Hoteli nzuri ya kulala Mwanza

Hoteli nzuri ya kulala Mwanza

JATELO1

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2011
Posts
1,230
Reaction score
304
Habari,
Ndugu zangu, Kwa wenye uzoefu na Hoteli za Jijini Mwanza naomba msaada wenu wa kujua hoteli nzuri, safi na yenye ulinzi jijini Mwanza. Breakfast na Chakula siyo muhimu kwangu. Gharama isiwe zaidi ya 30,000 TZS kwa siku. Pia kwenye vyumba ni muhimu kuwe na kiti pamoja na meza nzuri ya kuweza kufanyia kazi kwenye Laptop na hata kuandikia. TV pia sio muhimu sana lakini kama ipo, then hakuna shida. Cha msingi ni usalama, usafi, maji ya moto kwa ajili ya kuogea, kiti, meza nzuri na isiwe nje ya Mji.

Natanguliza shukrani.
 
Ulizia mahala pazuri pa kufikia Mwanza kwa elfu thelathini sio Hoteli nzuri mkuu.
 
Kuna annox hotel iko furahisha..ila ni nzuri
 
Ryan's bay hotel ,,
Hapa utakula upepo Wa ziwa.


Aspain hotel mtaa Wa uswahilini .
Hapa utapata kipozeo bure,

Gold_crest hotel
Hapa ni mkabala na Mwanza hotel bajeti yako ndogo
 
Bei hiyo ni ya guest siyo hotel kiongozi
Bei ya Hotei ni Tshs. Ngapi kwa Mwanza? Mbona hata Dar na Arusha zipo Hoteli nzuri kwa hiyo bei? Naomba msaada wako kama ipo sehemu nzuri unayoijua kwa hiyo bei na inakidhi hivyo vigezo tafadhali.
 
Mkuu kwa nini kupata shida yote hiyo? Wewe nenda tu Pale Kumalija Hotel karibu na stendi ya mabasi Nyegezi. Utapapenda bure. Vyote hivyo vya muhimu ulivyosema vipo na ziada juu. Bei yao kama haijabadilika ni Tsh 20,000/= kwa chumba.
 
Ryan's bay hotel ,,
Hapa utakula upepo Wa ziwa.


Aspain hotel mtaa Wa uswahilini .
Hapa utapata kipozeo bure,

Gold_crest hotel
Hapa ni mkabala na Mwanza hotel bajeti yako ndogo
Aspen
newpark
chrismas tree
wande
DJ
 
Habari,
Ndugu zangu, Kwa wenye uzoefu na Hoteli za Jijini Mwanza naomba msaada wenu wa kujua hoteli nzuri, safi na yenye ulinzi jijini Mwanza. Breakfast na Chakula siyo muhimu kwangu. Gharama isiwe zaidi ya 30,000 TZS kwa siku. Pia kwenye vyumba ni muhimu kuwe na kiti pamoja na meza nzuri ya kuweza kufanyia kazi kwenye Laptop na hata kuandikia. TV pia sio muhimu sana lakini kama ipo, then hakuna shida. Cha msingi ni usalama, usafi, maji ya moto kwa ajili ya kuogea, kiti, meza nzuri na isiwe nje ya Mji.

Natanguliza shukrani.
Nenda Holmand hotel,kama utabook mapema wahi Sparrow hotel hutojuta huzo sehemu mbili
 
Kumbe tunatofautiana. Mi naulizia sehemu ya kulala ya elfu 20 ila natafuta sehemu safi yenye misosi mikali mchanganyiko.
 
Nenda Holmand hotel,kama utabook mapema wahi Sparrow hotel hutojuta huzo sehemu mbili
Mkuu Kabas, Kati ya hizo mbili ipi iko poa zaidi na location ni wapi? Nitakaa hapo zaidi ya wiki, hivyo nahitaji sehemu tulivu ili niweze kufanya majukumu yangu. Naomba usinichoke tafadhali nisaidie hizo taarifa Mkuu.
 
Back
Top Bottom