Hongera Wazalendo Industries ltd - Arusha kuweka mpango kutengeneza pikipiki

Hongera Wazalendo Industries ltd - Arusha kuweka mpango kutengeneza pikipiki

Kikiwo

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2017
Posts
2,018
Reaction score
1,107
Kutokana na gazeti la leo "Daily News" 31/10/2019 kuonyesha kwamba hawa "Wazalendo Industries Ltd" Arusha wana mpango kuanza kutengeneza pikipiki kutokana na kwamba sasa hivi wanatengeneza vifaa vya pikipiki, naona kweli watasaidia vijana wengi kupata ajira na kujikwamua katika maisha magumu.

Nilikua najiuliza, hivi Tanzania kwa mwaka tunaagiza pikipiki ngapi? Kwa sasa pikipiki zinatumika sehemu nyingi sana karibu nchi nzima kwahiyo soko lipo labda watashindwa wenyewe kama hazitakua na ubora na uimara.

Vichochoro vingi Bodaboda ndo mpango mzima kwamba zinatumika sana. Hawa jama wamekuja na wazo zuri sana.
Big up !
 
Inabidi kiwanda kikianza kufanya kazi pikipiki kutoka china ziongezewe kodi kwa 100% ili kukuza soko la ndani
 
Hongera zao sana, naamini ntawaungisha hata mbili tatu hivi ili kusapoti wazalendo wetu.
 
Back
Top Bottom