Hongera Radio Maria Tanzania

Balantanda

JF-Expert Member
Jul 13, 2008
12,476
4,752
-Wakuu,naomba kuitumia nafasi hii kuwapongeza Radio Maria Tanzania kwa utaratibu wao wa kurusha matangazo ya moja kwa moja kupitia mtandao(Internet)..Binafsi wamekuwa wakinifanaya nijihisi niko nyumbani Tanzania,kwani pamoja na kuniburudisha pia nimekuwa nikipata taarifa mbalimbali za yale yanayoendelea nyumbani Tanzania(kupitia haya matangazo yao ya moja kwa moja)..Hongereni sana Radio Maria Tanzania kwa kazi hii nzuri.

-Ni vizuri pia Radio nyingine zilizopo Tanzania kama TBC,STZ,RFA,Radio One,Clouds FM,KISS FM na nyingine nyingi zikaanza utaratibu huu wa kurusha matangazo kwa njia ya mtandao kama ilivyo kwa Radio Maria Tanzania ili watusaidie sisi tulio nje ya Tanzania kujua kile kinachoendelea nchini kwetu(japo mengi tunayapata kupitia Jukwaa hili tamu-JF) ikiwa ni pamoja na kupata burudani safi ya Muziki.

-Hongereni sana Radio Maria..Waweza kuisikiliza Radio Maria Tanzania kwa kugonga link hii hapa chini:-

http://www.dullonet.com/maria.php
 
Mods naomba heading iwe Hongera Radio Maria Tanzania badala ya Hongera Rdio Maria Tanzania kama inavyoonekana hapo juu...Pamo jah
 
Ni nzuri sana, nimeicheki hapa, sikujua kabla
Nashukuru sana Mkuu Balantanda for info na link pia
Najinoma na news nzuri hapa kutoka Radio Maria
 
Imagine nipo home tz haswaaa afu siju hii kitu ya redio maria kwenye net!!! thanks man!!!
 
Hii redio ni Kongwe na haina mpinzani kwa baadhi ya maeneo.

Hasa audibility yake ni super!..Lkn nikushukuru Mkuu Balantanda kwa kunijuza juu ya kupatikana kwao mtandaoni!..Krismas itakuwa njema hapahapa
ofisini..!

Big-up to these guys!
 
Ni nzuri sana, nimeicheki hapa, sikujua kabla
Nashukuru sana Mkuu Balantanda for info na link pia
Najinoma na news nzuri hapa kutoka Radio Maria

Unasikiliza kipindi cha MVIWATA siyo..hongera sana Radio Maria,wako juu sana hawa watu
 
Lakini Mkuu Balantanda, Asinus asinum fricat ndo Kitu gani hii tena?
Nadhani umeiandika kwa nia ya kuwasiliana na sisi!
 
hata mimi naungana na kakangu PJ, would love to know maana ya hiyo signature yako

Ni msemo tu wa lugha ya kilatini meaning:- The ass rubs the ass(Conceited people flatter each other about qualities they do not possess)
 
-Wakuu,naomba kuitumia nafasi hii kuwapongeza Radio Maria Tanzania kwa utaratibu wao wa kurusha matangazo ya moja kwa moja kupitia mtandao(Internet)..Binafsi wamekuwa wakinifanaya nijihisi niko nyumbani Tanzania,kwani pamoja na kuniburudisha pia nimekuwa nikipata taarifa mbalimbali za yale yanayoendelea nyumbani Tanzania(kupitia haya matangazo yao ya moja kwa moja)..Hongereni sana Radio Maria Tanzania kwa kazi hii nzuri.

-Ni vizuri pia Radio nyingine zilizopo Tanzania kama TBC,STZ,RFA,Radio One,Clouds FM,KISS FM na nyingine nyingi zikaanza utaratibu huu wa kurusha matangazo kwa njia ya mtandao kama ilivyo kwa Radio Maria Tanzania ili watusaidie sisi tulio nje ya Tanzania kujua kile kinachoendelea nchini kwetu(japo mengi tunayapata kupitia Jukwaa hili tamu-JF) ikiwa ni pamoja na kupata burudani safi ya Muziki.

-Hongereni sana Radio Maria..Waweza kuisikiliza Radio Maria Tanzania kwa kugonga link hii hapa chini:-

http://www.dullonet.com/maria.php

Mzee nakuunga mkono na mguu katika hilo. Hawa bwana wananikosha sana. Kuna wakati huwa nashangaa kulikoni hatuwezi kuzipata TBC, Radio one au Radio free Africa (ambayo wanarusha recorded habari)? Lakini pia kuna radio nyingine ya kibongo, though yenyewe ni kwa ajili ya mziki tu, but inaweza kukufanya ujisikie upo home: http://www.bongoradio.com/mediaplayer.html
 
Back
Top Bottom