Hongera Makamu wa rais kwa kiingereza kizuri

Mkuu bado hujanielewa huyo mkorea hakusomea udaktari wake kwa kiingereza,sisi ni tofauti masomo yote ni kiingereza na bado ufike hadi PhD bado hujakiielewa hapo ndipo penye swali badala ya kusema ni lugha kama lugha nyingine tukosoe mfumo wa kutumia lugha mbili kufundishia kitu kinachowachanganya wanafunzi.
Mkuu, hapo ndipo tulipoteleza kama Taifa. Huwezi kuwa na lugha mbili za kufundishia. Nimekuelewa mkuu na kama ulinipata ni kwamba tatizo liko kwenye msingi. Msingi wa lugha hujengwa katika elimu ya awali na msingi, sisi tunajenga kiingereza chetu kwenye msingi wa kiswahili ambao tumewekewa kwenye shule zetu za chini. Ukweli hatutaweza kuimudu lugha hii kwa njia hii. Na haifai kwa mtanzania kushindwa kukijua kiingereza ukitilia maanani kwamba Tanzania ni moja ya nchi za kiingereza. Maana mataifa yamegawanyika katika matabaka ya lugha: Nchi za kifarasa, Kiarabu, kireno, n.k.
 
Katika Kiswahili hakuna kitu kinaitwa LUGHA YEYOTE. Tuna kitu kinaitwa LUGHA YOYOTE.

Kiongozi yeyote anayeshindwa kuzungumza Kiingereza kwenye hafla rasmi lazima liwe ni suala la kujadiliwa kwa sababu hakuna aliyemlazimisha kuzungumza Kiingereza. Angeweza kuzungumza kwa Kiswahili na kutumia Mkalimani na hakuna mtu yeyote ambaye angemshangaa mbali ya kumsifu. Kama Kiingereza hukimudu, kwa nini ung'ang'anie kuongea. Kwa nini usitumie lugha unayoimudu!
Hapo umenena mkuu.
 
Back
Top Bottom