Hujuma zingine Wagombea wa CHADEMA Simiyu

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Wagombea udiwani wa CHADEMA katika Kata ya Tindabuligi, Ndugu Zunzu Ndatulu Humu na Kata ya Kisesa, Ndugu Shanemhanga Mabula Makonge , Wilaya ya Meatu, mkoani Simiyu, wamenyimwa fomu za kukata rufaa baada ya kuenguliwa kwenye uchaguzi jana usiku.

Jitihada za wagombea hao na viongozi wa Chama kupata fomu hizo na. 12(c) kwa Msimamizi wa Uchaguzi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Ndugu Manoza, hadi sasa hazijafanikiwa baada ya Msimamizi huyo kutoonekana ofisini tangu asubuhi tofauti na alivyokuwa amewaahidi na kuwataka wafike kwake wachukue fomu hizo. Hata simu zake ambazo alikuwa anapokea hadi jana usiku, hazipatikani.

Wagombea hao walirejesha fomu zao za kugombea kwa Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi katika kata hizo Jumatatu, 20 Agosti, mwaka huu. Hadi majira ya jioni jana Jumanne Mgombea wa Kata ya Tindabuligi alikuwa hajawekewa pingamizi lakini ghafla saa 1.30 usiku kuwa akataarifiwa kuwa amewekewa pingamizi na akapewa barua ya kuenguliwa kwenye uchaguzi.

Taarifa za awali zimesema kuwa mgombea huyo pamoja na viongozi wa chama walipohoji kuenguliwa bila haki ya kujibu mapingamizi yaliyowekwa, waliambiwa hakuna fursa hiyo. Taarifa hizo zimedai kuwa kitendo hicho kilifanyika mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi (Mkurugenzi) pamoja na maofisa wakuu wa vyombo vya dola ngazi ya wilaya waliokuwepo ofisini kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi.

Kwa upande wa Kata ya Kisesa, mapingamizi yaliyowekwa saa nne asubuhi jana, yalijibiwa na mgombea na kurejeshwa kwa wakati jana hiyo hiyo, lakini ilipofika majira ya 2.30 usiku naye akataarifiwa kuwa ameenguliwa kwenye uchaguzi.

Jitihada za wagombea wote kuwataka Wasimamizi Wasaidizi wawapatie fomu na. 12(c) kwa ajili ya kukata rufaa zilishindikana kwa kile kilichodaiwa kuwa fomu hizo hazipo bali zinapatikana kwa Msimamizi wa Uchaguzi watazipata.

Walipowasiliana na Msimamizi wa Uchaguzi jana usiku, aliwataka wafike ofisini kwake Jumatano, Agosti 22, mwaka huu (leo) asubuhi ili awapatie hizo fomu waweze kukata rufaa. Hadi jioni hii hajaonekana ofisini wala hapatikani.

Kata ya Mwanhuzi, Simiyu

Katika Kata ya Mwanhuzi ambayo nayo inatarajia kufanya uchaguzi wa marudio, Msimamizi Msaidizi alikataa kuzipokea fomu za Mgombea wa CHADEMA, baada ya kuzipitia na kuzihakiki, akisema kuwa zipelekwe siku ya Alhamis, Agosti 23 ambayo ndiyo siku ya mwisho ya kurejesha fomu na kufanya uteuzi wa wagombea katika kata hiyo.

Makene
 
Hii ndo hasara ya kuteua wanachama kindakindaki wa CCM kuwa wakurugenzi, maDC na maRC. Huu upuuzi wa NEC kutumia watu hawa kama "wasimamizi wa uchaguzi" ipo siku utakuja kuleta maafa na machafuko makubwa nchini. Something needs to be done urgently. Come 2020 kuna watu watachomwa moto mchana kweupe kama huu uzwazwa utaendelezwa
 
Mijitu mizima inashenzika kwenda mbele. Yaani ni wagombea wa upinzani peke yao wanaofanya makosa kila uchaguzi. Kumbukeni JPM aliwachagua walio utaka ubunge wengi na kushindwa kuwa ma DED. Hawa mtawafahamu vizuri 2020 watakapojaribu tena na hawataki waonekane kua upande usiofaa. Inasikitisha lakini ndiyo Tanzania yetu.
 
s
Wagombea udiwani wa CHADEMA katika Kata ya Tindabuligi, Ndugu Zunzu Ndatulu Humu na Kata ya Kisesa, Ndugu Shanemhanga Mabula Makonge , Wilaya ya Meatu, mkoani Simiyu, wamenyimwa fomu za kukata rufaa baada ya kuenguliwa kwenye uchaguzi jana usiku.

Jitihada za wagombea hao na viongozi wa Chama kupata fomu hizo na. 12(c) kwa Msimamizi wa Uchaguzi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Ndugu Manoza, hadi sasa hazijafanikiwa baada ya Msimamizi huyo kutoonekana ofisini tangu asubuhi tofauti na alivyokuwa amewaahidi na kuwataka wafike kwake wachukue fomu hizo. Hata simu zake ambazo alikuwa anapokea hadi jana usiku, hazipatikani.

Wagombea hao walirejesha fomu zao za kugombea kwa Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi katika kata hizo Jumatatu, 20 Agosti, mwaka huu. Hadi majira ya jioni jana Jumanne Mgombea wa Kata ya Tindabuligi alikuwa hajawekewa pingamizi lakini ghafla saa 1.30 usiku kuwa akataarifiwa kuwa amewekewa pingamizi na akapewa barua ya kuenguliwa kwenye uchaguzi.

