How much do you spend in weddings for a year?

Hapana Radical, kwa mtu asiyemwelewa atanikosoa na sio kusuta...
kama wewe hujaoa mwambie mchumba wako unataka harusi ya watu 10 na huitaji mchango kwa vile mtatumia laki 5 au 6 uone atakupa jibu gani.

Kwa maelezo zaidi soma hii koti hapa ya sister pretty

Sikumaanisha kihivyo boss, my message was that female wangekuangukia coz najua wasingekubali kuambiwa ving'ang'anizi.
 
Wazazi wengine wanapenda sifa so ukienda na ka-idea kako wana-kabrush off wanakuuliza vipi dogo unadhani hatuna marafiki na ndugu...unakuwa mdogo
 
Wenye kumbi za sherehe nao wamegundua hilo deal. Ukigusa tu unaambiwa tsh 1,000,000, za ukumbi, chakula 10,000 - 20,000tsh per plate na vinywaji navyo vinapandishwa bei basi mnakusanya hela yoote mnampelekea kwa maumivu.
 
ukianza kuhesabu utaona ni nying sana ila ni mambo ya kijamii zaidi huwezi kukwepa. ila inabidi system ya harusi nzima ibadilishwe maarusi wawe wanapewa kiasi kikubwa tofauti na ile zawadi ya kamati
 
Hii posti hapa chini naona imejibu swali la "kwa nini watu hawachangishani kugharimia elimu au afya"


kuna harusi moja ndugu wa bi harusi tulikusanya milioni 8 na ushee kwa send off tu, nikashauri tupange sherehe ya kawaida tu simple ya kumuaga bini halafu tuwape maharusi angalau milioni tatu wanunue hata kakiwanja...watu waka kataa kata kata...wakaishia kuwapa jiko la gesi la alfu 60 ati ndio zawadi ya kamati...halafu kwenye vunja kamati watu wakatumia mapesa meeengi kunywa na kula


Mnawataka "watanzania" wabadilike, je, watu weupe huwa wanatumia fedha kiasi gani kwa leisure, relaxation or socializing?

Hizi fedha za harusi zingekuwa zinapelekwa nje ya nchi ningehamaki.
Mnataka taifa la makundi ya watu waliojiajiri wenye vipato halali .....au taifa lenye watu wachache wanaovuna jasho la mlalahoi isivyo halali?
 
na utaowa tu!!!! labda uamuwe kuwa padri!!! si umechangia $5000 na wao watakuchangia usiogope

Hahahaha,

Unalazimisha sasa? Mimi sijapata anayekuwa na principles zangu za Kikafiri.
 
Kuchanga inategema na unavyojisikia. Sioni haya wala aibu kuchanga elf 15, 20, 30 kadiri na nipatacho na ninavyojisikia na ukaribu wangu na mhusika. Na kama sina au sijisikii sikupi tu na nakuangalia usoni nakwambia - sina kwa sasa. Sitakuwa mtumwa kamwe wa kuchanga michango ya harusi za kifahari bila sababu, unajikuta una kadi kumi kwa mwezi, mkeo tano, mkitoa elfu 50 nlika kadi ni Tshs laki 6. Shauri zenu na sifa zenu. Jamaa zangu nawaambiaga, ukitaka harusi ya kifahari, kaza buti tafuta hela, ila sitatembeza mikadi kila mahali.
 
Hahahaha,

Unalazimisha sasa? Mimi sijapata anayekuwa na principles zangu za Kikafiri.

inabidi nikulazimishe sasa maana we mwanume umezidi khaaaa!!! upadiri hutaki sasa na kuo pia tukuache tu....no wei

lazima kuna atakaeafikiana na principles zako za kikafiri au 'atakaekuweza'...

hata ibilisi ana wakwake bluray..iweje wewe???
 
inabidi nikulazimishe sasa maana we mwanume umezidi khaaaa!!! upadiri hutaki sasa na kuo pia tukuache tu....no wei

lazima kuna atakaeafikiana na principles zako za kikafiri au 'atakaekuweza'...

hata ibilisi ana wakwake bluray..iweje wewe???


Tofautisha "kuwa na wako" na "kuoa"

Unaweza kuwa na wako bila kuoa, na unaweza kuoa bila ya kuwa na wako.

Akili kumkichwa.
 
Tofautisha "kuwa na wako" na "kuoa"

Unaweza kuwa na wako bila kuoa, na unaweza kuoa bila ya kuwa na wako.

Akili kumkichwa.

haya basi ninayemzungumzia mimi hapa ni yule wa kuoa....achana na mapungufu ya lugha.

maana wewe ulisema huoi ng'oo!!!
 
