sio asikaribishwesitta hata kkkt kanisani asikaribishwe tena, huu ni wizi wa mchana ... Anatenda dhambi anajua anatenda dhambi ... Wananchi wanashida wao wanachezea pesa! .... Angalia tu jinsi rais aliporudi dar kwenda temeke kukagua kambi ya ebola akakuta ni tofauti na matarajio yake .... Pesa hakuna!!!
Uhuni huu wa CCM na serikali yake bila kujali haki za wananchi ipo siku watajutia kupingisha kilichotoka kwa wananchi kwa masilahi yao binafsi.Sitta ni mhuni jana, leo na milele. CCM ni wezi, jana, leo na hadi kiama.
Mi nazidi kuwashauri wajumbe wa CA ingawa ni too late waonyeshe huruma kidogo kwa walala hoi wa nchi hii.
Inasikitisha kule kuna hadi wachungaji, maaskofu na wazee wa kanisa lakini dhamira zao zimeuawa na hawaoni kuwa mabilioni wanayoteketeza hapo Dodoma yangeweza kwenda kuokoa maisha ya watanzania wanaokufa kwa kukosa huduma za afya nchi hii
Inasikitisha sana...
Nashangaa mna mlaumu sitta kwa lipi. Wakulaumiwa ni UKAWA ambao walikacha kwa masudi kuendelea na bunge. Nia nzuri ya Kikwete kuwaachia wa Tanzania katiba mpya imekwamisha na uroho na ubinafsi wa ukawa
Huwa nikiangalia picha ya Sitta nahisi kichefuchefu...
kingine kizuri ni kwamba roho katili ya sitta imedhihirika mapema,.. i cant believe wameamua to rob the poor and the hungry in broad day light!
nimesikia ujuha mwingine ndio ukanitia kichefu chefu kabisa .... eti wana mpango wa kuhakikisha wale walioko nje ya bunge nao wanapewa fursa ya kupiga kura .... utoto na unafiki wa Sitta hauishi .... mtu hayupo bungeni ni kwamba kwa sababu moja au nyingine HAYUPO FULLSTOP ... wafanye uamuzi walioko ndani kama vikao vingine vya bunge!
Hiyo katiba ya watanzania ndiyo inajadiliwa au umekurupuka tu...Nashangaa mna mlaumu sitta kwa lipi. Wakulaumiwa ni UKAWA ambao walikacha kwa masudi kuendelea na bunge. Nia nzuri ya Kikwete kuwaachia wa Tanzania katiba mpya imekwamisha na uroho na ubinafsi wa ukawa
Hivi Sitta hana mtu wa kumuwajibisha? Jk naye anashindwa nini kuonyesha nguvu ya uraisi kwa kulivunja hili bunge. Mnapo sema mtaendelea na mchakato 2015 mna hakika gani raisi ajae atakubali huu uhuni uliofanywa na bunge la Sitta let alone ccm kushinda.
...kiukweli kale kazee kamechemsha sana, kanalazimisha tu hata hakaoni aibu. akidi haitimii kamekomaa mpaka wanawatisha wana ccm waliogoma kufanya ujinga huu. baada ya kuona hawatishiki basi kameamua kuwapa fursa ya kupiga kura kule waliko. Wamempa fursa ya kuonekana anabusara kuahirisha mchakato yeye kakomaa tu. hata muuza muuza ugolo hawezi kufanya maamuzi kama haya ya mzee 6...!!
Hii nchi ina mambo ya ajabu sana. Rais wa nchi aliyeunda tume ya Warioba hana mamlaka ya kusimamisha hili Bunge la Posho! Mwenye mamlaka hayo ni huyo fisadi Sitta!!! Hivi hii sheria ya Bunge hili la posho kutoweza kuvunjwa na Rais bali mwenye mamlaka ya kulivunja ni Spika ilitungwa katika kikao kipi cha Bunge? Kama kuna mtu ambaye amewahi kuiona sheria hii hebu aiweka hapa. Kweli hi nchi ni kichwa cha mwendawazimu, Rais wa nchi anaona pesa za walala hoi bilioni 21 zikiteketea bila la maana lolote kufanyika. Rais kauchuna tu!!!
Hivi Kikwete leo hii akiamua kulivunja Bunge hili la posho, mamlaka ambayo hana je, atachukuliwa hatua za kisheria zipi!? Na ni taasisi ipi itakayomchukulia hatua za kisheria Rais? Bunge la posho au Bunge la Jamhuri? au ni Sitta ndiye atampandisha kizimbani Rais? Je, Rais kwa kulivunja Bunge hili la posho na hivyo kunusuru mabilioni ya pesa za walipa kodi anaweza kufungwa au kuondolewa madarakani kwa nguvu!? Ujinga umezidi kukithiri nchi hii.