Mwaka mmoja uliopita niliandika ujumbe na kusema Lema badilika na kwa kweli ni lazima niseme Lema kabadilika. Lema wa sasa ni mbunge anayeangalia maslahi ya mji wa kibiashara wa Arusha, ni kiongozi wa Arusha yote sio wana Chadema pekee, na Lema sasa anatangaza Arusha kwenye mikutano AICC, Madini na vilevile kwenye utalii. Lema wa sasa ana nguvu zaidi kuliko Lema wa miaka miwili iliyopita kwasababu Lema wa sasa ni Lema wa maendeleo ya Arusha. Wafanyabiashara sasa wanampenda Lema baada ya kugundua si adui na anawajali. Inawezekana ni umri au kufuta mawazo lakini ni lazima tumpe credit Lema kwa kubadilika. Kabla Lema hajawa mwanasiasa alikuwa mfanya biashara bna tunataka Arusha iwe kama Moshi chini ya Ndesamburo yaani ya kibiashara, safi, uchumi unaokuwa na no drama. Kila mtu Tanzania mwenye kuelewa anaelewa kuwa Moshi ni kati ya miji inayoendeshwa vizuri Tanzania na tunataka Arusha iwe ya Kibiashara.