Kwa taarifa yako hawa jamaa hawaui nyoka. Nyoka anaitiwa hao polisi wa wanyama waje kumchukua au anaachiwa aishie. Kwa macho yangu nimeona jamaa wakimpiga picha nyoka tu halafu akatokea jamaa akamtishia mateke nyoka akabadili njia na kuelekea kwenye majani.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Yaani siku nilipoona nyoka akisindikizwa arudi majanini nilizima sigara. Nikabaki najiuliza ingechukua sekunde ngapi kwa wabongo kumponda kichwa yule nyoka.
Na pia nilipata picha kwanini nyoka wa Bongo wana usongo na hawana masihara na mtu.