Toka maktaba:
View: https://m.youtube.com/watch?v=tMtyZvDJWGI
Mjumbe wa Kamati ya Katiba Pendekezwa ndugu Humphrey H. Polepole ahoji mambo mengi mazito ktk ukumbi wa Mlimani City .. kuwa hii Katiba pendekezwa ya 2014 ni katiba ya Kimapinduzi iliyokusanya maoni ya wananchi na siyo maoni ya viongozi kama wabunge n.k
Katiba hii pendekezwa inatoa nafasi kuwawajibisha viongozi waliochaguliwa na wananchi bila kusubiri muda wao wa kukaa madarakani baada ya uchaguzi uishe, ni kwamba kama kiongozi haeleweki basi atafungashiwa virago mapema kabla ya miaka mitano kuisha..
Yule mwamba wa movie Arnold Alois Schwarzenegger gavana wa ... aliingia madarakani baada ya wananchi wa jimbo kuonesha kutokuwa na imani na mtangulizi wake ndipo akapata nafasi ya kuchaguliwa mwigizaji mwamba Arnold Alois Schwarzenegger .. nchi nyingi katiba zao zinaruhusu kiongozi kuondolewa madarakani kabla ya muhula wake kuishi Kenya, Peru, Ecuador, Uswiss kwa kutaja kwa uchache ...kiongozi huweza kuondolewa kikatiba anapofanya vitu visivyoeleweka kwa wapiga kura wake..
..
Humphrey Polepole, aliitaka serikali kusambaza Katiba inayopendekezwa pamoja na rasimu ya Tume hiyo kwa wananchi ili waisome na kuielewa kabla ya kuipigia kura ya maoni.
Kuhusiana na suala la elimu ya wabunge, alisisitiza kuwa ni vema wabunge wawe na elimu ya kidato cha nne, tofauti na katiba inayopendekezwa inayowataka wawe wanajua tu kusoma na kuandika.
Alisema endapo Katiba itapitishwa kama ilivyo kwamba wabunge wajue kusoma na kuandika pekee, itamuwia vigumu rais kupata mawaziri wenye elimu ya kutosha ya kusimamia shughuli za maendeleo ya nchi.
“Unawezaje kusema wabunge wawe wanajua kusoma na kuandika tu, isipokuwa mawaziri, je, wakichaguliwa wabunge wote ambao uwezo wao ni wa kusoma na kuandika tu, hao mawaziri watatoka wapi na shughuli za maendeleo wataendeshaje?” alihoji Polepole.
Kadhalika, alisema kuwa anashangaa mawaziri kuipigia chapuo Katiba inayopendekezwa na kuipinga serikali tatu, wakati hata wao walitoa maoni wakiitaka muundo wa serikali hizo.
“Mimi nilishiriki katika kikao cha kukusanya maoni ya mawaziri, walipendekeza serikali tatu, na hata baadhi ya mawaziri wakuu nao walipendekeza serikali hizo, na wasitake tufikie huko wanakotaka, wakibisha tunaweza kuwataja,” alisema huku walioshiriki mdahalo huo wakitaka awataje. Na akaongeza hii katiba mpya ni kwa ajili ya wananchi kuweza kuwadhibiti viongozi lakini, nashangaa viongozi wanapinga haki hiyo ya msingi ya wananchi kuweza kuwadhibiti viongozi waliowachagua pale vigogo hao wanapokengeuka
Pia ukumbini waliokuwa wajumbe Tume ya Mabadiliko ya Katiba wameendelea kuikosoa vikali Katiba inayopendekezwa na kusema kwamba haitakuwa na manufaa kwa Watanzania.
Kadhalika, wamesema Muungano uliopo kwa sasa upo katika hatari ya kuvunjika na kwamba hali hiyo itasababishwa na Katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba (BMK).
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba (pichani chini), akizungumza katika mdahalo wa kujadili katiba inayopendekezwa uliofanyika ukumbi wa City jijini Dar es Salaam jana, alisema Katiba hiyo imeondoa matarajio ya wananchi waliotegemea kupata katiba ya kuwakomboa katika miaka mingine 50 ijayo.
Alisema Muungano umefika hapa ulipo, umetokana na kudra za Mwenyezi Mungu na hekima za viongozi waliopita kwa kuuendesha kwa hekima licha ya katiba hiyo kubeba changamoto lukuki.
“Mimi nimeshangaa kuona waheshimiwa hawa wananitukana na kunikashfu eti nimemsaliti Mwalimu Nyerere, wanadiriki kutumia nguvu na maneno ya kashfa kupitisha katiba. Katiba haiwezi kupitishwa kwa namna hiyo, katiba ni maridhiano ambayo pia yanashirikisha maoni ya wananchi,” alisema Warioba na kuongeza:“Hata kama Nyerere angelikuwapo leo angeipinga Katiba hii inayopendekezwa.”
Warioba alisema hata kama wataipitisha kwa nguvu, lakini wanatakiwa kufahamu kuwa italeta matatizo baadaye na ni vizuri wafahamu kuwa hata kama itapita itakuwa na matatizo
Hoja za Humphrey Polepole ni moja ya hotuba zilizowanyanyua kutoka vitini wananchi waliojazana ukumbi huku pia majumbani familia na marafiki wakikodolea skrini za televisheni zao kufuatilia hotuba motomoto kutoka ukumbi wa Mlimani City.