Taarifa za awali zimesema kuwa mgombea huyo pamoja na viongozi wa chama walipohoji kuenguliwa bila haki ya kujibu mapingamizi yaliyowekwa, waliambiwa hakuna fursa hiyo. Taarifa hizo zimedai kuwa kitendo hicho kilifanyika mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi (Mkurugenzi) pamoja na maofisa wakuu wa vyombo vya dola ngazi ya wilaya waliokuwepo ofisini kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi.

Kwa upande wa Kata ya Kisesa, mapingamizi yaliyowekwa saa nne asubuhi jana, yalijibiwa na mgombea na kurejeshwa kwa wakati jana hiyo hiyo, lakini ilipofika majira ya 2.30 usiku naye akataarifiwa kuwa ameenguliwa kwenye uchaguzi.

Jitihada za wagombea wote kuwataka Wasimamizi Wasaidizi wawapatie fomu na. 12(c) kwa ajili ya kukata rufaa zilishindikana kwa kile kilichodaiwa kuwa fomu hizo hazipo bali zinapatikana kwa Msimamizi wa Uchaguzi watazipata.

Walipowasiliana na Msimamizi wa Uchaguzi jana usiku, aliwataka wafike ofisini kwake Jumatano, Agosti 22, mwaka huu (leo) asubuhi ili awapatie hizo fomu waweze kukata rufaa. Hadi jioni hii hajaonekana ofisini wala hapatikani.

Kata ya Mwanhuzi, Simiyu

Katika Kata ya Mwanhuzi ambayo nayo inatarajia kufanya uchaguzi wa marudio, Msimamizi Msaidizi alikataa kuzipokea fomu za Mgombea wa CHADEMA, baada ya kuzipitia na kuzihakiki, akisema kuwa zipelekwe siku ya Alhamis, Agosti 23 ambayo ndiyo siku ya mwisho ya kurejesha fomu na kufanya uteuzi wa wagombea katika kata hiyo.

Makene
ijui hapa wale CCM kindakindaki wanasimamia wapi? juzi tu kuna waliokatwa kwamba siyo watanzania, mara korogwe, nazani buyungu kimewafunza kitu, wenye akili watapita na kujifanya hawayaoni ila mazwazwa ya kutumiwa yataendelea bila ya aibu kuytetea hili,
2020 huu mchezo utaonekana wa kawaida, lakini utatugharimu sana
 
Kibiti kwa nini yalikuwa yanatokea yale? Na jee yakitokea pande zote za nchi tutaweza kuyadhibiti?
Au tutasema kazi ya Mungu haina makosa?
Haya, walio ambiwa wasiwe neutral waendelee ila kuna siku watoto wao watawasababisha wakae matanga

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha waendelee kyfukia mbegu ardhini kwa lengo la kuziua bila kujua kuwa hiyo ndiyo tunaota kupanda mbegu za chuki na ni process ya kuzipa uhai zaidi.
Tutakuja kuulizana tulipomosea wakati sasa hivi wanatumia nguvu na pesa kufanya hayo makosa. Hawajui umbali wa mizizi yake unapokwenda
 
Wanasiasa na siasa zao, Wenye nchi na nchi yao, Wazalendo na taifa letu.
Fumbua fumbo hili.
 
Hivi haiwezekani kutumia hata pinde na mishale tu?! Hawa watu ni wachache sana kuendeleza huu uovu.
 
Eti chama cha mapinduzi yani sijawahi kuona chama oga na lakipuuzi kama hili! Aisee mambo haya naamini 2020 tutarajie misiba mingi ya visasi! Choko choko hizi zina mwisho...
 
Walipowasiliana na Msimamizi wa Uchaguzi jana usiku, aliwataka wafike ofisini kwake Jumatano, Agosti 22, mwaka huu (leo) asubuhi ili awapatie hizo fomu waweze kukata rufaa. Hadi jioni hii hajaonekana ofisini wala hapatikani.
Leo ni sikukuu yakhe
Tueleweshe wameenguliwa kwa mapingamizi ya sababu zipi?
Naona umekwepa kueleza mapingamizi ni ya nini,chadema kuna udhaifu wa kuteua wagonbea na ujazaji fomu
mwaka 2010,chadema waliwahi kuteua jambazi liliowahi kufungwa miaka 30 likaachiwa kwa msamaha
 
Tukiwa majukwaani tunasifika kwa kuhubiri mshikamano lkn maisha halisi nje ya jukwaa yamejaa fitina na hayajengi taifa lente umoja bali utengano.
 
Leo ni sikukuu yakhe
Tueleweshe wameenguliwa kwa mapingamizi ya sababu zipi?
Naona umekwepa kueleza mapingamizi ni ya nini,chadema kuna udhaifu wa kuteua wagonbea na ujazaji fomu
mwaka 2010,chadema waliwahi kuteua jambazi liliowahi kufungwa miaka 30 likaachiwa kwa msamaha
huna akili wewe kutwa kubwabwja unadhani wananchi tutaendelea kukulipia fedha ukakamuliwe megu ili utuletee mazezeta ishia huko acha ujinga wewe marehemu wa kisiasa kwanza hata miguu ya kukimbilia huna ikitokea wananchi wanalianzisha kujaza makalio tu
 
Back
Top Bottom