Hongera Mwigulu na Easter Bulaya

Hongera Mwigulu na Easter Bulaya

Sio mwigulu au Estar peke yao,yeyote alie na akili timamu hawezi kuona upumbavu waliofanya polisi alafu akaupongeza,huwezi ona mtu aki mdhalilisha mwana adamu mwenzako alafu ukafurahia,kama hawa polisi watakuwa wanapongezwa kwa haya ina maana kuna siku watakufanyia wewe au ndugu yako na je utafurahia.
 
Napenda kuwapongeza viongozi hawa wawili kwa msimamo wao wa kuacha ushabiki na kutetea haki za binaadam na kukiri hadharani kutokubaliana na kile kilichofanywa na police dhidi ya Profesa Lipumba hapo jana

Kwa hili na mimi nawapongeza sana. Hawa kweli wanafaa kuwa viongozi!
 
Mwigulu alinacha mambo yake ni mtu mzuri sana, kitu kimoja tu ninachomsifu anauwezo wa kuongea jambo hadharani bila kuisubiri wanasisiem wampe ruksa
 
Ule waliofanya polisi ni ujinga...especially maneno waliokuwa wakitamka..ni ujinga,...kudhibiti wapinzani sio kule...na lile koa lakuwambia watu waingie polisi kwa kichura chura ni la kipumbavu sana..inabidi ukawa wasimame kiume hu ni ujinga
 
Mwigulu kama wana ccm wengine, their hipocrity. Hata ulivyomuona jana wakati anacomment anajiumauma! Anataka aonekane neutral while naye anatangaza amani huku kaficha panga mgongoni
 
Napenda kuwapongeza viongozi hawa wawili kwa msimamo wao wa kuacha ushabiki na kutetea haki za binaadam na kukiri hadharani kutokubaliana na kile kilichofanywa na police dhidi ya Profesa Lipumba hapo jana
Bulaya Kamanda! Huyo Mzee wa Maskafu a.k.a Mwigulu msaka tonge mbona hakutoa maelezo mazuri kama ya Kamanda Bulaya? Yeye nikujiumauma na kukodoa macha alitaka kujiunga na Makinda waunde TUME! Hatuzitaki tena tume zakifisadi bora KIPORO kuliko tume
 
Issue kama hizi ndio Mwigulu hujichukuliaga point kujijazia ili afike magogoni, I am sure haitoki Moyoni hiyo. Na ana bahati kweli huyu Mwigulu, maana kila usanii akiufanya basi Wapo mambumbumbu wanaouamini.

Kwa Ester Bulaya naamini, yule ni 49% Ukawa!
 
Kauli za wanasiasa si hoja sana. Tatizo kubwa kweli tulilo nalo ni kufa kwa ustaarabu katika uongozi wa nchi. Walio madarakani wanaonekana kama miungu - wanaweza kuagiza mtu adhalilishwe, auawe au atiwe kilema na polisi wanatekeleza kama agizo la kawaida! Na ikaishia hapo! Rejea polisi waliowauwa Zona na Mwangosi.

Halafu, tuseme wazi kabisa: polisi hawatakiwi kupiga watu mahali pasi po na mapigano. Ni dharau kubwa sana kupandisha watu kwenye gari na mateke na virungu.

Kwa Lipumba, ujumbe aliopewa na watawala ni: "you're nobody; we can do anything to you and there's nothing you can do about that!". Huo ndio mtizamo wa watawala wetu kuhusu watu walio nje ya "kundi lao" linalomiliki nchi hii. Ndivyo wanavyouona mfumo wa vyama vingi. Ni ama mnawasujudia ama mnaadhirika. Na sisi wananchi katika wingi wetu bado hatujaiona hatari iliyo mbele ya macho yetu: we still entertain dancing with the devil.
 
Opportunist aka attention seekers ...
Napenda kuwapongeza viongozi hawa wawili kwa msimamo wao wa kuacha ushabiki na kutetea haki za binaadam na kukiri hadharani kutokubaliana na kile kilichofanywa na police dhidi ya Profesa Lipumba hapo jana
 
Natamani hao polisi waburutwe mahakamani


Kwa unyama huu wa Jeshi la Polisi. Itawasababisha Wananchi kuachukia Polisi. Wanashinda kuelewa kuwa nao wanaishi mitaaani na tupo nao nyumba moja au mtaa mmoja.

Sasa ikitokea bahati mbaya Askari polisi jirani yako anapigwa na vibaka au majambazi mtu mwenye akili timamu hawezi kumtetea au kumsaidia. Kwani wanajenga uadui na wananchi.

Hiki kipigo hakipashwi kuwa kimefanyika Tanzania tunaypimba eti NCHI YA AMANI, NCHI YA DEMOKRASIA!!!!!!!!!!

Labda kingefanyika nchi ambazo hazia amani.

Lakini mwisho wao utafika wa kuacha kuwatumikia hao mabwana. Watakuja juta.

Sijui wataweka wapi sura zao.


ATTACH=CONFIG]222568[/ATTACH]

View attachment 222572

Askari na Mwangosi.JPG

usingizi_(1).jpg

Ofisi ya CCM 01.JPG

profilepic 2015.JPG



MIZAMBWA
INANIUMA SNA!!![
 
Natamani hao polisi waburutwe mahakamani


Mkuu siyo kufikishwa Mahakamani kuvuliwa vyeo vyote walivyo navyo na kufungwa na baada ya kifungo kupigwa marufuku kujihusisha na masuala ya kijamii au kukaribia katika mikusanyiko hawa ni hatari kuliko shetani
 
Nadhani Mwigulu anatafuta kufukuzwa ccm, Ni marufuku kwa mwanaccm kusema ukweli hadharani hata kama kwa kufanya hivyo anadhulika...!!!!

BACK TANGANYIKA

Kwakweli nchi yetu haitaki mtu mkweli has a kwa wakati huu wa uchaguzi mtu akisema ukweli wanadhani anatafuta umarufu
 
ID za JF za mwigulu zote zipo active! huyu mwigulu sitakaa nimuamini maisha yangu na ya ukoo wangu yote yaliobakia humu duniani mpaka pale atakapojitokeza hadharani na kutuambia kwa nini alimchinja mbwambo na chain saw, kwanini alimmwagia tesha tindikali na kumbabika kwa watu wengine wasio na hatia, kwanini aliingiza video ya lwakatare sauti na kumbamkia ugaidi, kwa nini aliturushia bomu kule arusha! najua hatakiri hadharani lakini Mwenyez Mungu atamsambabishia aibu atakiri kwa vitendo tu! days are numbered

Nakubaliana na wewe mkuu kwa asilimia mia moja,huyu jamaa ni gaidi na wala hana chembe yoyote ya ubinadamu,kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi ndio anajifanya kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu.Sitakaa nimuamini huyu mtu.
 
Back
Top Bottom