Kuna rafiki yangu alifanya harusi ambayo ilikuwa na watu 30 tu. Nikamuuliza mbona watu kidogo akaniambia kila aliyepo hapa ni mtu muhimu sana kwake, lengo lake ni kufurahi na watu waliokuwa na umuhimu katika maisha yake. Na hakutuomba michango :) Na mimi nikijaaliwa kuolewa nitamuiga yeye kwasababu kuna rafiki yangu alioa halafu nusu ya wageni waalikwa hawafahamu kwasababu ni watu waliotoa michango na wanafahamiana na wanakamati!!!
 
Kuna wakati enzi zile tupo wadogo, harusi zilikuwa zinafanyika majumbani, wanawake wanapika weee, wana changishana vyombo, sebule inaandaliwa, tent la kijani linapigwa uwani, ndugu jamaa marafiki na majirani wanakuja...harusi moto moto, watu kuimba na kucheza mpaka makoo yanakauka hakuna DJ wala nini sana sana music system ya uncle inaletwa basi...kina aunt na madada walimbwende wanasaidiana kumpodoa bi harusi halafu anachaguliwa rafiki au ndugu machachari kwa kuongea anakuwa ndio MC...na harusi zilikuwa zinapendeza tuu

sasa haya mambo ya ukumbi milioni, mapambo laki kadhaa, chakula mpaka cattering, DJ, muziki, MC, Saluni, kukodi magari nk nk nk sijui yametokea wapi yarabi..
 
Kuna wakati enzi zile tupo wadogo, harusi zilikuwa zinafanyika majumbani, wanawake wanapika weee, wana changishana vyombo, sebule inaandaliwa, tent la kijani linapigwa uwani, ndugu jamaa marafiki na majirani wanakuja...harusi moto moto, watu kuimba na kucheza mpaka makoo yanakauka hakuna DJ wala nini sana sana music system ya uncle inaletwa basi...kina aunt na madada walimbwende wanasaidiana kumpodoa bi harusi halafu anachaguliwa rafiki au ndugu machachari kwa kuongea anakuwa ndio MC...na harusi zilikuwa zinapendeza tuu

sasa haya mambo ya ukumbi milioni, mapambo laki kadhaa, chakula mpaka cattering, DJ, muziki, MC, Saluni, kukodi magari nk nk nk sijui yametokea wapi yarabi..


Ishakuwa mambo ya mashindano.

Hamna kuoa, ni show tupu.
 
harusi inatakiwa iwe nzuri ya kuridisha lakini isiwe na israf na ufujaji wa pesa wala kujionyesha.

nafikiri tutakapoanza kufanya harusi kwa uwezo wetu tu bila ya kuchangishana basi tutafanya harusi z kiasi

Mzee ume-summarize kila kitu. I see the future ...

nashukuru mungu na namuomba aendelee kunisaidia niwe nakaidi kuchanga.

Tuko pamoja. Mwanzo mgumu lakini wataelewa tu ...

dawa ni kugoma kuchangia! Kwani hawataoana?? Watu wanapendana huko halafu kero na usumbufu kwa wengine!

Yaani mtu unafuatwa na michango ya harusi..utadhani una deni la mtu!

Watu bwana! We acha tu!

Hahaha utamaduni hujengwa na watu wenyewe. Ukikubali kuchangia ujue unasaidia kuuendeleza utamaduni. Usimlaumu yeyote bali we mwenyewe.

ukianza kuhesabu utaona ni nying sana ila ni mambo ya kijamii zaidi huwezi kukwepa. ila inabidi system ya harusi nzima ibadilishwe maarusi wawe wanapewa kiasi kikubwa tofauti na ile zawadi ya kamati

Jisemee mwenyewe. Sema "siwezi kukwepa". Wenzako wengine wanaweza.

Kuchanga inategema na unavyojisikia. Sioni haya wala aibu kuchanga elf 15, 20, 30 kadiri na nipatacho na ninavyojisikia na ukaribu wangu na mhusika. Na kama sina au sijisikii sikupi tu na nakuangalia usoni nakwambia - sina kwa sasa. Sitakuwa mtumwa kamwe wa kuchanga michango ya harusi za kifahari bila sababu, unajikuta una kadi kumi kwa mwezi, mkeo tano, mkitoa elfu 50 nlika kadi ni Tshs laki 6. Shauri zenu na sifa zenu. Jamaa zangu nawaambiaga, ukitaka harusi ya kifahari, kaza buti tafuta hela, ila sitatembeza mikadi kila mahali.

Nimependa msimamo wako. Ila we hukuwachangisha? :) Maana nilicho notice kingine ni kwamba watu hawapendi kuchangishwa (na inawaauma kweli kuzitoa) lakini kwenye zamu yao wanakuwa experts wa kukusanya michango. I don't know what happened to "do unto others what you would like to be done unto you".

Si vibaya kumsaidia ndugu au rafiki kukamilisha vizuri shughuli kama hiyo ambayo ni muhimu sana kwake. Lakini katika mtindo huu wa kisasa, mtanisamehe bure tu.

