Hongera Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kwa kutumia mapato ya ndani kujenga zaidi ya madarasa 78 matundu ya vyoo 119, Nyumba za walimu 14

Robert S Gulenga

JF-Expert Member
Jan 3, 2013
2,161
1,493
Ni wajibu wa viongozi kutekeleza majukumu waliyokabidhiwa ili kuwaletea maendeleo Watanzania, pale inapotokea Viongozi hawa wamefanya jambo nzuri ambalo yawezekana sehemu nyingine hawajafanya kwa kiwango hicho na wangeweza kufanya, basi ni muhimu viongozi hawa waliofanya vizuri tukawatia moyo na kuwapongeza kwa kazi nzuri waliofanya.

Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kwa kwa muda wa mwaka mmoja na miezi mitano kupitia mapato yao ya ndani wanayokusanya wameweza kujenga jumla ya vyumba vya madarasa 78 kwa Shule za Msingi na Sekondari, Matundu ya vyoo 199 kwa Shule za Msingi na Sekondari, nyumba za Walimu 14 pamoja na madawati 3302.

Miradi hii ni kwa sekta ya Elimu tu, ipo miradi mingine wametekeleza kama ya Afya , Kilimo, Barabara etc. Pia idadi hii ni nje ya vyumba vya madarasa Elfu nane (8000) vilivyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan ili kuhakikisha hakuna Mtoto mwenye sifa za kwenda shule anayekosa kwenda shule wala kukaa chiini kwa sababu ya upungufu wa vyumba vya madarasa

Hongera na pongezi saana kwenu uongozi wa Halmashauri ya Rufiji, kuanzia Mbunge wa Rufiji, Baraza la Madiwani, Menejimenti (Mkurugenzi wa Halmashauri na timu yake ya CMT), Watumishi wote wa Halmashauri kwa namna ambavyo mmeweza kufanikisha hayo kwa kuweza kubana matumizi ya kawaida na Fedha zinazokusanywa kuelekezwa kwenye Miradi ya Maendeleo.

Hongera pia uongozi wa Wilaya ya Rufiji kuanzia Mkuu wa Wilaya na timu yake yote kwa kusimamia vizuri utekelezaji huu wa miradi, watoto wetu wote wanasoma kwenye vyumba vya madarasa vyenye madawati ya kutosha.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan
View attachment 2479910
View attachment 2479920View attachment 2479921View attachment 2479924
 
Usiwe tomaso mkuu Aniko jr kwahiyo unahisi naweza andika uongo kwenye vitu viko wazi kama hivi?
Nani amekwambia muongo?kwani picha ilikuwa ina shida kuweka hapa na tukalinganisha ulichotuandikia?hukuona shule moja mkoani Dar,Wilayani Kinondoni imejenga matundu 5 ya vyoo na hayajakamilika kwa mil 29?picha inaleta maana na uisemacho.

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Ni wajibu wa viongozi kutekeleza majukumu waliyokabidhiwa ili kuwaletea maendeleo Watanzania, pale inapotokea Viongozi hawa wamefanya jambo nzuri ambalo yawezekana sehemu nyingine hawajafanya kwa kiwango hicho na wangeweza kufanya, basi ni muhimu viongozi hawa waliofanya vizuri tukawatia moyo na kuwapongeza kwa kazi nzuri waliofanya.

Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kwa kwa muda wa mwaka mmoja na miezi mitano kupitia mapato yao ya ndani wanayokusanya wameweza kujenga jumla ya vyumba vya madarasa 78 kwa Shule za Msingi na Sekondari, Matundu ya vyoo 199 kwa Shule za Msingi na Sekondari, nyumba za Walimu 14 pamoja na madawati 3302.

Miradi hii ni kwa sekta ya Elimu tu, ipo miradi mingine wametekeleza kama ya Afya , Kilimo, Barabara etc. Pia idadi hii ni nje ya vyumba vya madarasa Elfu nane (8000) vilivyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan ili kuhakikisha hakuna Mtoto mwenye sifa za kwenda shule anayekosa kwenda shule wala kukaa chiini kwa sababu ya upungufu wa vyumba vya madarasa

Hongera na pongezi saana kwenu uongozi wa Halmashauri ya Rufiji, kuanzia Mbunge wa Rufiji, Baraza la Madiwani, Menejimenti (Mkurugenzi wa Halmashauri na timu yake ya CMT), Watumishi wote wa Halmashauri kwa namna ambavyo mmeweza kufanikisha hayo kwa kuweza kubana matumizi ya kawaida na Fedha zinazokusanywa kuelekezwa kwenye Miradi ya Maendeleo.

Hongera pia uongozi wa Wilaya ya Rufiji kuanzia Mkuu wa Wilaya na timu yake yote kwa kusimamia vizuri utekelezaji huu wa miradi, watoto wetu wote wanasoma kwenye vyumba vya madarasa vyenye madawati ya kutosha.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan
Halmashauri nyingi zinafanya hayo Wala hakuna maajabu, mfano Tunduma TC wanajenga shule za magorofa kabisa..
 
Asee hayo madarasa yamejengwa wapi mkuu

Mbona hapa shule ya msingi azimio hapa ikwiriri haina vyoo

Shule ya msingi mbwela visiwan watoto wanajisaidia vichakan

Hapo muhoro shule ya msingi kuna matundu 8 tu idad ya wanafunz n 459

Yapo mengi mkuu tolea maelezo
 
Asee hayo madarasa yamejengwa wapi mkuu

Mbona hapa shule ya msingi azimio hapa ikwiriri haina vyoo

Shule ya msingi mbwela visiwan watoto wanajisaidia vichakan

Hapo muhoro shule ya msingi kuna matundu 8 tu idad ya wanafunz n 459

Yapo mengi mkuu tolea maelezo
Kuna muda Peramiho yetu sio lazima useme uongo usio na sababu, Shule ya Msingi Azimio wana miradi mpaka ya Taasisi nyingine ikiwemo Mamlaka ya Elimu Tanzania wametekeleza mradi wa matundu ya vyoo hapo Azimio wenye thamni ya TSH 40,000,000.00 (Achilia mbali madarasa), Serikali ya Awamu ya sita chini ya Mh. Rais Samia Suluhu Hassan imepeleka miradi ya Elimu kote kulikokuwa kuna uhitaji na upungufu.
Tusipende kusema uongo kwa vitu ambavyo hatuvijui, ukisema ukweli hupungukiwi na kitu bali unapata thawabu kwa Mwenyezi Mungu. Hujui hata Mbwela iko Halmashauri gani mkuu utaweza kusema ukweli?
 
Back
Top Bottom