Hongera sana Mh Magufuli kwa kuonyesha uzalendo kwanza miradi ya ujenzi nchini.

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,882
13,172
Wiki iliyopita Mh Dr John Pombe Mgufuli, Waziri wa Ujenzi, akiongea na Makandarasi wa Kitanzania, alipngea kitu ambacho mimi binafsi kimenifurahisha sana.
Bodi ya Usajili wa Makandarasi nchini CRB(Contractors Registration Board), ilifanya kikao cha majadiliano na makandarasi nchini.
Mh Dr Magufuli alialikwa kufunga mkutano huo na kutoa nasaha zake.
Ndipo Magufuli akasema wazi kuwa sekta ya ujenzi nchi karibu zote duniani huwa inamilikiwa na wajenzi wazalendo.
Magufuli alisema Mantiki ya sekta kumilikiwa na wazalendo ni mkakati wa kuhakikisha fedha yetu inabaki nchini.
Magufuli alibainisha kuwa yeye na serikali watahakikisha wazalendo watapewa kazi ili kufanikisha azma hiyo.
Hapo nampa big up Mh Magufuli na Dr JK kwa uamuzi huo maana ni uamuzi mgumu na umepigwa vita na watendaji kwa miaka mingi.
Nikiwa kama mjasiria mali nampongeza sana Dr Magufuli kwa uamuzi huo wa makusudi maana najua jinsi watendaji wabinafsi wanavyopindisha sheria ili kuwanyima wakandarasi wazalendo kazi za ujenzi.
Mfano hai wa hivi karibuni ni aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa TANROADS Ephraim Mrema na kazi alizotoa kwa wingi kwa wachina wake.
Kwa kutambua umuhimu wa uzalendo hongera sana Mh Magufuli.

MODS nimeiweka tena mada hii kama mada inayojitegemea ingawa mliiunganisha na majibu ya Mh Magufuli Bungeni, vitu ambavyo ni vitu viwili tofauti na havihusiani.
Tumpe moyo Mh Magufuli na viongozi wengine wanaoonyesha uzalendo kwa KUWAPENDELEA watanzania katika kuwapa miradi ili kukwa mua uchumi wetu na kubakisha fedha zetu nchini humuhumu.
Jana nimemsikia hata Mzee Mengi akitetea jambo hilohilo la uzalendo wa viongozi wetu kuwaweka WATANZANIA KWANZA katika kutoa kipaumbele cha kuendeleza rasilmali zetu nchini na tenda za kazi.
Katika nchi hii watanzania ndio first class citizens, na ndio jambo linaloongelewa hapa, na si vinginevyo.
 
Ndugu Magufuli ana uzuri wake kiasi sema siyo kiivyo mnavyojaribu kumsifia. Uangalifu unatakiwa kwenye kupima kauli zake.

Jambo la kukuza na kuwapa upendeleo Contractors na Consultants wazawa ni kilio cha muda mrefu sana kwenye sector ya Engineering au Ujenzi kwa jumla. Nd Magufuli amekuwa mgumu sana kuweka sera ya wazi ya upendeleo unaojaribu kuwajenga local Contractors na Consultants, na hii ni toka miaka ile alipokuwa waziri wa ujenzi kabla ya kuupata tena safari hii.

Huyu Nd Magufuli amekuwa alisema mara kwa mara eti local companies zianzishe JV (joint venture partnerships) ili ziweze kushindana na kampuni za nje zenye uwezo wa kifedha, kirasilimali nk kutoka nje. Hii kitu haikuwezekana kwa sababu lengo la partneships anazopendekeza zinatakiwa zitokane na utashi wa kibiashara na kimashirikiano za kampuni husika na SI ETI KWA AJILI YA KUSHINDANA NA KAMPUNI ZA NJE. Wazo lake zuri kwa nje kiutekelezaji ni gumu kiasi.

Alichotakiwa afanye ni kutenga baadhi ya kazi specifically zifanywe na wazawa tu! Kwa mfano kazi zisizozidi labda 3 billion shs ni kwa wazawa tu, na zinapozidi hapo kuwe na policy document ya kusubcontract labda 10% ya value ya contract kwa local contractors in case kazi hizo zinaenda kwa foreigners. These are some of my recommendations, for short term empowerment ya local experts.

Nd Magufuli amekuwa na maneno matamu ya kisiasa na hatua chache sana on the ground! Malipo yanayochelewa nayo yanaiingizia hasara kubwa serikali na yanawaathiri sana local contractors na consultants. Huyu Ndugu Magufuli anatoka povu akisema kama mtu anachelewesha kazi kwa KISINGIZIO CHA KUTOLIPWA hatapewa nyingine! This is madness, serikali kama haina uwezo isiwe na miradi mingi inayosimama na kuingiza hasara ya interest payments nyingi to the tune of 50billion per annum!

Tuwe wakweli
 
Ndugu Magufuli ana uzuri wake kiasi sema siyo kiivyo mnavyojaribu kumsifia. Uangalifu unatakiwa kwenye kupima kauli zake.