Kosa la kwanza wanalofanya ni kuniambia ni-pledge. Huu ni mtindo mmbaya sana huu. Yaani ni kama kamfumo flani ka kutumia peer presure kumlazimisha mtu kutoa zaidi ya uwezo wake. Mimi nimeacha ku-pledge kabisa. Nnatoa kama nnajisikia kuto kwa kiasi nnachoweza na kutaka kutoa wakati ninatoa. Nilimuonea huruma rafiki yangu mmoja aliponiweka kwenye laud-speaker wakiwa kwenye kikao na washkaji wengine akidhani kwamba hiyo ingesaidia.

Mwingine alishangaa nilipo-pledge 500; imefika zamu yangu nnawaomba kwa utaratibu wani-excuse maana sintoweza ku-pledge kabla ya kuangalia budget yangu wao hawanielewi (maana hata shughuli yenyewe hatukuambiwa ni ya nini mpaka tunafika pale). Basi nikawaambia 500. Wakacheka wakidhani nnatania; iliwachukua muda kidogo kutambua kwamba sitanii. Nikatimiza ahadi, lakini sikuja hata kuambiwa harusi inafanyika lini.

Naungana mkono kabisa na Gaijin. Watu waanze kutayarisha harusi zao wenyewe kadiri ya uwezo wao. Mtu akiamua atumie 25M yake yote kwenye harusi yake, that is fine with me. Lakini hiyo 25M inapotoka kwa wengine, tena baadhi yao inabidi wachague kati ya kutoa mchango au kupeleka mtoto shule, inaanza kuwa mbaya kabisa.

Juzi juzi hapa ndugu mmoja aliye katika harakati za kuchangisha aliniomba nimpe namba ya ndugu mwingine ili akakusanye na huko. Hapo ilikuwa haijapita hata wiki mbili tumetoka kumkopesha huyu ndugu wa pili pesa za ada za watoto waliorudishwa nyumbani. Hivi nilikosea nilivyomnyima? Yaani hata hatutaki kujua watu wanaishije au wanatoa wapi hizo pesa, tunataka michango tu. Ndio maana ndoa nyingine zinakufa so prematurely, unakuta mmekusanya mpaka pesa za dawa za wagonjwa halafu mnategemea hiyo ndoa idumu kweli?

Unajua hata kama unachangisha watu, kumbuka hawa ni binadamu na wana mahitaji yao binafsi. Na hujui hizo pesa wamezitoa wapi, au wamefanya nini kuzipata. Usipite kama vile wana visima vya hela majumbani kwao, na kwamba wana wajibu wa kukupa wewe, au walikuwa wanakusubiria wewe upendane na mtu ndio zitumike.

At least usije kwangu kuchangisha. Nitaarifu tu kwamba unao/unaolewa, kama inakupendeza mimi kujua.
 
Kuna wakati enzi zile tupo wadogo, harusi zilikuwa zinafanyika majumbani, wanawake wanapika weee, wana changishana vyombo, sebule inaandaliwa, tent la kijani linapigwa uwani, ndugu jamaa marafiki na majirani wanakuja...harusi moto moto, watu kuimba na kucheza mpaka makoo yanakauka hakuna DJ wala nini sana sana music system ya uncle inaletwa basi...kina aunt na madada walimbwende wanasaidiana kumpodoa bi harusi halafu anachaguliwa rafiki au ndugu machachari kwa kuongea anakuwa ndio MC...na harusi zilikuwa zinapendeza tuu

sasa haya mambo ya ukumbi milioni, mapambo laki kadhaa, chakula mpaka cattering, DJ, muziki, MC, Saluni, kukodi magari nk nk nk sijui yametokea wapi yarabi..
Unisamehe sana Triplets kwa kauli yangu hii, naomba nikutangazie kwamba tayari umepitwa na wakati.


Wandugu, kuna aina ya harusi ambazo hamzitaji hapa, zile za jamaa walioshindwa kukodi gari la 500,000. Kutokana na uwezo wao mdogo, walitumia magari maku-kuu ya ndugu wenye afadhali kiuchumi.
Mwezi uliopita niliona msafara wa maharusi wenye magari matatu, kati ya hayo mawili ni taxi.
Kwa hiyo, si kila mtu anafanya mashindano kama ambavyo imeanza kuonekana kwenye hoja zinazotolewa.

Wapo pia watu walio kwenye status ya juu kiuchumi ambao hususia kwenda kwenye shughuli za ndugu zao wakijua kwamba watajidhalilisha wakihudhuria, kwani ukumbi unaweza kuwa kama ule wa kipaimara cha mwaka jana - ukumbi ambao pembeni ni baa, meza kuu iko karibu na mlango wa choo, halafu jirani kuna ukumbi mwingine unaopiga mziki mkubwa kwa hiyo kusikilizana hakupo.
 
Mi nilitaka kufanya harusi simple sana lakini wee! Mpenzi akaniona kama namdhalilisha. I had to go through the ordeal of looking around for michangos and other troubles I could avoid.
 
Back
Top Bottom