Hussein Mwinyi na fursa za Zanzibar katika Muungano

chuwaalbert

JF-Expert Member
Sep 17, 2010
3,598
2,115
Hussein Mwinyi, raia mwenye bahati ya kupata kuwa mbunge kupitia majimbo ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Pemba, alisema Bungeni kuwa kuondolewa kwa “kero” za Muungano ni kwa Zanzibar kuruhusiwa kujiunga na OIC, na kupata fursa SAWA katika ajira za Muungano, ili kupata amani na ustawi wa jamii. Alisema: “Kero ya mgawo wa ajira za Muungano uwekewe utaratibu utakao hakikisha uwepo (kuwepo?) kwa uwiano mzuri wa ajira za Muungano kati ya Zanzibar na Bara(tamka Tanganyika).

My take: Misimamo hii ya Wazanzibari ya “SIKAKI NATAKA” ndo inakwamisha kuimarika kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Tanganyika itoke katika mbeleko ya Tanzania na ije nje, wazi ili kila Nchi iwe na Hazina yake yenyewe na mambo madogo kama ya usawa wa ajira yatajitatua kwa kuangalia uwiano wa mchango wa kila Nchi katika Mfuko wa pamoja.
 
Huwa sifahamu kwa hawa viongozi, kwani muungano huu upo kwa ajili ya kugaiyana vyeo?
Hili ndilo linalotuathiri sisi Waznz, akipewa cheo basi hata kama alikua ana uchungu kiasi gani anabadilika na kama tunavowajua CCM ni wepesi sana kwa hilo.
 
Kwa znz fursa za ki uchumi katika serikali ya muungano, ni wao ku agizia bidhaa kwa ushuru mdogo na kuziuza bara bila kutozwa kodi kati ya kodi yao i.e rate na rate ya kodi ya bara, kwa maana nyingine ni kwamba wabara watoe kodi yao na kuwapa wa znz kuendesha serikali yao, na fursa ya ajira kwao ni 50% kwa 50% badala ya uwiano wa idadi ya watu na contribution kwenye serikali yamuungano
 
Back
Top Bottom