Humphrey Polepole avamiwa na majambazi

Humphrey Polepole avamiwa na majambazi

bato

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
3,960
Reaction score
3,474
Aliyekuwa mjumbe wa Tume Maalum ya Katiba (maarufu-Tume ya Warioba) na mchambuzi wa siasa, Humphrey Polepole, usiku wa kuamkia jana alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake,Mbezi Beach, Dar.

Polisi walifika haraka eneo la tukio. Hakuna madhara yaliyoripotiwa, pia hakuna aliyekamatwa kuhusishwa na tukio hilo.

Polepole.jpg
CHANZO: Raia Tanzania
 
Wanajuwa ccm wameshamvutia mkwanja ndo wanautafuta!
 
wanataka kuvuruga hali ya hewa ya ufunguzi wa kampeni ya ukawa wana mambo hawa. tutashuhudia mengi sana kati ya j3-ijumaa visa na mikasa. mara ohh kipindupindu kimezidi kusambaa mara masha mara polepole mara kesho hatujui litaibuka lipi wana mambo hawa. kudeal nao na wewe unahitaji kuwa na mambo mengi na akili ya mbele ya kufikiri zaidi yao .
 
Maigizo matupu eti Polisi Wamewahi, Kwani Polisi Wanalinda Nyumba yake. Mbona Polisi hao hao Wanashindwa kufika haraka Vituo

vyao Vinapovamiwa Leo imetokea Miujiza gani hadi kufika Haraka kwa HP. Kama Siku Hizi Huyu HP Analindwa Na Polisi Hapo Maswali

yatapungua Lakini Kama Sio basi Huu Utakuwa Ni Usanii mtupu, Kama Kuwatumia Wasanii Wakati Wa Kampain za Kisaii. Fanyeni

Campaign hacheni kutengeneza Matukio. Watu Wengi Wameuawa Na Majambazi Including Dr. Mvungi, Hakuna lolote Leo Hii Sinema

Hizi Hazieweki Baodo. Watanzania wa Leo Wanajua Kuconnect Dot Moja Na Nyingine.
 
ccm wameshaanza kututengenezea matukio.

Umeniwahi kwani nilitaka kusema exactly ulichoandika. Kama polisi walifika on time basi Huo ni mchoro. Hii ni Kama ile sinema ya amboni. Wanaofanya haya matukio hata hawajui namna ya kufanya story angalau iwe na lafudhi ya ukweli. Mfano hii ya Leo wangemkata mguu pole pole kwa pole pole hadi Hapo polisi watakapofika. Sijui kwa nini mkapa haoni hawa ni wapumbavu😇
 
BWN POLEPOLE amekuwa mwiba kwa LOWASA na mgombea wa ukawa. jana amevamiwa nybani kwake ambapo baada ya kuanza kumshambulia mgombeawa ukawa amekuwa akipata vitisho.
polisi wanaendelea na uchunguzi.
 
Vuvuzela wa ccm huyo, ni mbinu hakuna cha majambazi. Ana maana alikuwa anajadiliana nao wakaondoka kistaarabu? Hao polisi walikuwa upenuni wakimlinda yeye? Mbinu zingine za kilofa sana kutafuta umaarufu. Mandela alishaangaliza kwamba ukitaka kuwa maarufu uwe tayari kwa machungu. Asiweweseke ili apatiwe ulinzi. Kama anataka ving'oling'oli aanze siasa za kwenda yeye mwenyewe ikulu. Labda waume za kina mama anaoambiwa anawachakachua kazini kwake? Maana aliambiwa na msigwa kwamba hajawa mwadilifu na hakujibu mpaka leo. Labda kapora mali za watu wanamlazimisha awarudishie anawageuzia kibao. Simwamini tena dogo polepole amejiharibia heshima yake tangu alipokubali kutumiwa kama toilet paper
 
jamani mbona ni kituko cha mwaka eti polisi walifika haraka na akuna majeraha wala kilichoibiwa wala akuna aliye kamatwa du kichekesho kwa sababu kwanza polisi awana rekodi ya kuwai au kusaidia kwenye matukio akunaga iyo masta pili tutaaminije kwamba ni wezi ndio walikuja?
 
Ningeshangaa sana kama uvamizi huo usingehusishwa moja kwa moja na UKAWA. Ukiona hivyo ujue CCM iko nyuma ya tukio hilo. Washindwe na kulegea.
 
Acha polisi ifanye kazi yake mtu avamiwe na majambazi mseme ukawa
 
yani ccm wanataka kusema kuwa polepole kawasema ukawa na lowasa sasa wamemvamia. hawa ccm hawa ni wakuwatoa kabisa na hii habari ni ya kupotezea kama watanzania walivyompotezea lipumba baada ya kuona analeta gozigozi sasa hivi spidi 120 tu hadi kieleweke
 
Sipati pacha slow slow akifikisha miaka 45! Kwanza taarifa imetolewa na yeye mwenyewe kwa kupiga cm kwa mwsndishi wa gazeti lililonunuliwa na ccm la raia Tanzania. Ni usanii tu hakuna jambazi wala nin.
 
Back
Top Bottom