Ukipita huku mjini hata barabara ya Airport kuna mabango makubwa ya Hongera JK kwa kuchaguliwa M/kiti wa CCM. Mabango yamewekwa na Jerry Slaa lakini yana nembo ya manispaa ya Ilala. Swali ni je, fedha ni za Slaa au za Manispaa? Je, mabango yamelipiwa kodi? Kama kuna diwani wa upinzani Ilala tafadhali fuatilia hatuwezi kukubali fedha za walipa kodi zitumike kwa mambo binafsi.