MFIZIGO
JF-Expert Member
- Sep 30, 2014
- 374
- 232
Wanajamvi Salam,
Zikiwa zimebaki siku kumi na nne (14) tu kwenda kushuhudia historia ikiandikwa Tanzania, kwa ama wananchi kuendelea kuchagua ccm ambayo kiukweli imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili watanzania walio wengi au wananchi kwenda kuchagua Uhuru Haki na Maendeleo yao kwa kufanya mabadiliko ya uongozi hasa katika nafasi nyeti ya uraisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Kampeni za vyama vyote shindani zinaendelea na huku wadadisi na wachambuzi wa kisiasa wakipima upepo wa kisiasa hasa kwa kuangalia Sera za vyama vyote na idadi ya watu wanaohudhuria katika mikutano ya kampeni kwa vyama tofauti. Hali imekuwa si shwari kwa chama tawala, imekuwa kana kwamba wanapumulia mashine. Kampeni zao zimekuwa zikiratibiwa kwa kiasi kikubwa nje ya chama, hapa nikimaanisha kwa kutumia vyombo vya Dora pamoja na wasanii. Huku upande wa chama kikuu Cha upinzani CHADEMA Mambo ni bul bul. Hali hii imekuja baada ya ccm kukosea hapa
1. Wamefanya siasa kwa miaka mitano peke yao, hivyo ni Kama vile wananchi wamewachoka, wananchi wanataka kusikia mawazo mapya. Wanataka kusikia kile ambacho walikuwa wanafichwa kuambiwa kwa miaka mitano huku ccm wakisema peke yao. Ndiyo maana unaona kwenye mikutano ya chama kikuu Cha upinzani wananchi wanajazana pasi na aina yoyote ya ushawishi wa wasanii. Kwenye hili ccm imewakinaisha wananchi hivyo wanataka mawazo mapya.
2. Kizazi kilichokuwa ccm kufa na kuzikana kinazidi kuisha. Wale wazee waliokuwa 60+ mwaka 2015 wakati Magufuli anaingia madarakani wamezidi kuisha, hivyo kuja damu mpya ambayo bado haioni hayo maendeleo ambayo ccm wanajivuna kuwaletea wananchi zaidi ya maumivu makali kila uchwao.
3. Ccm wanecheza karata mbaya kwa Bernard Kamiliud Membe. Najua hii ndiyo ilikuwa kete pekee ya ccm kwenye uchaguzi huu. Maandalizi makubwa waliyafanya hapa kwa kumuweka Membe kuwa Kama kibaraka kwa wapinzani, lakini CHADEMA waliliona hilo wakaruka kihunzi hicho. Rejea maneno ya Membe baada ya kikao maalumu Cha kuhojiwa na kamati ya nidhamu ya chama. " Tumeongea Mambo mazuri kwa mustakabari wa taifa letu na chama chetu." Lakini pia wanaccm waliokuwa wakimshinikiza Membe kwenda upinzani walikuwa ni wengi kuliko upinzani wenyewe. Hii maana yake walijipanga kwenye hili.
4. Magufuli amechagua timu mbovu ya kampeni ambayo haina uzoefu na masuala haya ya pilika pilika. Watu wengi ikiwemo Mimi, tulitarajia kwenye timu ya kampeni ya ccm mwaka huu wangeweka full mkoko. Pale Kuna Nape, Makamba, Mzee Mangula pamoja na viongozi wengine wabobezi ndanibya chama. Lakini uwepo wa watu Kama Polepole na Bashiru kumefanya timu ya kampeni kupwaya sana ndani ya CCM. Angalia hata upangaji wa ratiba tu unawacost.
Sioni wapi CCM watashinda iwapo uchaguzi huu utafanywa kwa kufuata misingi ya Sheria ambazo wao wenyewe ndiyo wameziweka. Iwapo tume watakuwa tayari kumtangaza hata wasiyempenda, sioni CCM watashinda vipi.
