kwa kawaida mwanadamu hajawahi kuridhika na hatawahi kuridhika mpaka mwisho wa dunia.

Unatakiwa uijaze nafsi yako utajiri ili upate furaha ya kweli maishani mwako.

Kwa kukosa ridhiko la nafsi na roho watu wengi hutumia kipindi chote cha maisha yao kuhangaikia mali ambapo hawapati hata muda wa kufurahia kile kidogo walichovuna kwani kwenye maisha yao wanaamini bado hakiwatoshi.

Si ajabu kusikia mtu ana miezi sita hajakutana na familia yake kwa sababu yupo mbali akizisaka fedha na mali.

Watu wa aina hiyo wao huwa wanaamini kuwa bado wana kipindi kirefu cha kuishi hapa duniani kwa hiyo wanatakiwa wawe na mali nyingi ili waweze kuishi miaka mingi ya amani na furaha hapa duniani.

Siri ya pili ni kumjua MUNGU na sababu ya uwepo wako hapa duniani.

Unatakiwa ujue kuwa hapa duniani mwanadamu ni kama msafiri aliyepumzika chini ya kivuli cha mtu..nikiwa na maana bado safari yake inaendelea na ni lazima iendelee kwani hapa duniani sio makazi yake ya milele bali ni mpitaji tu.

Ndio maana watu kwa kunogewa na ulimwengu hushikwa na bumbuwazi wakisikia mtu amejenga nyumba yake nzuri lakini mtu huyo anafariki siku moja kabla ya kuhamia kwenye nyumba yake.

Ni vyema kila mtu kwa imani yake autafute utajiri wa mbinguni ambapo unaupata si kwa fedha bali kwa kutenda yale yanayompendeza muumba na sio utajiri wa hapa duniani kwani hivi vyote tutaviacha hapa hapa.

Nawasilisha

Mkuu itabidi uruhusu watu wacopy na kupaste sehemu mbalimbali ili huu ujumbe uwafikie watu wengi zaidi.
 
Kila mtu kwa nafasi yake anausaka utajiri kwa nguvu zake zote na kwa akili yake.Kkila mtu akilini mwake anaamini fedha na mali ndio kila kitu katika maisha yake.Wengi wanaamini kuwa huzuni walizo nazo, mateso waliyo nayo , na mahangaiko waliyo nayo duniani hapa duniani yataondoshwa na fedha.

Kila mmoja hutumia kila mbinu haijalishi ziwe za halali au ziwe za haramu kujipatia fedha na kujilimbikizia fedha.

Kuna watu wameshaitoa sadaka miili yao kwa ajili ya fedha au utajiri.

Wengine mpaka huwa wanawatoa kafara ndugu zao au hata wazazi wao kwa ajili ya mali na fedha.

Lakini cha kushangaza hao wote wanaotafuta fedha na mali wanajikuta bado hawana furaha maishani mwao hata baada ya kupata hizo fedha na mali.

Bado hawana amani ndani ya nafsi zao.

Walikuwa hawajui kuwa utajiri wa mtu na umasikini wa mtu unaanzia moyoni mwake.

Hapa namaanisha kuwa siri ya kwanza ya utajiri ni ridhiko la nafsi yako.

unatakiwa ujifunze kuridhika na kile ambacho unakipata hata kama ni kidogo kwani kwa kawaida mwanadamu hajawahi kuridhika na hatawahi kuridhika mpaka mwisho wa dunia.

Unatakiwa uijaze nafsi yako utajiri ili upate furaha ya kweli maishani mwako.

Kwa kukosa ridhiko la nafsi na roho watu wengi hutumia kipindi chote cha maisha yao kuhangaikia mali ambapo hawapati hata muda wa kufurahia kile kidogo walichovuna kwani kwenye maisha yao wanaamini bado hakiwatoshi.

Si ajabu kusikia mtu ana miezi sita hajakutana na familia yake kwa sababu yupo mbali akizisaka fedha na mali.

Watu wa aina hiyo wao huwa wanaamini kuwa bado wana kipindi kirefu cha kuishi hapa duniani kwa hiyo wanatakiwa wawe na mali nyingi ili waweze kuishi miaka mingi ya amani na furaha hapa duniani.

Siri ya pili ni kumjua MUNGU na sababu ya uwepo wako hapa duniani.

Unatakiwa ujue kuwa hapa duniani mwanadamu ni kama msafiri aliyepumzika chini ya kivuli cha mtu..nikiwa na maana bado safari yake inaendelea na ni lazima iendelee kwani hapa duniani sio makazi yake ya milele bali ni mpitaji tu.

Ndio maana watu kwa kunogewa na ulimwengu hushikwa na bumbuwazi wakisikia mtu amejenga nyumba yake nzuri lakini mtu huyo anafariki siku moja kabla ya kuhamia kwenye nyumba yake.

Ni vyema kila mtu kwa imani yake autafute utajiri wa mbinguni ambapo unaupata si kwa fedha bali kwa kutenda yale yanayompendeza muumba na sio utajiri wa hapa duniani kwani hivi vyote tutaviacha hapa hapa.

Nawasilisha
Samahani kidogo ndugu huu ujumbe unaweza kumfikishia Lowasa,Chenge,Kinana na wengine wa chama chao!!?Wanafkiri wao wataishi milele hapa kivulini hebu fanya bidii waupate na wajue hata hila zao wanafanyia kivulini na safari inaendelea.
 
Samahani kidogo ndugu huu ujumbe unaweza kumfikishia Lowasa,Chenge,Kinana na wengine wa chama chao!!?Wanafkiri wao wataishi milele hapa kivulini hebu fanya bidii waupate na wajue hata hila zao wanafanyia kivulini na safari inaendelea.
tena na zile pesa zetu za escrow wazirudishe mapema kwa sababu zitaenda kuwawashia moto muda ukifika
 
Baraka ni vile mambo yako yanavyokunyookea na mipango yako kukamilika na bila kusahau kujawa na amani ya nafsi......dhambi adhabu zitatolewa siku ya hukumu kwa sisi tunaoamini...........

Mbona kuna watu ni watenda dhambi na hawamjui mungu na wanamtukana huyo mungu hadharani lakini wana izo Baraka na mafanikio na wamejawa amani ya kutosha..

Na kuna watu wanampenda mungu wanamtumikia kila jambo lakini wao ndio hawana izo Baraka ni tabu na matatizo....go to any evangelical church you can find a lot of people in dimbwi la matatizo mbalimbali.....
 
Utapatwa na matatizo ndugu, hizo ni kudra kwa siku hizi tunaita mitihani, na ukiziami kudra basi ukubali za kheri na za shari. Yaani uwe tayari kupokea raha na shida, uzima na maradhi, utajiri na ufakiri, kupata watt na kufiwa na wtt, nk

Wat I see ni uoga....matatizo yapo yatakuwepo na hayataisha hata uwe huyo mungu unamuomba na kumtaja 24/7....

Kama ulisoma vizuri mtiririko wangu wa post kuna swali linahusiana na hayo uliyoyaainisha..

Mungu yupo sema hameiacha dunia ijiendeshe yenyewe kwa theory of natural selection....

Religion was inverted by a foolish guys..
Islam,Christianity and other fucken religion.
 
Mara nyingi halmashauri ya kichwa cha KikulachoChako huwa nakikubali nayeye mwenyewe anajua hilo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom