Chemagati
JF-Expert Member
- Apr 3, 2018
- 214
- 284
Katika kupambana kuenea kwa ugonjwa wa Corona, wameweka maji tiririka na sabuni ya kunawia ya kimiminika katika malango ya kuingia sokoni lakini kilichonifurahisha ni uhamasishaji wa wafanyabiashara katika soko hilo kwa wateja wao kunawa kabla hawajaingia sokoni kupata huduma, kwa hili la wafanyabiashara wadogo wakulima kusisitiza wateja, nawapa pongezi viongozi wa soko, pia viongozi wa jiji la Mwanza. Naamini hali ni hii katika masoko yote nchini.