Asalam Alleykum
Zikiwa zimebaki siku kumi na nne (14) tu kwenda kushuhudia historia ikiandikwa Tanzania, kwa ama wananchi kuendelea kuchagua ccm ambayo kiukweli imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili watanzania walio wengi au wananchi kwenda kuchagua Uhuru Haki na Maendeleo yao kwa kufanya mabadiliko ya uongozi hasa katika nafasi nyeti ya uraisi wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Kampeni za vyama vyote shindani zinaendelea na huku wadadisi na wachambuzi wa kisiasa wakipima upepo wa kisiasa hasa kwa kuangalia Sera za vyama vyote na idadi ya watu wanaohudhuria katika mikutano ya kampeni kwa vyama tofauti. Hali imekuwa si shwari kwa chama tawala, imekuwa kana kwamba wanapumulia mashine. Kampeni zao zimekuwa zikiratibiwa kwa kiasi kikubwa nje ya chama, hapa nikimaanisha kwa kutumia vyombo vya Dora pamoja na wasanii. Huku upande wa chama kikuu Cha upinzani CHADEMA Mambo ni bul bul. Hali hii imekuja baada ya ccm kukosea hapa
1. Wamefanya siasa kwa miaka mitano peke yao, hivyo ni Kama vile wananchi wamewachoka, wananchi wanataka kusikia mawazo mapya. Wanataka kusikia kile ambacho walikuwa wanafichwa kuambiwa kwa miaka mitano huku ccm wakisema peke yao. Ndiyo maana unaona kwenye mikutano ya chama kikuu Cha upinzani wananchi wanajazana pasi na aina yoyote ya ushawishi wa wasanii. Kwenye hili ccm imewakinaisha wananchi hivyo wanataka mawazo mapya.
2. Kizazi kilichokuwa ccm kufa na kuzikana kinazidi kuisha. Wale wazee waliokuwa 60+ mwaka 2015 wakati Magufuli anaingia madarakani wamezidi kuisha, hivyo kuja damu mpya ambayo bado haioni hayo maendeleo ambayo ccm wanajivuna kuwaletea wananchi zaidi ya maumivu makali kila uchwao.
3. Ccm wanecheza karata mbaya kwa Bernard Kamiliud Membe. Najua hii ndiyo ilikuwa kete pekee ya ccm kwenye uchaguzi huu. Maandalizi makubwa waliyafanya hapa kwa kumuweka Membe kuwa Kama kibaraka kwa wapinzani, lakini CHADEMA waliliona hilo wakaruka kihunzi hicho. Rejea maneno ya Membe baada ya kikao maalumu Cha kuhojiwa na kamati ya nidhamu ya chama. " Tumeongea Mambo mazuri kwa mustakabari wa taifa letu na chama chetu." Lakini pia wanaccm waliokuwa wakimshinikiza Membe kwenda upinzani walikuwa ni wengi kuliko upinzani wenyewe. Hii maana yake walijipanga kwenye hili.
4. Magufuli amechagua timu mbovu ya kampeni ambayo haina uzoefu na masuala haya ya pilika pilika. Watu wengi ikiwemo Mimi, tulitarajia kwenye timu ya kampeni ya ccm mwaka huu wangeweka full mkoko. Pale Kuna Nape, Makamba, Mzee Mangula pamoja na viongozi wengine wabobezi ndanibya chama. Lakini uwepo wa watu Kama Polepole na Bashiru kumefanya timu ya kampeni kupwaya sana ndani ya CCM. Angalia hata upangaji wa ratiba tu unawacost.
Sioni wapi CCM watashinda iwapo uchaguzi huu utafanywa kwa kufuata misingi ya Sheria ambazo wao wenyewe ndiyo wameziweka. Iwapo tume watakuwa tayari kumtangaza hata wasiyempenda, sioni CCM watashinda vipi.
Asalam Alleykum