November 26, 2014
Mlimani City, Dar es SalaamHotuba ya karne ya Humphrey Herson Polepole iliyowainua watu Mlimani city 2014
Alichosema Polepole katika Mdahalo wa Katiba Mlimani - City 2014 kinachoishi jana, leo na hadi keshoAmb. Humphrey H. Polepole
View: https://m.youtube.com/watch?v=tMtyZvDJWGI
Mjumbe wa Kamati ya Katiba Pendekezwa ndugu Humphrey H. Polepole ahoji mambo mengi mazito ktk ukumbi wa Mlimani City .. kuwa hii Katiba pendekezwa ya 2014 ni katiba ya Kimapinduzi iliyokusanya maoni ya wananchi na siyo maoni ya viongozi kama wabunge n.k
Katiba hii pendekezwa inatoa nafasi kuwawajibisha viongozi waliochaguliwa na wananchi bila kusubiri muda wao wa kukaa madarakani baada ya uchaguzi uishe, ni kwamba kama kiongozi haeleweki basi atafungashiwa virago mapema kabla ya miaka mitano kuisha..
Yule mwamba wa movie Arnold Alois Schwarzenegger gavana wa ... aliingia madarakani baada ya wananchi wa jimbo kuonesha kutokuwa na imani na mtangulizi wake ndipo akapata nafasi ya kuchaguliwa mwigizaji mwamba Arnold Alois Schwarzenegger .. nchi nyingi katiba zao zinaruhusu kiongozi kuondolewa madarakani kabla ya muhula wake kuishi Kenya, Peru, Ecuador, Uswiss kwa kutaja kwa uchache ...kiongozi huweza kuondolewa kikatiba anapofanya vitu visivyoeleweka kwa wapiga kura wake..
..
Humphrey Polepole, aliitaka serikali kusambaza Katiba inayopendekezwa pamoja na rasimu ya Tume hiyo kwa wananchi ili waisome na kuielewa kabla ya kuipigia kura ya maoni.
Kuhusiana na suala la elimu ya wabunge, alisisitiza kuwa ni vema wabunge wawe na elimu ya kidato cha nne, tofauti na katiba inayopendekezwa inayowataka wawe wanajua tu kusoma na kuandika.
Alisema endapo Katiba itapitishwa kama ilivyo kwamba wabunge wajue kusoma na kuandika pekee, itamuwia vigumu rais kupata mawaziri wenye elimu ya kutosha ya kusimamia shughuli za maendeleo ya nchi.
“Unawezaje kusema wabunge wawe wanajua kusoma na kuandika tu, isipokuwa mawaziri, je, wakichaguliwa wabunge wote ambao uwezo wao ni wa kusoma na kuandika tu, hao mawaziri watatoka wapi na shughuli za maendeleo wataendeshaje?” alihoji Polepole.
Kadhalika, alisema kuwa anashangaa mawaziri kuipigia chapuo Katiba inayopendekezwa na kuipinga serikali tatu, wakati hata wao walitoa maoni wakiitaka muundo wa serikali hizo.
“Mimi nilishiriki katika kikao cha kukusanya maoni ya mawaziri, walipendekeza serikali tatu, na hata baadhi ya mawaziri wakuu nao walipendekeza serikali hizo, na wasitake tufikie huko wanakotaka, wakibisha tunaweza kuwataja,” alisema huku walioshiriki mdahalo huo wakitaka awataje. Na akaongeza hii katiba mpya ni kwa ajili ya wananchi kuweza kuwadhibiti viongozi lakini, nashangaa viongozi wanapinga haki hiyo ya msingi ya wananchi kuweza kuwadhibiti viongozi waliowachagua pale vigogo hao wanapokengeuka
Pia ukumbini waliokuwa wajumbe Tume ya Mabadiliko ya Katiba wameendelea kuikosoa vikali Katiba inayopendekezwa na kusema kwamba haitakuwa na manufaa kwa Watanzania.
Kadhalika, wamesema Muungano uliopo kwa sasa upo katika hatari ya kuvunjika na kwamba hali hiyo itasababishwa na Katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba (BMK).
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba (pichani chini), akizungumza katika mdahalo wa kujadili katiba inayopendekezwa uliofanyika ukumbi wa City jijini Dar es Salaam jana, alisema Katiba hiyo imeondoa matarajio ya wananchi waliotegemea kupata katiba ya kuwakomboa katika miaka mingine 50 ijayo.
Alisema Muungano umefika hapa ulipo, umetokana na kudra za Mwenyezi Mungu na hekima za viongozi waliopita kwa kuuendesha kwa hekima licha ya katiba hiyo kubeba changamoto lukuki.
“Mimi nimeshangaa kuona waheshimiwa hawa wananitukana na kunikashfu eti nimemsaliti Mwalimu Nyerere, wanadiriki kutumia nguvu na maneno ya kashfa kupitisha katiba. Katiba haiwezi kupitishwa kwa namna hiyo, katiba ni maridhiano ambayo pia yanashirikisha maoni ya wananchi,” alisema Warioba na kuongeza:“Hata kama Nyerere angelikuwapo leo angeipinga Katiba hii inayopendekezwa.”
Warioba alisema hata kama wataipitisha kwa nguvu, lakini wanatakiwa kufahamu kuwa italeta matatizo baadaye na ni vizuri wafahamu kuwa hata kama itapita itakuwa na matatizo
Hoja za Humphrey Polepole ni moja ya hotuba zilizowanyanyua kutoka vitini wananchi waliojazana ukumbi huku pia majumbani familia na marafiki wakikodolea skrini za televisheni zao kufuatilia hotuba motomoto kutoka ukumbi wa Mlimani City.