Hongereni walimu, mishahara juuu!


na kodi je itashushwa?
 
Kiongozi wa chama cha waalimu ndugu Gratian Mkoba amesema hawatakubaliana na ongezeko la mshahara huo kwani seruikali haikuwashirikisha katika mchakato wa ongezeko la mshahara (ambao hakuutaja ni kiasi gani). Mkoba amesema licha ya mahakama ya kazi kuiamuru serikali kukaa meza moja na waalimu; Serikali imekaidi na kukaa bila kuwashirikisha waalimu na kupanga mishahara. "Serikali wameleta ubabe, sasa watatapambana na wababe wenzao" alisema Mkoba alipokuwa akihojiwa na Redio One leo asubuhi.
 
aaaahhhhhh kumbe ni tetesi........kwa serikali ya kina Mulugo hili jambo ni ndoto za ubunwasi
 

kwa hii figure, naomba niwe TOMASO tu kwa serikali yetu sikivu
 
Hebu subiri kidogo!! Kwani sasa hivi mwalimu wa shshada analipwa tsh ngapi?Hiyo nyongeza ya kufikia tsh 850,000/= itakuwa ni kiasi gani? Nikipata majibu naweza kupata picha ya ukweli wa tetesi hii!!

mungu siyo athumani yote yanawezekana mungu bariki tz.
 
DUH....
mishahara haiwezi kupanda kwa wizara moja tu au kada moja tuu ya walimu,
vp kuhusu graduates wengine wenye umuhimu kama madaktari nk..
tetesi zingine ni sawa na ndoto za mchana. mtoa mada jipange kutafuta habari si kuletewa tetesi.
:A S 39::A S 39::tape2::tape2:
 
Hebu subiri kidogo!! Kwani sasa hivi mwalimu wa shshada analipwa tsh ngapi?Hiyo nyongeza ya kufikia tsh 850,000/= itakuwa ni kiasi gani? Nikipata majibu naweza kupata picha ya ukweli wa tetesi hii!!

Laki 532,000
 

Mukoba hajitambui, mashavu yake!
 
Sio rahisi kwa srikali inayoogopa kukaa na kushauriana na walimu iwaongezee mapesa yote hayo! Kama ni kweli basi huo utakuwa ni mwanzo wa mapinduzi ya kifikra au ishara ya wakubwa kuogopa nguvu ya umma. Kama wameweza kupuuza amri ya mahakama hakuna kinachoweza kuwatisha! Lakini ngoja tusubiri, ya Mungu mengi!
 
Kwahiyo ongezeko la tsh laki 318,000/=Tsh? Mmh!Nitahitaji maelezo zaidi kuamini hiyo tetesi!

Mkuu nami siamini sana juu ya hii tetesi ila naomba kutoa ufafanuzi kidogo. Kwa sasa ngazi ya TGTS D1 ni 532000 na TGTS E1 ni 720,000 kabla ya makato yoyote, lakini kwenye bajeti mpya mishahahara yote itapanda, kwa hiyo labda mleta mada anamaanisha kuwa TGTS E1 itapapanda toka 720,000 za sasa mpaka hiyo 850,000. Kwa maelezo yake ni kwamba serikali itawapandisha daraja moja moja kila mwalimu sambamba na hongezeko la kawaida yaani wale wanaostahilikuwa daraja la C sasa wanapelekwa D na kuendelea hivyo mpaka mwisho, kama wakiamua wanaweza na sio ajabu kwa serikali kupandisha mishahara ya kada moja na kuacha zingine, walishafanya hivyo kwa kada za afya na sheria. Kituko kikubwa kipo wizara za Kilimo na Mifugo, watu waliosoma chuo kimoja kozi moja na wameajiriwa siku moja na wizara moja ila idara tofauti wanatofautiana mishahara kwa zaidi ya mara tatu. Kwa mfano ngazi ya TGS D1 kwa idara za ugani na mafunzo ni 520,000 wakati wa idara ya utafiti wanapewa 1,400,000 wakati wamesoma kozi moja na kituo chao cha kazi ni kimoja. Kwa serikali hii hakuna cha kushangaa.
 
walimu piganieni haki zenu, Ccm wala msiitegemee iwakomboe
 


Ooh!Kweli sikuwa nimeelewa vizuri, akhsante kwa ufafanuzi Mkuu!!
 
Kwa kusheherekea hilo mmeruhusiwa tena na kuwatandika viboko madenti wenu.
 
Afadhali waifu aongezewe nmgarawa kdogo!
 
Hebu subiri kidogo!! Kwani sasa hivi mwalimu wa shshada analipwa tsh ngapi?Hiyo nyongeza ya kufikia tsh 850,000/= itakuwa ni kiasi gani? Nikipata majibu naweza kupata picha ya ukweli wa tetesi hii!!

mwalmu wa shahada anayeanza anaanza na sh. Laki 5 na elfu 30 hv.
 
Kwahiyo ongezeko la tsh laki 318,000/=Tsh? Mmh!Nitahitaji maelezo zaidi kuamini hiyo tetesi!

Na hapo bado hawajafika 100% tulizohitaji, hiyo ni kama 60% tu, ndio maana CWT wameanza gogoro,refer to mkoba today at Radio One
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…