Columbus
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 2,002
- 648
Kiasi fulani niliipenda hotuba ya Mkuu jana ingawa kuna maswali mengi ambayo hakuyatolea majibu km aliposema waajiri wanatoa masharti magumu wanapotangaza nafasi za kazi, kipengele cha uzoefu kinawazuia vijana wanaotoka vyuoni kupata kazi. Nilitegemea yeye Mkuu angetoa dira, ni kweli vijana hawana uzoefu ktk kazi na hii imetokana na wanafunzi vyuoni kukosa elimu ya mazoezi ya kutosha (field work). Pengine serikali ione umuhimu wa kutenga fedha zaidi kwa vyuo vyetu ili wanavyuo waweze kupata field work zaidi ili wasiwe kikwazo kwa waajiri pale wanapoajiriwa.Nawasilisha.