Showio
JF-Expert Member
- May 16, 2019
- 255
- 481
Kama ambavyo bahari haiwezi kufilisika maji, maana yenyewe ni maji. Kama ambavyo fukwe haziwezi kufilisika mchanga, maana zenyewe ni mchanga. Kama ambayo noti ya sh 10,000 haiwezi kuishiwa sh 10,000, maana yenyewe ndiyo sh 10,000. NDIVYO AMBAVYO MUNGU HAWEZI KUISHIWA UPENDO, maana YEYE MWENYEWE NI UPENDO. Si tu kwamba anaonyesha upendo. Si tu kwamba anatupa upendo. Si tu kwamba anatupenda. Bali yeye mwenyewe MUNGU ni PENDO. Hafilisiki kupenda, YEYE NI PENDO💪🏾
Showio😳😳 unasemaje?
Nasema hivi, Mungu hawezi kuacha kupenda kwa vile hafilisiki Pendo, yeye mwenyewe ni PENDO ( Waraka wa kwanza wa Yohana 4:8)
Anachukia dhambi, hachukii mtu!
Showio😳😳 Mbona unajichanganya?
Hapana, sijajichanganya. Kama ambavyo wewe unaweza kuchukia uchafu wa nguo lakini hutupi nguo, unaiosha. Kama ambavyo wewe unachukia giza ndani ya chumba lakini haimaanishi unachukia chumba. Ukiwasha taa giza likaondoka chumba kinabaki kizuri. Giza linazuia tu usione uzuri wa chumba si ndivyo?
Mungu hachukii mtu, anachukia dhambi iliyoko ndani ya mtu. Ndiyo maana anasamehe ili aendelee kuwa nawe! Mungu anakupenda. Yohana 3:16
Nikishatafakari hivyo, naona kila gumu limekuwa jepesi. Naamka na nguvu kuyakabili maisha!
Showio😳😳 unasemaje?
Nasema hivi, Mungu hawezi kuacha kupenda kwa vile hafilisiki Pendo, yeye mwenyewe ni PENDO ( Waraka wa kwanza wa Yohana 4:8)
Anachukia dhambi, hachukii mtu!
Showio😳😳 Mbona unajichanganya?
Hapana, sijajichanganya. Kama ambavyo wewe unaweza kuchukia uchafu wa nguo lakini hutupi nguo, unaiosha. Kama ambavyo wewe unachukia giza ndani ya chumba lakini haimaanishi unachukia chumba. Ukiwasha taa giza likaondoka chumba kinabaki kizuri. Giza linazuia tu usione uzuri wa chumba si ndivyo?
Mungu hachukii mtu, anachukia dhambi iliyoko ndani ya mtu. Ndiyo maana anasamehe ili aendelee kuwa nawe! Mungu anakupenda. Yohana 3:16
Nikishatafakari hivyo, naona kila gumu limekuwa jepesi. Naamka na nguvu kuyakabili maisha!