Hii sio hotuba makini kabisa,
1. Huwezi funga safari ukaenda kumusuta mtu nyumbani kwake.
2.Hao wanaotupa msaada si kwamba wanakupendeni wao wanataka uendelee kuwa hivyo, ili watoto anaowasema Dr. Slaa kuwa kodi zao zinalipa sisi, ni kinyume chake ni ili hao watoto wapate kwenda choo.
3. Anawaomba elimu, wakati hiyo ndo silaha yao mhimu ya kuhakikisha hawakupi hiyo elimu ili hao watoto waendelee kwenda shule na choo. wametunyima hiyo elimu ili tuendelee kuwafanya watuuzie hilo box la viatu, sasa akikupa hiyo teknolojia yeye box la viatu hataliuza wapi? Sana sana alichokifanya Slaa ni kuwaambia wabadiri namna ya kutunyima elimu kwa staili nzuri na yenye kasi zaidi.
Hotuba mbovu kabisa.
Ni sawa unajibu sahihi ktk swali tofauti.
Nafikiri Dr Slaa, pia anaangalia mambo kwa pepeteo jepesi sana, swala la elimu la kiteknolojia, huwezi kulichukilia kijepesi namna hiyo, labda kama anaongela elimu ya kukalili na kushusha ma equation ya akina aboti na rampati hapo sawa.
Elimu anayongelea inatakiwa ujasusi wa kutosha, ni swala la kijasusi kama ulivyo ujasusi mwingine na ili ulifanikishe linahitaji usiri na kuachana na hotuba zisikuwa na tija. Swala hili ili ufanikiwe lazima uandae SPECIAL FORCES, ambao wao unawapenyeza kwenye system za nchi zilizoendelea kiteknolojia, na wanakuwa wanatoa feedback huku TASK FORCE nyingine home kazi ni ku reverse engineering.
University za ukweli ulaya zinazofundisha mambo ya ukweli huwezi ingia murugaruga huko. sanasana utaingia kwenye university za kupigwa theory na viji hands-on ambavyo system zimeshatengenezwa tayari. Nchi nyingi utasikia hizo university ni military university sasa kuja kuingia huko kwenye military university nafikiri unafahamu ni nini kinapaswa.