Husband and Wife

Husband and Wife

laussane

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2009
Posts
255
Reaction score
132
Ni sahihi kwa wanandoa kila mnaloongea kufikisha ukweni? yaani namaanisha mwanamke afikishe kwao na mume afikishe kwao, haijalisha hayo mtakayoyaongea mazuri, mabaya, yanawahusu hayawahusu, naomba maoni yenu athari ya hii kitu mbeleni na kama vema kufikisha ukweni pia nijuzeni rafiki zangu
 
aisee...........
kwanza mtoa mada umeoa/olewa??
ukinijibu nitakupa jibu
 
Ni sahihi kwa wanandoa kila mnaloongea kufikisha ukweni? yaani namaanisha mwanamke afikishe kwao na mume afikishe kwao, haijalisha hayo mtakayoyaongea mazuri, mabaya, yanawahusu hayawahusu, naomba maoni yenu athari ya hii kitu mbeleni na kama vema kufikisha ukweni pia nijuzeni rafiki zangu

Kama wewe umeoa/umeolewa huwa unafanyaga vip? Tufahamishane kwanza!!
 
Mambo ya wanandoa inabidi yaishie ndani; na ukiona mwenzako anayatoa nje ujue kuna mapungufu - huenda yanakuwa yamemzidi au yeye hajui kujisimamia.
 
Nimeolewa my gfsonwin, tililika mama labda utatusaidia
 
Kama wewe umeoa/umeolewa huwa unafanyaga vip? Tufahamishane kwanza!!

Mimi nimeolewa na huwa sipeleki kwetu, sasa naona kama kuna uhalali wa kupeleka kutokana na situation ninayoipitia nilitaka kufaham na kutoka kwenu, ni vema kupeleka? ata kwa upande wangu sijazoea na sipendi kupeleka nifahamishe zaidi
 
ni mambo ya wanandoa tu lakini pia inategemeana na jambo lenyewe....
 
Mimi nimeolewa na huwa sipeleki kwetu, sasa naona kama kuna uhalali wa kupeleka kutokana na situation ninayoipitia nilitaka kufaham na kutoka kwenu, ni vema kupeleka? ata kwa upande wangu sijazoea na sipendi kupeleka nifahamishe zaidi
Bi.Laussane "sharing is caring" unaweza igawa nusu-nusu 50~50% yapo yakupeleka yapo yakumezea.... na maisha ni Saa hivi na Saa vile !!
Blessings..
 
He he he, kuna siku watati.ana kimgongo mgongo waende kusimulia kwa wakwe.

Lazima wajifunze kuchuja ya kusema.
 
Jambo labda liwe zito sana liwatatize katika kuamua ndo mwaweza kulitoa nje ya nyumba tena kwa namna ya busara na hekima.
 
Mimi nimeolewa na huwa sipeleki kwetu, sasa naona kama kuna uhalali wa kupeleka kutokana na situation ninayoipitia nilitaka kufaham na kutoka kwenu, ni vema kupeleka? ata kwa upande wangu sijazoea na sipendi kupeleka nifahamishe zaidi


inategemea na situation yenyewe, na huko kwenu unapeleka kivipi, unapeleka kimshitaka|? au kutaka ushauri..

wakati mwingine kama una mzazi mfn mama msiri waweza kumwambia akupe ushauri, lkn asimwambie baba na watu wengine..yaani aweke moyoni..kama unaelewana na mama yako mbona huyo ndo rafiki yako wa kwanza..ila pia uangalie na ishu yenyewe maana unaweza kumwambia mama yako kitu akaumia kuliko hata wewe mwenye tatizo mwishowe mkaanza kuuguza presha na kisukari..

mimi binafsi sina wazazi wote walishafariki, nina ndugu lkn huwa siwashirikishi matatizo ya home kwangu, lkn napata tabu sana kwani wakati mwingine huwa natamani mama yangu angekuwa hai, nimueleze kitu fulani anishauri au anipe moyo....basi naishiaga tu kuliaa na kubaki na matatizo yangu moyoni...kuna wakati hasa kwa msichana, binti aliyeolewa atahitaji ushauri wa mama..
huu ni kwa mtizamo wangu lkn
 
Inategemea na jambo lenyewe, mfano huwezi kupeleka ukweni habari za nyie kutaka kulipia bili za umeme.
Lakini mfano mume mlevi kupindukia anarudi usiku kila ukimweleza haelewi umetumia marafiki hasikii sio mbaya ukipata msaada huko.

lakini angalia na jambo lenyewe na busara za hao wakwe na je huyo mume anawaheshimu?
 
inategemea na situation yenyewe, na huko kwenu unapeleka kivipi, unapeleka kimshitaka|? au kutaka ushauri..

wakati mwingine kama una mzazi mfn mama msiri waweza kumwambia akupe ushauri, lkn asimwambie baba na watu wengine..yaani aweke moyoni..kama unaelewana na mama yako mbona huyo ndo rafiki yako wa kwanza..ila pia uangalie na ishu yenyewe maana unaweza kumwambia mama yako kitu akaumia kuliko hata wewe mwenye tatizo mwishowe mkaanza kuuguza presha na kisukari..

mimi binafsi sina wazazi wote walishafariki, nina ndugu lkn huwa siwashirikishi matatizo ya home kwangu, lkn napata tabu sana kwani wakati mwingine huwa natamani mama yangu angekuwa hai, nimueleze kitu fulani anishauri au anipe moyo....basi naishiaga tu kuliaa na kubaki na matatizo yangu moyoni...kuna wakati hasa kwa msichana, binti aliyeolewa atahitaji ushauri wa mama..
huu ni kwa mtizamo wangu lkn

Thanks mamy na pole sana,
 
Inategemea na jambo lenyewe, mfano huwezi kupeleka ukweni habari za nyie kutaka kulipia bili za umeme.
Lakini mfano mume mlevi kupindukia anarudi usiku kila ukimweleza haelewi umetumia marafiki hasikii sio mbaya ukipata msaada huko.

lakini angalia na jambo lenyewe na busara za hao wakwe na je huyo mume anawaheshimu?


Kijana asante kwa ushauri na umenifurahisha pia, well said lakini, hii ninayoulizia naona kama imepita mpaka yaani lolote tunalodiscuss lazima lifike pande zileee
 
kushirikisha wazazi ni vyema lakini jambo la kimaendeleo au lakutofautiana baina ya wanandoa, haya ni kwa yale mambo makubwa lakini si kunyimana unyumba siku moja huyo, au jamaa kachelewa kurudi huyo....!
Lakini haya yanategemea.......
 
ukioa wewe ndo Baba na wewe ndo mwanzo na mwisho wa yote,yawe mabaya au mazuri,kupeleka mambo yenu kwa wazazi wenu ni utoto na upumbavu,
Ref.mushi vs ufoo %#http://
 
Back
Top Bottom