Jakaya Mrisho Kikwete ni Rais wa ajabu sana, anahutubia taifa lakini toka ameanza kuongea haongelei mambo specific kwa nchi yake, naona anaongea mambo too general, ni hotuba ambayo mtu yeyote anaweza tu kuiandika, sio htuba ya rais, mtu tunayetegemea atuambie mipango ya nchi na utekelezaji wa baadhi ya mipango yetu ya hapo awali (kama ilikuwepo).
Ametumia muda wake wote kuelezea mkutano wa AGRA uliofanyika Arusha, amemshukuru Kofi Annan kwa kuleta mkutano wa AGRA Tanzania, amesema hiyo ni heshima kubwa kwa nchi, akaendelea kumshukuru waziri wa kilimo na mkuu wa mkoa wa Arusha kwa kuandaa mkutano mzuri, ameusifu uongozi wa hoteli waliyolala hao wageni, kwamba walihudumiwa vizuri.
Rais ametumia muda mwingi kuelezea hiyo AGRA ni kitu gani, na kwamba mkutano wa kwanza ulifanyika accra Ghana na sasa huu ni mkutano wa pili, kwa hiyo tumepewa heshima kubwa! pia ameeleza jinsi AGRA inavyosaidia kuendeleza kilimo katika nchi za Africa.
Jaribu ku-imagne, Obama ametoka kwenye UN General assembly sasa anahutubia taifa, anawaeleza wananchi wake hiyo UN General assembly ni kitu gani, ilianzishwa lini, kazi zake ni nini, yaani kama anafundisha watoto wa shule hivi.
Tuna hali ngumu, tunahitaji visionary, tunahitaji mtu anyeweza kutuvusha hapa, ninasikitika kusema hivi, lakini silioni hili kwa Rais wangu wa sasa