Viongozi wakuu wa umoja wa katiba ya
wananachi UKAWA wakiongozwa na
mwenyekiti wa chama cha Democrasia na
maendeleo CHADEMA Mh FREMAN MBOWE
pamoja na makamu mwenyekiti wa
CHADEMA Profesa SAFARI na kaimu
mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF
ambaye pia ni mbunge wa bunge la Africa
mashariki Mh TWALHA TASLIMA leo jioni
wamehudhuria Baraza la kuu la idd
lililoamndaliwa na Taasisi za kiislam
Tanzania shughuli iliyofanyika katika hotel
ya LAMADA Jijini Dar es salaam.
Katika shughuli hiyo ambayo iliambatana na
dua mbalimbali pamoja na hotuba za
viongozi mbalimbali pia walialikwa
wagombea urais wa vyama vyote Tanzania
lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kufika
huku mgombea wa UKAWA akiwakilishwa na
Mh FREMAN MBOWE.
Mh mbowe alipata nafasi ya kutoa Hotuba
fupi ambayo iliwagusa mamia ya waislam
ambao walikuwa katika shughuli hiyo na
hapa nimekunukulia baadhi ya mambo
ambayo mbowe aliyazungumza na kushtua
wengi
1-Nashukuru sana kwa ukaribisho wa
shughuli hi,mgombea wetu ndugu EDWARD
LOWASA alitamani kuwa nasi jioni hii lakini
kutokana na ratiba ya kampeni kubana
imebidi aunganishe kwenda kwenye
kampeni za kesho huko manyara-- MH
MBOWE
2-Swala la mashekh ambao wapo jela bila
hukumu yoyote,tulisema siku ya ufunguzi
wa kampeni na tunaendelea kusema kuwa
tumewaagiza wanasheria wa chama chetu
kufwatilia kwa makini na kuona nini hasa
kimetokea kwao kama kuna mahali
kunahitajika msaada wa kisheria tupo tayari
kulishuhulikia hilo kwani sisi lengo letu ni
kurudisha umoja na mshikamano Tanzania.
-- MH MBOWE
3-Zimebaki siku takribani 30 sasa kabla ya
watanzania kufanya maamuzi halisi,ni muda
wa maamuzi ndugu watanzania. -- MH
MBOWE
4-TANESCO imefilisika na watanzania wengi
hawajui hili,sasa shirika la umeme halina
hata sent na wameamua kufanya mgao wa
kimya kimya lakini ukweli ni kwamba huu
mgao ni mkubwa sana huko tuendako kwa
sababu hawana hela na wanaficha
ukweli,kuna mgao mkali sana sasa wa kimya
kimya na utaendelea kuwa mkali kadiri siku
zinavyokwenda. -- MH MBOWE
5-Kuna wizi mkubwa sana wa mafuta
Tanzania na kuna baadhi ya watu wakubwa
wanauratibu wizi huo,Tanzania ina akiba ya
mafuta hadi mwezi wa 11 lakini serikali
imetoa hati ya kuingiza mafuta nchini
ambapo baadhi ya wahusika ni familia ya
Rais KIKWETE. -- MH MBOWE
6-Serikali yetu ya awamu ya tano sio serikali
ya visasi kama inavyodhaniwa,ila ni serikali
ya kuwarudisha watanzania pamoja kwa
maridhiano,na maelewano,ila kuna watu
itabidi washughulikiwe kwa mijibu wa
sheria kutokana na kuligharimu taifa hao
tutafanya hivyo. -- MH MBOWE
7-Tume ya uchaguzi ya miezi miwili iliyopita
sio tume ya sasa,mwenyekiti yupo ila
watendaji wengi wameondolewa bila sababu
za msingi. -- MH MBOWE
8-Mtendaji mmoja mkuu wa tume juzi
tumepata taarifa kuwa ameondolewa na
kupelekwa kusikojulikana na amerudhishwa
na kutakiwa kukabidhi ofisi mara moja. --
MH MBOWE
9-Tume ya sasa inaongozwa na wanajeshi na
usalama wa taifa,mimi mbowe ndio nasema
kama kuna mtu anabisha waje wanikamate
leo,hatuwezi kuvumiliana kiasi hiki ni
wakati wa kuwekana wazi ili watanzania
wafanye jambo wanalolitaka. -- MH MBOWE
10-Nasema hivi hatutakubai hujuma hizi
ambazo zinaendelea sasa tutasema hadi
mwisho. -- MH MBOWE
11-Mwisho kabisa nasema hivi ni wajibu
wetu kutafuta kura,kupiga kura na kulinda
kura hivyo ndugu zangu waislam nawaomba
tushirikiane katika hili,ASANTENI KWA
KUNISIKILIZA-- MH MBOWE
Share