Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
Wakongo waandamana Dar
na Mwandishi wetu
WAFANYABIASHARA na waagizaji wa magari kutoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wameandamana wakiilalamikia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuwazuia kutoa magari yao bandarini bila kuwapa sababu za msingi.
Tukio hilo lilitokea mjini Dar es Salaam jana, ambapo wafanyabiashara na waagizaji hao walilazimika kuandamana kutoka bandarini hadi kwenye ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kumtafuta Kamishna wa TRA, ambaye alikuwepo hapo kwa ajili ya kuhudhuria mkutano.
Wakizungumza na waandishi wa habari, Wakongo hao walisema magari yao yamezuiliwa kwa kipindi cha muda mrefu na ilidaiwa magari hayo yana mfumo wa usukani wa upande wa kushoto badala ya upande wa kulia, kitu walichosema eti ndio sababu ya kutopewa na kusema si sababu ya msingi kwao.
Sababu iliyotolewa si ya msingi kutokana na nchi yetu kutojali mfumo wowote wa usukani wa gari. Sisi tunataka Mamlaka ya Mapato waruhusu tuchukue magari yetu hata kama yana matatizo yatajulikana huko nchini kwetu Kongo, wala si hapa Tanzania, alisema mmoja wa Wakongo ambaye hakutaka jina lake litajwe.
na Mwandishi wetu
WAFANYABIASHARA na waagizaji wa magari kutoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wameandamana wakiilalamikia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuwazuia kutoa magari yao bandarini bila kuwapa sababu za msingi.
Tukio hilo lilitokea mjini Dar es Salaam jana, ambapo wafanyabiashara na waagizaji hao walilazimika kuandamana kutoka bandarini hadi kwenye ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kumtafuta Kamishna wa TRA, ambaye alikuwepo hapo kwa ajili ya kuhudhuria mkutano.
Wakizungumza na waandishi wa habari, Wakongo hao walisema magari yao yamezuiliwa kwa kipindi cha muda mrefu na ilidaiwa magari hayo yana mfumo wa usukani wa upande wa kushoto badala ya upande wa kulia, kitu walichosema eti ndio sababu ya kutopewa na kusema si sababu ya msingi kwao.
Sababu iliyotolewa si ya msingi kutokana na nchi yetu kutojali mfumo wowote wa usukani wa gari. Sisi tunataka Mamlaka ya Mapato waruhusu tuchukue magari yetu hata kama yana matatizo yatajulikana huko nchini kwetu Kongo, wala si hapa Tanzania, alisema mmoja wa Wakongo ambaye hakutaka jina lake litajwe.