Jambo la kukuza na kuwapa upendeleo Contractors na Consultants wazawa ni kilio cha muda mrefu sana kwenye sector ya Engineering au Ujenzi kwa jumla. Nd Magufuli amekuwa mgumu sana kuweka sera ya wazi ya upendeleo unaojaribu kuwajenga local Contractors na Consultants, na hii ni toka miaka ile alipokuwa waziri wa ujenzi kabla ya kuupata tena safari hii.

Huyu Nd Magufuli amekuwa alisema mara kwa mara eti local companies zianzishe JV (joint venture partnerships) ili ziweze kushindana na kampuni za nje zenye uwezo wa kifedha, kirasilimali nk kutoka nje. Hii kitu haikuwezekana kwa sababu lengo la partneships anazopendekeza zinatakiwa zitokane na utashi wa kibiashara na kimashirikiano za kampuni husika na SI ETI KWA AJILI YA KUSHINDANA NA KAMPUNI ZA NJE. Wazo lake zuri kwa nje kiutekelezaji ni gumu kiasi.

Alichotakiwa afanye ni kutenga baadhi ya kazi specifically zifanywe na wazawa tu! Kwa mfano kazi zisizozidi labda 3 billion shs ni kwa wazawa tu, na zinapozidi hapo kuwe na policy document ya kusubcontract labda 10% ya value ya contract kwa local contractors in case kazi hizo zinaenda kwa foreigners. These are some of my recommendations, for short term empowerment ya local experts.

Nd Magufuli amekuwa na maneno matamu ya kisiasa na hatua chache sana on the ground! Malipo yanayochelewa nayo yanaiingizia hasara kubwa serikali na yanawaathiri sana local contractors na consultants. Huyu Ndugu Magufuli anatoka povu akisema kama mtu anachelewesha kazi kwa KISINGIZIO CHA KUTOLIPWA hatapewa nyingine! This is madness, serikali kama haina uwezo isiwe na miradi mingi inayosimama na kuingiza hasara ya interest payments nyingi to the tune of 50billion per annum!

Tuwe wakweli
Mkuu umenena kweli ingawaje mimi naona una miss ile message niliyotaka kuisemea hapa.
Magufuli amethubutu kuenzi utanzania kwanza, tofauti na watendaji wengi ambao wanasukumwa na maslahi binafsi katika kutoa kazi kwa watanzania.
Ule mfano wa Ephraim Mrema wa TANROADS nimeuweka makusudi, na jinsi alikuwa akifanya kazi kwa ridhaa yake au kwa maelekezo ya wakubwa wake na kugawa kazi kwa wachina kama hana akili nzuri.

Sekta zote za umma zingekuwa na msimamo huo nani angelalamikia rasilmali kwenda nje. Tukumbuke kuwa mtanzania anayepata tenda nchini anaajiri familia nyingi tu za kitanzania hivyo kupunguza tatizo la ajira.
 
Tumpe moyo Mh Magufuli na viongozi wengine wanaoonyesha uzalendo kwa KUWAPENDELEA watanzania katika kuwapa miradi ili kukwa mua uchumi wetu na kubakisha fedha zetu nchini humuhumu.

Sahihisho

Hii miradi ilibuniwa na awamu ya pili; ikawekewa mikakati na awamu ya tatu kwa kuuwa viwanda vyetu ili tupate misaada kwenye Integrated Roads Project zote. Kama tunawapa pongezi ni hao waliofanya kazi hiyo (Prof Lipumba mmoja wapo). Kama kawaida Magufuli alipenyezwa na mfumo kwa uhodari wa wizi wa kutumiwa na mfumo kwa kumlinda na tuhuma zote. (Usisahau nyumba za serikali zilipoishia na serikali imenyamaza). Itabaki kweli kuwa mbele ya wasiomjua Magufuli kwa kutumia vyombo vya habari kujitangaza watamuona ni keki kumbe nazi koroma.


Jana nimemsikia hata Mzee Mengi akitetea jambo hilohilo la uzalendo wa viongozi wetu kuwaweka WATANZANIA KWANZA katika kutoa kipaumbele cha kuendeleza rasilmali zetu nchini na tenda za kazi.

Nchi hii imepitia kwenye wakati mgumu sana

1. Mzalendo ni yule anayetoka CCM

2. Mzalendo ni yule asiyejali rasilimali ya taifa iwanufaishe wote. Anaiba na hakamatwi

3. Mzalendo ni yule anashika madaraka kwa hila

4. Mzalendo ni yule anaetoa misaada ya chakula badala ya jembe la kulimia mtu apate chakula.

5. Mzalendo ni yule mwenye maamuzi ya mwisho juu ya rasilimali za nchi lakini hajui kwa nini watu ni maskini

6, Mzalendo ni yule anyechangia chama cha CCM ili aendelee kufanya hujuma nyuma ya pazia

NI KWELI USHABIKI NI MAJALIWA LAKINI USHABIKI WA UPOFU UPOFU NI JANGA LA TAIFA.

Katika nchi hii watanzania ndio first class citizens, na ndio jambo linaloongelewa hapa, na si vinginevyo.

Katika nchi hii watanzania non citizens, wageni kwa kivuli cha uwekezaji ni first class citizen (wamasai wanaondolewa Loliondo kupisha first class citizens) na ndio jambo linaloongelewa hapa na linalotendeka kwa vitendo, na si vinginevyo
 
Back
Top Bottom