Hongera Salva Kiir - Rais wa Sudan Kusini

Hongera Salva Kiir - Rais wa Sudan Kusini

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
13,219
Reaction score
20,565
Katika kipindi kifupi cha chini ya mwaka mmoja tangu nchi yako ipate uhuru tarehe 9/7/2011 juhudi zako za kuwaondolea umaskini wananchi wako tumeziona;
  1. Kukuza kilimo na kuondoa njaa kutokana na vita vya muda mrefu - HONGERA
  2. Elimu na kujenga uzalendo wa wananchi wako - HONGERA
  3. Kuzuia wizi wa mafuta uliokuwa unafanywa na Sudani Kaskazini - HONGERA
  4. Mradi wa ujenzi wa reli na bomba la mafuta kutoka Juba hadi Lamu Kenya - HONGERA
Hivi Tanzania tunajifunza nini kutoka nchi hii changa?
  1. Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya - ZERO
  2. Mpango wa reli kutoka Mtwara hadi Mbamba Bay (Mtwara Corridor) - ZERO
  3. Mabasi yaendayo kasi DSM - ZERO
  4. Kuimarisha reli ya kati kwa kuwa na treni zinazotumia umeme - ZERO
  5. Reli ya kutoka Tanga hadi Musoma - ZERO
  6. Kilimo kwanza - ZERO
  7. Elimu ya sekondari -ZERO
  8. Maji jijini DSM - ZERO
  9. Michezo - ZERO
  10. Usalama wa raia kutoka kwa polisi - ZERO
  11. Kuzuia rushwa - ZERO
Wana JF wapi Tume ya MIpango! Wapi tunakokwenda!
 
... dah, nilidhani unamzungumzia Salva Rweyemamu kumbe ufanno tu wa majina!!
 
Si ni mafundi wa kusimamia ujenzi wa mabanda ya kuku, shule za chekechea na vitu vya namna hiyo ambapo wakati wa uzinduzi wake makamo wa rais ambaye anakuwa amelipwa hela nyingi za per dm yeye na wake zake pamoja na msafara wake wenye gharama mara 100 ya mradi anaouzindua!

Utashangaa mradi wa ofisi ya kijiji anayozindua huyu makamu wa rais wa uzinduzi huwa haina hata thamani kulinganisha na gari aliyofika nayo hapo kwenye uzinduzi!
 
Hayo yote uliyoompa hongera mzee wa pama,,tunayathibitishaje?
 
Hayo yote uliyoompa hongera mzee wa pama,,tunayathibitishaje?
Jana kwa mfano alikuwa Lamu Kenya ambako Rais Kibaki alikuwa anazindua ujenzi wa bandari kubwa ambayo itakuwa inatumika kusafirisha bidhaa kutoka Sudan Kusini kwa kutumia treni iendayo kasi na mafuta yatakayokuwa yanasafirishwa kwa bomba linalotarajiwa kujengwa.
 
Wa Sudan wengi wapo Canada, Marekani na USA na walipelekwa huko na kikundi cha John Garang ambaye alisomea hapa Tanzania huko Tanga shule ya Magamba. NIna hakika wakirudi hao wataalam waliopelekwa nje kusomea fani mbali mbali ile nchi ina take off mapema na mabenki ya Kenya na makampuni yao yameshakimbilia Sudan.

Sisi alienda Kikwete tu kwenye kuapishwa huyu bwana na sidhani kama alibeba na delegation ya kina Mengi 's na Bakhresa's kuwatambulisha huko.Hamna sehemu ambazo zina biashara nzuri kama ambazo zinazotoka kwenye machafuko. Uliza Mabenki na makampuni mengine yanavyopata faida huko Angola.
 
Back
Top Bottom