Kumekuwa na kauli za kukinzana za Mh. Magufuli pale anapokuwa anahutubia wananchi kwa hotuba za Kichwani.
Mfano: Nimejitoa Mhanga kutumbua majipu. Hatachomoka mtu.
Baadae, Nitawalinda wastaafu wote, waishi kwa amani.
Nataka watanzania wawe na maisha bora.
Baadae, Nitawashusha wanaoishi kama Malaika waishi kama shetani.
Ni marufuku kuagiza Sukari toka nje.
Baadae, Serikali imeagiza sukari ili kufidia upungufu wa Sukari nchini.
Hii ni mifano ya kauli tata, alizowahi kutamka Mh. Magufuli anapotoa Hotuba toka Kichwani.
Ushauri: Mh. Magufuli, achana na hotuba za kutoa Kichwani, anza kusoma hotuba. Usipofanya hivyo utaendelea kujichanganya na kuwachanganya wananchi.
Kwenye suala la diplomasia na busara tukubaliane Raisi wetu siyo mtaji wake..Hata kama ulikuwepo uwanja wa Taifa na kusikiliza hotuba yke ya kwanza kama Raisi yaani alikuwa anachanganya tu mambo.Ila ndo Magu huyo,tutamisi sana hotuba za Msoga.how comes Rais wa nchi anaongea vile?
Kweli ss watanzania tuna shida kichwani..... Cjui akae nani asiletewe dosari.
Yeye ndo mkuu hakuna, jaji kamteua yeye lazima jaji alipe ili aendelee kuwa pilato,Sasa huoni kuwa jamaa wa NIDA keshahukumiwa na akipelekwa mahakamani jaji lake ni moja tu, kumfunga? Kimsingi magu asiwe anatoa hukumu kwani anawanyima wanasheria uwezo wa kufanyakazi kwa kuwaingilia. Hebu awaachie wenye kazi yao kwani watatoa hukumu za kumpendeza yeye na hii ni kinyume cha haki.
Inawezekana hata sio mtu wa NIDA mkuu. Labda ni kimada wa Mkurugenzi aliyepangishiwa apartment na kupewa Vitz. Sasa pesa zimekuwa Adimu maana jamaa serikali imefreeze assets na mkwanja. Mbwembwe za Insta kwisha,utaacha kumuona Mh. Rais kavu!!?? Tehe tehee.Watu wa NIDA utawajua tu