Mideko
JF-Expert Member
- Mar 30, 2015
- 36,522
- 196,618
katika mji mkuu wa Kinshasa, mtandao umekuwa haufanyi kazi tangu alfajiri huku ukiwa chini katika miji muhimu ya Goma na Lubumbashi.
Kampuni ya huduma za intaneti duniani ilituma ujumbe kwa wateja wake kwamba serikali imeamuru kufungwa kwa huduma hiyo, ripoti za AFP zimesema.
AFP imesema kuwa wawakilishi wa Vodacom pia wamesema kuwa serikali iliwaagiza kufunga mawasiliano ya intaneti. lakini waziri wa mawasiliano Emery Okundji aliambia BBC alikuwa hafahamu kuhusu hali hiyo.
Kundi la kampeni la mgombea wa upinzani Martin Fayulu liliishutumu serikali kwa kuamrisha kufungwa kwa mtandao ili kusitisha matangazo ya ushindi mkubwa wa mgombea wake.
Waziri wa mawasiliano nchini humo Emery Okundji alisema kuwa hajui kuhusu hali hiyo. Wachunguzi wamelalamikia visa vya wizi wa kura wakati wa uchaguzi huo.
Chanzo_: Bbc
Kampuni ya huduma za intaneti duniani ilituma ujumbe kwa wateja wake kwamba serikali imeamuru kufungwa kwa huduma hiyo, ripoti za AFP zimesema.
AFP imesema kuwa wawakilishi wa Vodacom pia wamesema kuwa serikali iliwaagiza kufunga mawasiliano ya intaneti. lakini waziri wa mawasiliano Emery Okundji aliambia BBC alikuwa hafahamu kuhusu hali hiyo.
Kundi la kampeni la mgombea wa upinzani Martin Fayulu liliishutumu serikali kwa kuamrisha kufungwa kwa mtandao ili kusitisha matangazo ya ushindi mkubwa wa mgombea wake.
Waziri wa mawasiliano nchini humo Emery Okundji alisema kuwa hajui kuhusu hali hiyo. Wachunguzi wamelalamikia visa vya wizi wa kura wakati wa uchaguzi huo.
Chanzo_: Bbc