Naanto Mushi
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 6,236
- 15,602
Kuna huu mrengo wa kiuwanaharakati huko twitter ambao kwa siku za karibuni umejidhihirisha kuwa upo sambamba na sehemu muhimu ya chama cha ACT Wazalendo. Mrengo huu kwa siku za karibuni umekuwa ukifanya mashambulizi ya wazi wazi kwa chama cha CHADEMA pasipo haswa kuwa na hoja zenye mashiko zaidi ya matusi kwa viongozi wakubwa wa CHADEMA.
Pamoja na mrengo huu wa kiuanaharakati kuonesha kila mara kuikosoa serikali ya Rais Magufuli ila ajenda yao ya kuishambulia CHADEMA imekuwa fikirishi kwa wajuzi wa mambo kwamba yawezekana Grand Architects wa harakati hizi za Twitter wana nia ya kuiporomosha CHADEMA kutoka chama kikuu cha upinzani ili kuisaidia CCM kuendelea kubaki madarakani.
Wanachoshindwa kuelewa wana harakati hawa uchwara ni kwamba, hawajajua haswa ajenda kuu ya Grand Architects wa harakati hizi. Wamejisahau wanakula na nani, wapo gizani, na matokeo ndo haya tunayaona wanapotezwa taratibu taratibu na dola.
Hili ndo tatizo la kufanya harakati za kupelekwa na upepo kama bendera, pasipo kujua ajenda za anaye kutumikisha ni zipi. Ukweli ndo wanaupata sasa hivi kwamba hizo #harshtag na hao maaskari nyuma ya keyboard hawana msaada wowote.
Heri ya Christmas na Mwaka Mpya
Nipo Kibosho – Moshi
N.Mushi
Pamoja na mrengo huu wa kiuanaharakati kuonesha kila mara kuikosoa serikali ya Rais Magufuli ila ajenda yao ya kuishambulia CHADEMA imekuwa fikirishi kwa wajuzi wa mambo kwamba yawezekana Grand Architects wa harakati hizi za Twitter wana nia ya kuiporomosha CHADEMA kutoka chama kikuu cha upinzani ili kuisaidia CCM kuendelea kubaki madarakani.
Wanachoshindwa kuelewa wana harakati hawa uchwara ni kwamba, hawajajua haswa ajenda kuu ya Grand Architects wa harakati hizi. Wamejisahau wanakula na nani, wapo gizani, na matokeo ndo haya tunayaona wanapotezwa taratibu taratibu na dola.
Hili ndo tatizo la kufanya harakati za kupelekwa na upepo kama bendera, pasipo kujua ajenda za anaye kutumikisha ni zipi. Ukweli ndo wanaupata sasa hivi kwamba hizo #harshtag na hao maaskari nyuma ya keyboard hawana msaada wowote.
Heri ya Christmas na Mwaka Mpya
Nipo Kibosho – Moshi
N.Mushi