mwathu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2012
- 403
- 210
Ndoa ni ya mke na mume, wazazi wa pande zote nao wana matatizo yao na wanayamaliza kimya kimya sasa wewe jibebeshe yako uwapelekee utaishia kupata majibu negative tuu na ambayo hayana maslahi na ndoa yenu. Kwa wanandoa kila mmoja anapaswa awe mtetezi wa mpenzi wake kwa wazazi wako. kiasili mzazi huwa anampenda na kumsikiliza zaidi mtoto wake kuliko mtoto wa mtu mwengine hivyo ukiongea mazuri ya mpenzio kwa wazazi wako unaongeza maisha ya ndoa yenu na baraka zaidi. hakuna perfect ndoa duniani hata wasuluhishi nao huwa wanatamani wapate mtu wa kusuluhisha yao.
Ni sahihi kwa wanandoa kila mnaloongea kufikisha ukweni? yaani namaanisha mwanamke afikishe kwao na mume afikishe kwao, haijalisha hayo mtakayoyaongea mazuri, mabaya, yanawahusu hayawahusu, naomba maoni yenu athari ya hii kitu mbeleni na kama vema kufikisha ukweni pia nijuzeni rafiki zangu