Kipindi cha Kikwete tumeona "life span" imepanda kwa miaka zaidi ya miaka 5 kwa miaka 7 tu. Haijwahi kutokea kabla yake, wakati Nyerere anamuachia Mwinyi madaraka "life span" ya Mtanzania ilikuwa miaka 48 tu. Kipindi cha Mwinyi na Mkapa ikapanda miaka 2 (imagine kwa miaka 20 imepanda kutokea 48 na kufika 50), kipindi cha Kikwete imepanda na kufika 55, ni miaka 7 kwa miaka saba tu. Halafu huyo huyo anaonekana mbaya kwenye afya.
Life span aliyoacha Nyerere 48 years - Miaka 24 ya kutawala
Life span waliyoacha Mwinyi na Mkapa 50 years - Miaka 20 ya kutawala
Life span iliyopo wa huu wa Kikwete 57.4 years - Miaka 7 ya kutawala. (rikodi ya dunia).
Source:
World Development Indicators and Global Development Finance - Google Public Data Explorer
Afya haipatikani hospitali pekee, ni kuanzia kwenye lishe, namna ya kukinga maradhi, huduma za mwanzo (vituo vya afya).
Hakuna aliyemfikia Kikwete kwa hayo yote. Vituo vya Afya na zahanati ni vingi zaidi kuliko wakati wowote, huduma ya mwanzo ni kubwa zaidi kuliko wakati wowote (vibajaji ni mfano mzuri), Kuzuwia maradhi (vyandarua ni mfano mmoja wapo).
Rais Kikwete alipoingia madarakani tu alikutana na matatizo sugu na makubwa matatu aliyoyarithi kutoka kwa Mkapa nayo ni; Njaa, Umeme na Ujambazi (nani asiyekumbuka?). Na akayashughulikia hayo ipasavyo. Bado tu ni mbaya?